Lowassa: Tuko tayari kuingia vitani na Malawi...

Lowassa: Tuko tayari kuingia vitani na Malawi...

Membe na Lowassa wamevunja katiba kwa kutamka mambo ya vita. Ibara ya 44 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 toleo la mwaka 2005 inasema...'Rais anaweza kutangaza kuwapo kwa hali ya vita kati ya ya Jamhuri ya Muungano na nchi yoyote'.

Viongozi wetu waepuke kutamka maneno yanayoashiria vita. wanaweza kujibu hoja bila kuonyesha dalili kwamba vita vyaweza kutokea.

Kama Raisi ni Mdhaifu na asiyejali kitu na aliyejaza Pesa pale Ikulu Unadhania Wengine wenye Uchungu na Nchi Watakaa Kimya.... We Kaa na Vifungu Vyako... Raisi Pengine yupo kwenye Mfungo hataki kuondoa Udhu kwa Kusemea Umwagaji Damu....
 
DUNIANGUMU JR
Nimeshindwa kusoma font zako zinaniumiza macho, ngoja wengine wasome wafafanue unachoeleza
 
Last edited by a moderator:
Suala hili la uvamizi liko mahakamani, si vema sana kulizungumzia tutaingilia uhuru wa mahakama. Wazambia wanadai mambo makubwa sana ambapo taifa Kwa Sasa haliwezi kuwatimizia..

Wazambia tena mbona sikuelewi Eng. Y. Bihagaze, imebidi niulize tu hata kama hili suala lipo mahakamani na wewe pia nijibu
 
Last edited by a moderator:
Nimeshindwa kusoma font zako zinaniumiza macho, ngoja wengine wasome wafafanue unachoeleza

Kama umegundua font zinaumiza macho si ungerekebisha mwenyewe hapo kwa kuongeza Font size au umenunua zile Apple - laptop ambayo ina application complicated kidogo
 
kuna ajali iliotokea tabora watu wamekufa lakini bus lilikuwalimejaa kama watu 90 police wapo lakini hawafanyi kazi itakuwa hao wanajeshi ....
si bora waliache hilo ziwa waje waturudishie dhahabu zetu wanazowapa wazungu nani atakubali akapigani kwa faida ya wachache lowasa anajuwa atapata nin cha kumnufaisha

Kwa maana nyingine unatuambia kwamba inabidi tuangalie faida tuliopata kutoka ziwa Nyasa tangu kupata uhuru tukilinganisha na gharama za vita na kama gharama za vita zikiwa kubwa tuachane na mpango wa vita (mie napita tu)
 
haahaa yaani tukapigane kabisa na malawi! yesu wangu kwa kisa gani hicho tunagombea Kisima cha mafuta ua Mgodi wa Almasi.
acheni hizo Miezi 18 ya shida mara baada ya vita na Uganda haijaisha. ACHENI KUTULETEA SHIDA JUU YA SHIDA KWA KIPANDE CHA ARDHI.
 
Ni Lowassa na nani wako tayari kuingia vitani Malawi?
 
Ni Lowassa na nani wako tayari kuingia vitani Malawi?[/QUOTE....kaka lowasa ni luten wa jeshi mstaafu anajua vyema anachokiongea,,zaidi ni mwenyekiti wa kamati husika,ya ulinzi na mambo ya nje,,sauti yake ina nguvu,ujumbe wake ni mzito kwa maana ya nafasi yake,,pm mstaafu nithreat,na vita haianzi tu na milio ya risasi na mizinga,,membe alipiga risasi,,hawajajibu lowasa kasindilia kombora,,wakileta za kuleta,,unapigwa wimbo wa taifa amiri jeshi anaisogelea mic anazungumza maneno machache sana,,,wakati anaokota glasi anywe maji,,vijana wanaizingra lilongwe,,,bulantaye tayari meya atakuwa kamanda wa jeshi,,,yule mamaatakimbilia south africa kwa hifadhi ya muda,,kuelekea marekan,,,tutamelekacapt john komba,,awaimbie kwaya,na kuwa rais wa muda mkulo waziri mkuu mzee chipaka makamu wa rais ,,wamalawi watatuita wakombozi,,,,,heshma mbele,,,,weee subiri,,cheza na tpdf wewe,,,
 
Siamini hili; hii ndio sababu ya kwanini siamini anafaa kuwa Rais. Anazungumzia vita leo? kwa lipi hasa? wanataka kuescalate vitu bila sababu ya msingi. Hafai kuwa Amiri Jeshi Mkuu. Kama hii ni sababu ya kwenda vitani basi tumekosa viongozi kweli kweli!

Mwanakijiji,
watu kama nyie ndio mnawaomba wake zenu samahani mkiwafumania wake zenu wanapigwa bao na wanaume wengine, yaani kwa upeo wako uandishi hii sababu ya Malawi kutaka kumega sehemu ya Tanzania ni ndogo sasa sijui kubwa kwako itakuwa ni ipi?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
watu wa lowassa mmepata pa kutokea,eti kauli ya lowassa!hivi ni ya lowassa ama ya kamati anayoingoza?nahitaji ufafanuzi zaidi
Anayeshika usukani ndiye dereva na wengine wote ni abiria tuu!. Hata kama mmiliki wa gari, naye yumo garini, naye pia ni abiria tuu!. Tunasikiliza sauti ya aliyetoa sauti, na sauti iliyosikika ni sauti ya aliyeitoa, not otherwise!.
 
Nasubiri kauli ya fisadi mkubwa Dr. Slaa

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Membe na Lowassa wamevunja katiba kwa kutamka mambo ya vita. Ibara ya 44 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 toleo la mwaka 2005 inasema...'Rais anaweza kutangaza kuwapo kwa hali ya vita kati ya ya Jamhuri ya Muungano na nchi yoyote'.

Viongozi wetu waepuke kutamka maneno yanayoashiria vita. wanaweza kujibu hoja bila kuonyesha dalili kwamba vita vyaweza kutokea.
Kwani kuna vita yoyote imetangazwa?.
 
Inapendeza sana kuwa na viongozi kama Lowasa,Hatuwezi kukaa kimya wakati nchi inataka kuporwa jamani.Na sasa hivi hatusubiri mpaka Malawi aingie kyela,Lungwe .Tutampiga huko huko kwao.Hatutaki ya Kagera yajirudie!! Shime JWTZ
 
Kwahili na mkubali JK always subira uleta heli! Hakuna aja ya kukurupuka mara wanapeleka vifaa na wanajeshi nini km sio ukosefu wa fikra? Malawi juzi walituma delegation tena mpaka Bungeni hiyo yote ni kzungumza na sio vinginevyo..LEO TUMEONA KAULI TATA ZA CHEAP POLITICIANS WENYE NIA YA KUINGIA IKULU..SITTA.... MEMBE....LOWASSA.. Hawa wote kwa mtizamo wangu ni wakurupukaji and gullible leaders yani ni wafuata upepo...viongozi bora ni watulivu, wasiokurupuka na wanaopenda majaridiano na sio vinginevyo...VITA NI HATUA YA MWISHO KABISAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA
kijana haujui unachongea wewe pole sana.swali kwako huo ujumbe uliotumwa na malawi unajua ni ujumbe gani?pili hao waliotumwa unafahamu walifika kuonana na nani bungeni au spika peke yake?unafaha kazi za kamati za bunge?Nakushauri faham vizuri utendaji wa bunge kwanza itakusaidia sana.Loawasa ni mwenyekiti wa bunge ulinzi na usalama na kauli ilikua ni ya bunge na sio kauli yake binafsi. kauli ya membe ni kauli mhimili(serekali) na kauli ya lowasa ni kauli ya mhimili (bunge) kusupport kauli ya serekali.na kamati yake ilijiridhisha na ujumbe huo wa malawi ndio wakatoa kauli.fanya research kabla ya kuchangia bwana.
 
nilisikitika sana hawa viongozi wa CCM akiwemo Bernad Membe waziri wa mambo ya nje, Samweli Sitta waziri wa Afrika mashariki,pamoja na mh. lowasa waziri mkuu mstaafu kuwa wa kwanza kutaka vita na Malawi ilihali wao wenyewe huwa wanakiri kuwa vita ni mbaya. najiuliza ni kwanini wasiingie kwenye mazungumzo ya kidplomasia kabla ya kuihitaji hiyo vita.vitisho na vita iwe silaha ya mwisho. Sisis wananchi tutaaminije kuwa hawa ni watu wazuri ili hali wao wamekuwa wa kwanza kuomba vita. Mbona wamalawi wamekuwa waungwana hawajataka shari na wameondoka ili kupisha mazungumzo. wananchi sasa ndi wakati wa kuona na kutambua CCM haitufai kwa sanbabu wanapenda vita na upinzani hawapendi vita ndio maana wanataka diplomasia.
 
Back
Top Bottom