Lowassa: Tuko tayari kuingia vitani na Malawi...

Lowassa: Tuko tayari kuingia vitani na Malawi...

....Jaribu kuwa MZALENDO kwa kulitetea TAIFA lako kwa Njia zozote iwe kwa Diplomasia iwe VITA, yote JIANDAE NAYO...

Sio Unalaumu laumu kama Si MTANZANIA vile.

Hapo hakiangaliwi CHAMA, Dhehebu, Kabila, Rangi ,.. HAPA NI KUITETEA TANZANIA NA MIPAKA YAKE....

via M4C

Kubali tu kuwa Lowassa amekurupuka!
 
Katu Wazanzibari hawatoingia vitani kwa kuitetea Tanganyika, Nendeni WaTanganyika mkawanyanga'nye Wamalawi Ziwa lao, maana hamtajiwi mafuta na gasi mnatoka kipovu.

Ila wanajitayarisha kuikomboa Zanzibari, mkimaliza Malawi nendenii Muipige Zanzibar maana na wao wanataka Ardhi yao, ina mafuta na gesi nyingi.
 
Umasikini tuliofikia hapa ni juu ya vita vya Uganda. na ni vita ya JK Nyerere na kwa kipindi kile hazina ilikuwa na hela tofauti na leo hii fedha iko mifukoni mwa nyang'au weusi. natahadharisha hata hiyo vita ikipiganwa wiki mbili Watanzania watachoka kuliko Zimbabwe. Lowasa apotee zake.
 
Katu Wazanzibari hawatoingia vitani kwa kuitetea Tanganyika, Nendeni WaTanganyika mkawanyanga'nye Wamalawi Ziwa lao, maana hamtajiwi mafuta na gasi mnatoka kipovu.

Ila wanajitayarisha kuikomboa Zanzibari, mkimaliza Malawi nendenii Muipige Zanzibar maana na wao wanataka Ardhi yao, ina mafuta na gesi nyingi.
Mwana akililia wembe....................................................
 
Kauli hii ya matumaini na ya kujuvunia, tulitarajia itolewa na JWTZ au Rais, lakini hata hiuvyo sio mbaya!

Asante kamati ya bunge!

Unga mkono JWTZ kulinda mpaka ya nchi yetu!

Nitalinda mipaka ya nchi yangu ya Zanzibar na sio ya Tanganyika hainihusu.
 
Hakuna taifa lolote duniani ambalo litakuwa tayari ku-sacriffice primary interest kirahisi
Katika Diplomasia inajulikana Primary Interest za Taifa lolote ni

1: Ardhi ndani ya mipaka inayotambulika kimataifa
2:Raia wakndani ya mipaka pamoja na Raia wake walioko nje ya nchi n.k

Hizi ni interest ambazo taifa lolote lipo tayari kutumia millitary option.

Bernard Membe alitoa ujumbe ambao ni thabiti kabisa na mara zote nimesema Membe anafanya kazi yake kama wwa Mambo ya Nje vizuri na anafuata principle zote za diplomasiapamoja na mapungufu yake ya hapa na pale.Alionyesha maturity,patriotism na intellectual capacity alipokuwa akijadili hili la Malawi


hapo red n bolded jwtz ikatokea wameitungua ndege inayovinjari anga la tz huko ziwa nyasa kwa ajili ya utafiti wa gas na mafuta. ndani ya ndege unakuta rubani mwingereza na mtaalam wa utafiti ni myahudi mathlani, inamaana tunaweza ingia vitani na haya mataifa?
 
hapo red n bolded jwtz ikattokea wameitungua ndege inayovinjari anga la tz huko ziwa nyasa kwa ajili ya utafit wa gas na mafuta. ndani ya ndege unakuta rubani i mwingereza na mtaalam wa utafiti ni myahudi mathlani, inamana tunaweza ingia vitani na haya mataifa?
Sheria za kimataifa zitazingatiwa.....

Pia niliposema Raia walioko nje namaanisha kuna Ubalozi ambao unashughulikia Interest za the sending state kwa nchi husika.Pia Ubalozi una kinga hata polisi hawatakiwa kuvamia tu itakuwa ni kama umeingilia nchi nyingine kinyume na sheria.Vita inaweza kutangazwa

Kama watu wanafanya utafiti lake Nyasa bila kuzingatia sheria on personal capacity sheria za kimataifa ndizo zitakazoamua.Kama Ndege ni mali ya Malawi au watu wenyewe wametumwa na serikali ya Malwi pia hii itakua a very serious case kama ilivyo hivi sasa na inaweza kupelekea vita.Kwenye sheria za kimataifa hii ni act of aggression.Sehemu ambako uhalifu unaanzia wakuwa labelled aggressors
 
Inapotakiwa maamuzi magumu yatolewe haitakiwi kumung'unya maneno and EL did good.
 
vita vya adui fisadi bado havijaisha mkuu
Vita vimeisha siku nyingi mkuu. Rais kama anatangaza hakuna cha Kesi ya Rada wala Rushwa yake na Waziri wake wa sheria anatamka Bungeni kuwa mjadala huo umefungwa kama ule wa Richmond unaelewa nini hapo?
Jibu ni kuwa hakuna tena vita ya adui Fisadi. Ni kama zile siku 90 za magamba kujivua, kila zikiisha inaongezwa sifuri moja mbele kuwa tulisema siku 900 na itaendelea hivyo bila ukomo.
 
hapo red n bolded jwtz ikatokea wameitungua ndege inayovinjari anga la tz huko ziwa nyasa kwa ajili ya utafiti wa gas na mafuta. ndani ya ndege unakuta rubani mwingereza na mtaalam wa utafiti ni myahudi mathlani, inamaana tunaweza ingia vitani na haya mataifa?

Come again!
 
Vita inagharama kubwa sana. Tusikimbilie huko kila jitahada za kidiplomasia zifanyike ili kuepuka kuingia vitani na ndugu zetu majirani. Isije kuna wakubwa wako nyuma na mgogoro huu ili hatimae tukiingia vitani wa wake pemebeni wakifuhahia biashara yao ya silaha kupata soko kufuatia vita hivi. Waswahili tuna usemi wetu usemao " Vita vya panzi furaha ya kunguru." Vita tuliyonayo watanzania dhidi ya maadui wanne ujinga,umaskini, maradhi na ufisadi inatosha. Tupigane kwanza hii. Si jeshi tunalo wa kupambana na adui hawa hasa adui ufisadi. Narudia tena jitihada za kidiplomasia zifanyike na kila upande uwe na ushahidi wa ya yale yanayolalamikiwa kutoka pande zote mbili.Tushindane kwa hoja ili tuiepuke vita hii.
 
Colleagues,
The political situation we are in now leads to our leaders to give provoking announcmenets that have great implications to our nation. They think they will be safe (hasa kwa chama tawala ambacho muelekeo wake hauonekani) but it will not be the case. We pray that this country remains safe with smooth transfer of power from one party to another. My worry is that in state of insecurity due to war-there will be no constitutional review, no peaceful general election (may even be postponed and all those guys continue to steeling). Let's be watchful!!!
 
Lowasa alikuwa anajitafutia umaarufu kwani hili sakata sio la leo baada ya kusikia washindani wake Sitta na Membe wametoa kauli na kupata sapoti na yeye akapata cha kuzungumza ilitakiwa mara baada ya kupatikana kauli za viongozi wa malawi wangekaa kuishauri serikali na kutoa tamko sio baada ya
kumbuka wanasiasa wote duniani huwa wanazungumza mambo wanayopenda kusikia wananchi
 
Sheria za kimataifa zitazingatiwa.....

Pia niliposema Raia walioko nje namaanisha kuna Ubalozi ambao unashughulikia Interest za the sending state kwa nchi husika.Pia Ubalozi una kinga hata polisi hawatakiwa kuvamia tu itakuwa ni kama umeingilia nchi nyingine kinyume na sheria.Vita inaweza kutangazwa

Kama watu wanafanya utafiti lake Nyasa bila kuzingatia sheria on personal capacity sheria za kimataifa ndizo zitakazoamua.Kama Ndege ni mali ya Malawi au watu wenyewe wametumwa na serikali ya Malwi pia hii itakua a very serious case kama ilivyo hivi sasa na inaweza kupelekea vita.Kwenye sheria za kimataifa hii ni act of aggression.Sehemu ambako uhalifu unaanzia wakuwa labelled aggressors

Ben I salute you brother! You have never lost your objectivity in your approach to issues. Emotions have never reigned or impaired your brilliance and courtesy. Membe has exhibited rare diplomatic credentials that many of our leaders are desperately starved of and are envious. We may disagree on some of the issues or have divergencies but he is performed better by a country mile. That is jot saying that Membe is an angel or that he cannot err here or there but for a fact, you dont spit fire on issues that can be nipped in the bud without engaging the exchequer or shed blood of innocent people in the name of patriotism that is intended to gain a political mileage.

Thank you for seeing through the Committee's juvenile approach to this matter.
 
Lowasa alikuwa anajitafutia umaarufu kwani hili sakata sio la leo baada ya kusikia washindani wake Sitta na Membe wametoa kauli na kupata sapoti na yeye akapata cha kuzungumza ilitakiwa mara baada ya kupatikana kauli za viongozi wa malawi wangekaa kuishauri serikali na kutoa tamko sio baada ya
kumbuka wanasiasa wote duniani huwa wanazungumza mambo wanayopenda kusikia wananchi

You are absolutely right. Tatizo hapa ni kuona mahasimu wake wametoa kauli na yeye akona ataachwa nyuma katika hili na ndiyo maana hakulitoa hili kama mchango wake katika hotuba ya bajeti ya Waziri. Kama ni hivyo basi atachoka maana hawa jamaa hawakurupuki na haya yataendelea katika kila topical issue.
 
Kwanza nawaomba waheshimiwa wana JF katika kipindi hiki cha mgogoro kati ya Tanzania na Malawi tulete thread na kuchangia kwa kuzingatia maslahi ya Taifa. Tuache SIASA na maslahi.

Pili naomba michango yenu kwa kuzingatia maslahi ya Taifa, ni nani anayestahili kutangaza kwa mara ya kwanza uwezo na nguvu yetu ya kijeshi? Membe alizungumza na kuionya Malawi baadae akaja Lowassa akasema tuko imara na tayari kwa vita! Sasa suala la nani atangaze ni nyeti sana na lina sababau nyingi na athari zake kitaalamu.
 
Back
Top Bottom