Nitandelea...
NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it
[/SIZE]
Aljazeera, mimi nakubaliana na wewe kuwa tatizo la Tanzania ni Elimu sawa!, lakini katika Elimu hii tuliyonayo ni nini kinakosekana? Maana tukienda jumla jumla tutasema hivyo Elimu, Elimu, Elimu!! Je hatuna wasomi? Hatuna Vyuo vikuu? Hatuna shule za kutosha? Nini kinachokosekana ambacho kinawafanya wasomi wetu wakishamaliza vyuo wawe mafisadi? Leo hii vijana wanaomaliza vyuo hwatulii sehemu moja makazini!! wakipata nafasi wanapiga pesa na kusepa!!! Je ndiyo Elimu tunayoizungumzia?Mwanakijiji
Tatizo la Tanzania siyo ufisadi bali ni ukose wa elimu ambayo humwezesha mtu kutofautisha aliye msafi na fisadi. Upinzani kwa zaidi ya miaka tano imekuwa ikipiga kelele kuhusu ufisadi lakini ikifika uchaguzi wananchi wanashiriki kwenye ufisadi kuchagua mafisadi.
Kumbuka Elimu ni maarifa ya kutambua ambalo ulikuwa hulitambui na kutatua matatizo ya jamii.
Bila elimu bora na yenye kujumlisha utu, bado watanzania wataendelea kuona mwizi kama shujaa na wapiga dili kama watu wajanja.
Hata sasa hivi wananchi wanakosa namna ya kutofautisha Lowasa na wengine kwa sababu ya kukosa elimu.
Elimu itasaidia watanzania kujitambua.
saafi mkuu, naomba topic nyingine ndeeefu ya kumuongelea anayefaa na umtaje jina. Siyo lazima atoke ccccmmm.![]()
Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".
Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.
Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).
Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).
Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.
Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".
Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"
Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.
Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.
Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi
Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.
Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.
Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.
Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.
Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.
Nitandelea...
NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it
Anataka rais anayeitwa Ukawa, yeye ana jina hilo moja tu maana ni yatima.Kwaio wewe unataka raisi awe nani labda
Mzee Mwanakijiji ametimiza wajibu wake... kilichopo ni kwamba, endapo mathalani MM angepewa uwezo wa kupiga kura 25 million peke yake na kura hizo pekee kuamua mustakabali wa rais wetu, basi kwa mujibu wa MM ni kheri kura hizo zote aziharibu kuliko kumpa Lowasa! Kinyume chake, kuna wengine endapo wangepewa uwezo huo wa kuhodhi kura 25 million peke yao, basi haijalishi Lowassa anasimama na nani... zote hizo wangempa Lowassa! Haidhuru, kura hizo 25 million tunaweza kuziita a powerful veto vote yenye uwezo wa kuamua nani awe rais bila kuhitaji kura ya yeyote ya ziada... ni tofauti na ile ya UN yenye uwezo wa kukataa peke yake! Hapa ndipo unaposimama umuhimu wa hoja ya MM, haidhuru hata kama Lowassa, hatimae atashinda kwa kishindo hata kama ni kwa 95% na zaidi... bado haitaondoa ukweli wa Lowassa kwamba hafai; si tu kwa mujibu wa Mzee Mwanakijiji bali kwa mwingine yeyote yule ambae hana amtakae kwenye kinyang'anyiro hiki; iwe kutoka chama tawala au upinzani!Ndio Mkuu Mzee Mwanakijiji, unasema kuwa Lowassa Hafai, and yes you said it so what?!.
Ila sio Lowassa tuu hafai, kama nakumbuka vizuri uliwahi kusema hata JK hafai, and you said it!, pia uliwahi kusema hata CCM haifai and yes you said it!, ni JK ndiye aliyechaguliwa na CCM ndich chama tawala mpaka leo, na leo tena amesema Lowasa hafai, sitashangaa ikiwa ni Lowasa na 2015 ni CCM tena, ila hizi "Yes I said It" za Mkuu Mzee Mwanakijiji, zitaendelea kwa hao wanaofuata!.
Na kwa ajili ya kuweka kumbukumbu safi, hizi ni baadhi ya yes I said it za Mkuu
Pasco
- Rostam, Msabaha, Kikwete and Richmond - Yes I said it again ...
- Rashid Othman: Umeshindwa Jiuzulu! - Jamii Forums
- Ni lazima tugawanyike; Lazima tusiwe na umoja! -Yes I said it ...
Ingekuwa kauli hizi za Yes I said it, zinaandamana na doing something kuzitekeleza, ingekuwa something, lakini kama ni kauli tuu za Lowassa Hafai! Yes I said It, baada ya hapo nothing more, nothing less, then 2015 rais wetu ni Edward Ngoyai Lowassa, say it or don't, it makes no difference!.
Mwanakijiji
Tatizo la Tanzania siyo ufisadi bali ni ukose wa elimu ambayo humwezesha mtu kutofautisha aliye msafi na fisadi. Upinzani kwa zaidi ya miaka tano imekuwa ikipiga kelele kuhusu ufisadi lakini ikifika uchaguzi wananchi wanashiriki kwenye ufisadi kuchagua mafisadi.
Kumbuka Elimu ni maarifa ya kutambua ambalo ulikuwa hulitambui na kutatua matatizo ya jamii.
Bila elimu bora na yenye kujumlisha utu, bado watanzania wataendelea kuona mwizi kama shujaa na wapiga dili kama watu wajanja.
Hata sasa hivi wananchi wanakosa namna ya kutofautisha Lowasa na wengine kwa sababu ya kukosa elimu.
Elimu itasaidia watanzania kujitambua.
Nani katika CCM amewahi kukemea au kulaani ufisadi?? Wote tu ndani ya ccm hawafai.Kweli Lowasa hafai kabisa sijawahi kumsikia akikemea au kulaani ufisadi hata siku moja.
Kwa nini unadhani CCM itachagua mtu anayefaa? Anayefaa kwa maslahi ya nani? Kama 2005 walichagua asiyefaa, watakuwa wajinga hivyo leo wachague anayefaa?
Umepewa LIKE mpaka na mmiliki wa JF MAXENCE MELO???????we kiboko aisee duhh!!!