Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it

Napitia baadhi ya hizi nyuzi huku nikitafakari kwa kina how 'if you can't beat them, join them', can work out here!.
It is either with us or against us!, join them or fall out!.
Kwenye vita sometimes one is forced to join forces with the devil against a common enemy!.
Pasco
 
Napitia baadhi ya hizi nyuzi huku nikitafakari kwa kina how 'if you can't beat them, join them', can work out here!.
It is either with us or against us!, join them or fall out!.
Kwenye vita sometimes one is forced to join forces with the devil against a common enemy!.
Pasco

What if your enemy was sent by the Devil? Btw so unakiri kuwa Lowassa ni the devil?
Unataka kupata utakatifu kwa kushirikiana na Ibilisi? Kweli utakuwa umefanya jambo gani kama si kuingia mtego wa Shetani. Utetezi wenu una mushkeli!
 
Ndo maana nikasema hawa jamaa mda mrefu wamekuwa wakituchekesha Na sisi tulikuwa tukuwaangalia bila kucheka. Sasa nadhani ni mda muafaka wa kuwasapoti kwa kucheka wanapoanza kuchekesha.

Naomba tuwape sapoti ya kucheka wanapoamua kuchekesha kwa sababu ni dhahiri kuwa sasa hivi wamejipanga kutuchekesha.

Wacha tucheke Na vichekesho vyao.

Naanza kama ifuatavyo:

Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha

Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha

Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha

Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha
 
Hivi Mods hii post mmeunganisha na ya Mwanakijiji kwa sababu zipi wakati ni vitu viwili tofauti. ya mwanakijiji inatoa sababu za kutofaa wakati hii inatoa siri ya watu kumchafua

Umewaona hawa moderaters wanavyokadiria watu ee?

Ndio zao mkuu kugroup threads ili kuzifinya.
Hawajaanzia kwako..
Ndio tabia yao.
 
Napitia baadhi ya hizi nyuzi huku nikitafakari kwa kina how 'if you can't beat them, join them', can work out here!.
It is either with us or against us!, join them or fall out!.
Kwenye vita sometimes one is forced to join forces with the devil against a common enemy!.
Pasco

kutambua na kuyajua haya yanahitaji busara ya ziada mkuu. Kwa mwenye ghiba, visasi, mafundo na utashi binafsi moyoni si rahisi kukuelewa wala kuwaelewa wengine.

Ahsante sana Pasco
 
Mkuu

Hapa kwetu limeingia kwa kasi kiasi kwamba, mafisadi wananunua na kuchagua nani aende Ikulu nani awe nani

Katika mkutano wa juzi Lowassa amesaidia wasiomjua. Ameeleza, pesa anazopata zinatoka kwa marafiki zake.

Utaratibu wa nchi yetu vyama hudhamini watu wao na kuendesha kampeni kwa niaba ya mgombea wao.

Ndilo chimbuko la ruzuku za vyama vya siasa. Sasa Lowassa anapotuambia anachangiwa na marafiki zake, je huo ndio utaratibu wa CCM wa siku hizi? Kwanini hakusimama ili sheria ya mgombea binafasi kama yeye ipite? Marafiki zake ni akina nani, wanamchangia ili iweje?

Kuhusu suala la Elimu, akiwa mbunge hakuna kumbu kumbu zinazoonyesha kama aliwahi kupingana na chama chake ndani ya vikao kuhusu kilimo kwanza au elimu kwanza.

Pengine ushahidi mzuri ungekuwa yeye kujiuzulu nafasi za uongozi kupinga sera zisizo sahihi. Hakufanya hivyo. Leo anaingia na sera yake

Hapa anatuambia, anachotaka kufanya si sera za wana CCM bali ana zake.

Ukichanganya na hoja ya kuchangiwa na marafiki, hakuna shaka kuna 'kachama' kake pembeni kanakohitaji 'label' au logo ya CCM

Lakini pia, tunataka EL atuambie, anasimama vipi katika ufisadi ambao ni tatizo linalodumaza Kilimo kwanza na Elimu kwa upana wake?

Huwezi kufanikisha sera ya elimu akiwa umefungwa mikono na miguu na mafisadi waliowekeza kumpeleka Ikulu

Tuna mahali pa kuanzia na si kutekwa na wafanyakazi wake wanaoaminisha umma, anafaa bila kutueleza kivipi.
teh teh teh lakini Mbowe alivyomleta wote tuliufyataa hatukuhoji pesa za kampeni zinatoka wapi
 
Back
Top Bottom