Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

“Hapa hatuchagui mtu maarufu, Hapa tunachagua mtu safi na huyu si safi. Kama unapenda sura yake basi nenda kanywe naye chai. Wengine mnasema aaah ni tuhuma tu. Samuel (Sitta)! Yusuf (Makamba)! Mnasimama hapa Yusuf (Makamba) mnasema ni tuhuma tuhuma tu! Lakini mtakumbuka mke wa Kaisari alipotuhumiwa kwa ugoni Kaisari akaagiza uchunguzi ufanyike. Uchunguzi ukafanyika na ikabainika kwamba sio kweli. Lakini Kaisari bado akamuacha, akasema mke wa Kaisari hapaswi hata kutuhumiwa. Na sisi hapa Mgombea wetu hapaswi hata kutuhumiwa wakati wapo wengine safi ambao hawana tuhuma. Kama mkimteua huyo mimi sitapiga kampeni. Siko tayari kumsafisha mtu matope halafu ndio nimuombee kura. Hapana kabisa. Huyu mimi najua si msafi na nchi nzima inajuasi msafi. Hafai kuwa mgombea wetu.” – Mwl. Julius Nyerere, NEC Dodoma, Juni 1995 Nyerere, NEC Dodoma, Juni 1995

Asante sana...You made my day

Nalog Off

cc Washawasha
 
Last edited by a moderator:
edward-lowassa.jpg


Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it

Ufisadi upo kwenye agenda na ni kipaumbele pia ila elimu kwanza tukimaanisa elimu hata ya watu wazima ili tuweze endesha sekta zetu wenyewe migodi,viwanda,kilimo pia, utalii nk. Kwahiyo kusema elimu hii iwe kipaumbele ni kuwawezesha watanzania wa sekta zote ili waweze kuwa wafanisi zaidi kwenye sekta zao
 
Mimi ndiyo ninapaswa nijue ya kwamba Mke wangu ni malaya na siyo niambiwe na mtu, kama Watu wanamuona Mke Malaya lkn mimi namuona siyo hilo halininyimi Usingizi!
Hadi ngoma ikuchukue eti eh!!
 
Kutokana na elimu mbovu, karibu kila mtanzania ni fisadi unafahamu maana ya kupiga pesa. Wewe kama unakijinafasi usipopiga pesa jamii inayokuzunguka wote watakuona mchovu. Viongozi wote ni mafisadi wa upinzani na wanao tawala.
Ukubwa wa ufisadi wanaofanya unatofautiana kulingana na urefu wa kamba walizonazo kwa sasa, lakini kimantiki wenda ni mafisadi kuliko hata Lowasa.

Too low. Kwahiyo unapendekeza tuache mambo yaendelee kama yalivyo? Think again, think big!
 
...Lowassa hafai hafai kabisa....na inasikitisha kama taifa mtu huyu ambavyo kuna watu wamejitoa ufahamu kumsafisha ili tu agombee urais...
....Huyu mtu hafai kuwa rais kwa kuchafuka tu pale alipoachia uwaziri mkuu kwa kashfa ya richmond....Inasikitisha leo eti anapata nguvu ya kutoka na kutaka kujisafisha eti hakuhusika na richmond!!....yaani mtu aachie uwaziri mkuu kwa kashfa alafu leo tumwone msafi???....eti anasema walimchafua...eti waliutaka uwaziri mkuu???...really???kwanini wautake uwaziri mkuu wake???...yeye nani hadi watu wautake uwaziri mkuu wake kipindi kile???....Inasikitisha sana watanzania wanavyofanywa wajinga kuwaamini hawa wezi wa mali za umma....

....Lowassa anasema eti yeye hapendi umaskini anapenda utajiri???.....yaani mtu aibe tu ili kuupata huo utajiri ...yeye kwake Lowasa hilo sawa tu....Ndio maana huwezi kumsikia Lowassa anakemea rushwa/ufisadi....maana yeye huo kwake ni njia ya kuupata utajiri anaoupenda yeye...Mtu wa fikra hizi akipewa urais si anauza nchi kwa gharama zozote....ili raia/watu wake wawe matajiri.....

....Kwa mtu makini anaemsikiliza Lowasa unaona kabisa ni mtu mchafu anaetumia nguvu nyingi kujisafisha ili kupata haki ya kugombea urais TZ...mtu wa namna hii hafai...maana mtu msafi hatakiwi kuhisiwa kuwa mtu wa rushwa/ufisadi....kwanini yeye Lowasa ahusishwe na ufisadi???kwanini yeye???who is he??..lazima maswali haya watanzania wahoji kabla ya kufanya maamuzi ya kumfagilia fisadi kuwa rais...

...kule ccm waliwahi kumhusisha Lowasa na kuvuana magamba....hili nalo limesahauliwa???..hili Lowassa atalisemeaje??

...Wanaosema eti kama Lowassa fisadi ashtakiwe....watanzania hawajiulizi ni mafisadi wangapi wameshtakiwa TZ???...kama mfumo waliojiwekea watawala wanashindwa kushtakiana vipi watu hawa waonekane wanafaa....

....Juzi wamepeana eti adhabu huko ccm wale walioanza kampeni....adhabu gani hizo wakati wote leo wanakubaliwa wagombee??....ni utaratibu gani huu ukubalike wakati watu hawaadhibiani pale wanapofanya makosa???

....Taifa hili linahitaji fikra za mabadiliko hakika...kabla ya kufikia kufanya maamuzi kama haya ya kutafta wagombea urais....Watu wanaowafagilia wezi kwenda ikulu hawana uwezo wa kuchagua viongozi bora....

...Mwisho...Mkiniuliza nani anafaa agombee urais TZ....nasema ni mtu mmoja tu..nae ni Mh.Tundu Lissu....maana lazima tunapotoa critics tuwe na mbabala....


Ndugu yangu hii nchi ni ya ajabu sana, usishangae mtu wa aina ya EL anakuwa rais wa nchi hii kwani hapa watu wanachagua kutokana na nguvu ya media na sio uwezo wa mtu. Ukijaribu kuangalia ndio kashaiteka media kwa hiyo wananchi wote watafanyiwa mindgames na ikifika wakati wa uchaguzi unakuta anapata ushindi. Kwa hili nawaomba upinzani waandae vipindi vya redio, television nk kuhakikisha wanaupa umma elimu ya kutosha kuhusu kufanya kosa wakati wa uchaguzi. Sasa hivi hata wale watu waliokuwa na uelewa wakati pia eti wanasema EL anakubalika bila hata kujua kwamba tunachezewa mchezo uleule wa mwaka 2005, sifa za rais kijana, ambaye picha yake itapendeza kwenye noti. Hivi leo tumesahau kwamba vyombo vya habari ndio vilitufikisha hapa tulipo na sasa naona picha ile ikitaka kujirudia tena. Niviombe vyombo vya habari hata kama ni kununuliwa lakini waangalie athari ya kile kitakacho likuta taifa letu huko mbele ya safari.
 
Hadi ngoma ikuchukue eti eh!!

Inaweza isinichukuwe pia! Wapo walioambiwa kwamba Mke wako ni malaya wakasikiliza kumbe waliomwambia walikuwa wanaona wivu na kutaka kumuharibia ndoa yake na sasa wanamcheka na kumkimbia, hivyo maadamu tu watu wanasema fulani ni mbaya haimaanishi ya kwamba ni kweli ni mbaya mpaka waliniletee uthibitisho na kwa kutumia mfano wako mpaka wanipeleke mahali ambapo Mke wangu amelala na Mwanaume na niwakute live ndio nitachukua hatua bila ya hivyo nitapuuzia tu!
 
edward-lowassa.jpg


Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it


Mungu akubariki sana mzee mwanakijiji kwa kuliona hili kiufupi lowassa hafai ni fisadi ambayr hata kukemea tu ufisadi kwa maneno hawezi achilia mbali vitendo
 
Speed yake kipindi alichokua waziri mkuu japo ni kwa mda mfupi lakni vitu vichache alivyofanya vimeleta impact kubwa kwenye jamii. Elimu ni kitu muhimu kitacho mkomboa mtanzania. Shule za kata zimesaidia sana jamii. Angeweza kukaa na mheshimiwa kipindi chote nchi ingekua mbali. Huu ndio naona ni ubora wake.

Kuna vijana wengi karibia 90% wamepita bila chochote na kupelekea serikali hii kubadilisha ufaulu ili kuficha uchafu huo! Hivi ilikuwa lazima tuwe na shule za kata! shule za tarafa hazikuwa suluhisho au shule kadhaa katika wilaya moja kuliko huu unaosema shule za kata zimesaidia! Hizi shule ndio credit ya UKAWA na sio CCM tena! Pole
 
Ufisadi upo kwenye agenda na ni kipaumbele pia ila elimu kwanza tukimaanisa elimu hata ya watu wazima ili tuweze endesha sekta zetu wenyewe migodi,viwanda,kilimo pia, utalii nk. Kwahiyo kusema elimu hii iwe kipaumbele ni kuwawezesha watanzania wa sekta zote ili waweze kuwa wafanisi zaidi kwenye sekta zao


Elimu inaweza vipi kuwa na matokeo yatarajiwayo kwa wengi wetu (majority) mahali ambapo kuna kutamalaki kwa ufisadi?
 
wanaweza pia wasikupeleke mahali ambapo mke wako kalala na mwanaume lakini ikawa ni kweli kalala na mwanaume ila wewe utaendelea kuamini kwamba hajawahi kulala na mwanaume japo huo utakuwa sio ukweli
 
Elimu inaweza vipi kuwa na matokeo yatarajiwayo kwa wengi wetu (majority) mahali ambapo kuna kutamalaki kwa ufisadi?

Mtu mmoja anakunja Tzs.1.6b mwingine Tzs.3trilion anazawadiwa ubalozi! Halafu leo tuseme kuna mwanaccm anakemea ufisadi! Hawa hawa wakati wanatanzania wakitegemea katiba itokane na maoni yao waliwapinga na kupiga kura tofauti. Halafu leo tupate kiongozi bora toka CCM. Labda bora kiongozi maana tunaona jinsi tunavyosurubishwa na dola kwa Shillingi lakini jamaa kimya!
 
Kwa maneno haya, na kwa ubabe wa wanamtandao, sasa naanza kujiuliza kama Baba wa Taifa alikufa kifo cha kawaida....
....kule Burkinafaso wamemfukua kaburini marehemu Thomas Sankara ili kujua nini haswa kilisababisha kifo chake....maana mazingira ya kifo chake yalikua tata sana....Hapa kwetu TZ ni wakati sasa huko tuendako ku probe ili kujua mazingira...na haswa chanzo halisi cha kifo cha Nyerere...maana hakika kwa matukio yaliyotokea baada ya kifo chake kuna umuhimu haswa ku probe mazingira....na hashwa chanzo cha kifo chake....Ukifatilia kwa makini utaona kuwa mambo mengi maovu kwa taifa hili yalifanywa baada ya kifo cha mzee wetu Nyerere...
 
Ufisadi upo kwenye agenda na ni kipaumbele pia ila elimu kwanza tukimaanisa elimu hata ya watu wazima ili tuweze endesha sekta zetu wenyewe migodi,viwanda,kilimo pia, utalii nk. Kwahiyo kusema elimu hii iwe kipaumbele ni kuwawezesha watanzania wa sekta zote ili waweze kuwa wafanisi zaidi kwenye sekta zao

Je, unayo habari kwamba Nigeria inayo wasomi wengi sana na bado maendeleo yake kama nchi si mfano wa kuigwa? Msome tena Mzee Mwanakijiji, hujamuelewa au . . .
 

Hili la kuaminishwa limenitisha kuliko nilivyodhani awali kuwa Lowassa ana friends wa kawaida tu.
Nimepitia Mahojiano yake na Raia Mwema ya Mei 27-June 2 2015 Tole Na.407 tena yaliyofanywa na Mhariri Ezekiel Kawanga sikuamini nilichokuwa na kisoma.
Shida niliyopata ni aina ya maswali ya Mhariri kwenda kwa Lowasa kiufupi ni kama maigizo, natumai wasomaji wengi watakuwa wameisoma na kupata mantiki ya mahojiano yale.

Kwa mtazamo wangu yamekaa katika kuaminisha Watu.''Nachukia Umaskini" Lowassa
Kazi kama hiyo haikufaa ifanywe na Gazeti kama Raia Mwema.




Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hawa wanaojiita Friends of Lowassa na ambao kwa uhakika ni WanaCCM kama hili
[h=3]Hotuba ya Mwalimu Nyerere, Mkutano Mkuu wa ... - YouTube[/h] haijawaingia akilini basi watakuwa wamelogwa .
Kushabikia na kumsifia Mtu Kama Lowasa asiyewezi kutamka hata neno Ufisadi kwa kinywa chake basi kunamatatizo makubwa mbele ya safari.

Bahati Nzuri Mwalimu alianza na hili la Ufisadi kuwa ni tatizo:
Mzee Mwanakijiji imeandikwa Mganga hajigangi kwa maana hiyo Suala hapa siku kuelewa au kukubali .




Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it
 
Back
Top Bottom