Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Hapo hauna msaada kwa nchi yako. Yes Lowassa hafai lakini hujasema nani anafaa, ungeandika mengi ya kumsifia ANAYEFAA ungekuwa na msaada kuliko kumponda asiyefaa kwa maneno mengi bila kuonesha mbadala. Hii nchi ina matatizo makubwa kuliko tunavyodhani kama thinkers ndio nyie
 
edward-lowassa.jpg

Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "safari ya matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai. Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences). Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haiitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi. Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it

Mimi kwangu hamna jipya ulilolisema na ninajua fika ya kwamba Bw.Lowasa ni fisadi lakini bado Nitampa Kura yangu kama akigombea, na sababu ni rahisi tu sioni mbadala wake, kama ni Mbowe pia aniaambie ni kwa nini alisema Serikali inafuja mali ya Umma kwa kununua mashangingi akarudisha lake na kulichukua tena na mpaka leo hii analitumia na juzi alikutwa nalo Mombasa, Kenya likiwa na namba za Kiraia, Je yeye siyo sehemu ya Ufisadi unaofanywa na Serikali aliokuwa analalamikia? Na kama akiwa raisi au Chama chake atwezaje kuondokana na ubadhirifu huu kama sasa hivi ameshindwa?

Hilo la kwanza la pili Serikali ya kifisadi ya CCM inaongeza Mishahara na marupurupu kwa Wabunge wote na wa upinzani sijasikia Mbunge yoyote yule kuanzia wa Upinzani wanaomuita Lowasa fisadi mpaka wa CCM akilalamikia hii dhuluma siajabu kubwa kulko yote TanZania kwa maana Majimbo ya akina Tundu Lisu haya zahanati wala Dawa lakini yuko kimya kwenye hilo, hivyo maadamu mimi sipati majibu ya maswali kama haya basi mimi kura yangu mpaka sasa hivi ni Fisadi Lowasa tu angalau namjua kuliko hawa nisiowajua!
 
Elimu jimboni kwake imemshinda , ataiweza nchi Nzima? Huyu mamvi

Vipi kwa Nyerere vipi kwa Mwinyi vipi Masasi vipi Chalinze mbona unaangalia Monduli kwenye changamoto kuliko kote huko au wewe wa Ilala nini?
 
edward-lowassa.jpg


Watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa anafaa kuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa Lowassa ni kiongozi bora ambaye Watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "Safari ya Matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa Lowassa (hasa baada ya kuwa Waziri Mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - Lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa Lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama Mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka CCM. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa Lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na NEC na yeye akaendelea kuwa Waziri Mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) Lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "Kilimo Kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "Elimu Kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya Kilimo Kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha Dakika45 (kinachorushwa na ITV). Alinukuliwa kusema "Mpango huu wa Kilimo Kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (CCM) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa Elimu Kabla ya Kilimo Kwanza"

Hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa Lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili Tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) Tanzania kufuata njia ya Nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama Nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la Tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

Lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere. Kutokuelewa kuwa Ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya Urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake Lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya" bali zaidi kwa kuwapa Watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua Bunge na ile ya Ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea Wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya CAG imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya CCM na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa Rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; I'm just stating the obvious.

Wanaomtaka Lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za Lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

NB: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: Kikwete Siyo Safi, Yes I said it


Sawa pendekeza wako unaeona anafaa bas
 
Ndio Mkuu Mzee Mwanakijiji, unasema kuwa Lowassa Hafai, and yes you said it so what?!.
Ila sio Lowassa tuu hafai, kama nakumbuka vizuri uliwahi kusema hata JK hafai, and you said it!, pia uliwahi kusema hata CCM haifai and yes you said it!, ni JK ndiye aliyechaguliwa na CCM ndich chama tawala mpaka leo, na leo tena amesema Lowasa hafai, sitashangaa ikiwa ni Lowasa na 2015 ni CCM tena, ila hizi "Yes I said It" za Mkuu Mzee Mwanakijiji, zitaendelea kwa hao wanaofuata!.

Na kwa ajili ya kuweka kumbukumbu safi, hizi ni baadhi ya yes I said it za Mkuu


  1. [*][h=3][URL="http://www.google.com/url?sa=t&rct=j&q=&esrc=s&source=web&cd=2&ved=0CCkQFjAB&url=http%3A%2F%2Fwww.jamiiforums.com%2Fjukwaa-la-siasa%2F15618-rostam-msabaha-kikwete-and-richmond-yes-i-said-it-again-7.html&ei=joJkVaWjA8SxygPPlYHoCw&usg=AFQjCNHIxxq05spU3z_OFkl2GRUumm28QA&bvm=bv.93990622,d.bGQ"]Rostam, Msabaha, Kikwete and Richmond - Yes I said it again ...
    [/h]
  2. [h=3]Rashid Othman: Umeshindwa Jiuzulu! - Jamii Forums[/h]
  3. [h=3]Ni lazima tugawanyike; Lazima tusiwe na umoja! -Yes I said it ...[/h]Ingekuwa kauli hizi za Yes I said it, zinaandamana na doing something kuzitekeleza, ingekuwa something, lakini kama ni kauli tuu za Lowassa Hafai! Yes I said It, baada ya hapo nothing more, nothing less, then 2015 rais wetu ni Edward Ngoyai Lowassa, say it or don't, it makes no difference!.

    [/URL]



Pasco
 
Ukweli ikiwa Edo ataupata uraisi itakuwa ni janga la kitaifa . Kwa nini

(1) Lazima hao marafiki zake waliomchangia watataka kurudisha hela zao na yeye pia atataka kurudisha fedha zake alizotumia kwani kila mtu anajua jinsi alivyomwaga fedha kununua kuungwa mkono. Wote tunajua hakuna atakayetoa hela yake bure bila kujua atazirudisha vipi kwani kama ungekuwa ni msaada basi hata hao watoa msaada wangeweza kunipa mimi nipeleke kanisani na msikitini lakini hawakufanya hvyo kwani walikuwa wanajua wanachokitafuta kupitia kwa Edo. Uraisi wake utakuwa wa kununua na si vinginevyo. Angalia tangazo la kwenye gazeti la Mwananchi la tarehe ya leo 26/5 ni tangazo la bei mbaya. Kizuri kinajiuza kibaya kinajitangaza.

(2) Uraisi wake utaongeza mpasuko ndani ya chama cha mapinduzi na serikalini hasa kwenye vyombo vya usalama na kutakuwa na kulipiza visasi na kuhujumiana sana kuonyesha kila upande ulivyo na uwezo mdogo wa utendaji jambo litakaloongeza gharama za uendeshaji na matumizi mabaya wa taasisi za serikali

(3) Kutokana na mambo hayo mawili ufanisi wa serikali na vyombo vyake utakuwa mdogo sana hivyo uchumi utayumba, rushwa itaongezeka sana na itatuumiza, kutakuwa na Serikali ya kulazimishana na kutokana na hilo vyama vya upinzania vitapata nguvu sana (4) Kuongezeka kwa nguvu ya vyama vya upinzania kutafanya Serikali izidi kuwa ya kigandamizi kuua kabisa haki za msingi za kiraia. Hivyo fedha nyingi sana na nchi zitatumika kwa ajili ya kugandamiza haki za binadamu badala kulipia gharama za maendeleo.

Kitendo cha kusema eti kama angeendelea kuwa Waziri Mkuu hii nchi ingekuwa na maendeleo zaidi ni kitendo cha kuiponda Chama Chake na Serikali iliyoko madarakani ambayo ni kitu kibaya sana kwa mshikamano wa Chama na Serikali. Sidhani kitu hicho kitavumiliwa na Watanzania wenye nia njema na nchi hii.

Vile vile kule kusema kuwa eti walimvizia Mkurugenzi wa Kampuni ya Maji ili wamfukuze kabla hajaenda mahakamani kupata zuio la kimahakama inaonyesha kabisa akipata Urais atakuwa Rais wa namna gani. Kila mtu awe mtanzania au sio ana haki ya kupata haki yake kupitia mahakami na hairuhusiwi Serikali wala mtu yeyote kuzuia haki kwa sababu yeyote.

Ninaomba Watanzania watafakari hilo.

 
ndani ya ccm hakuna mwenye uwezo wa kumwonyeshea kidole mwenzake wote hawafai.
VOTE FOR UKAWA.
Mimi sina chama ila najua kupitia UKAWA na ndani ya CCM pia kuna watu makini sana tu wanaweza kwa ukamilifu kutuongoza kujenga Nchi yenye maziwa na asali..lakini cha kwanza kabla ya vyote UFISADI NA RUSHWA viondoke ndani ya ofisi za serikali, Binafsi, Majumbani mwetu, ndani ya mifuko ya rafiki zetu, matajri, wanasiasa na umma kwa ujumla wake.

Sio kuwa Watanzania hawezi kuwa na maisha yao bila UFISADI ama RUSHWA.Ukisha kuwa na mfumo wa matedno hayo mawili mfumo mzima wa maendeleo UNAKUFA GANZI.HAKI aina nafasi katika kufanya maisha ya RAIA walio wengi kuata MKATE wao wa kila SIKU na maendeleo ya JUMLA ya maisha yao katika njia na misingi ya HAKI kwa wote.Mgawanyo wa keki ya TAIFA inapokwenda kwa kikundi cha watu wachache ndipo uti wa mgongo wa maendeleo unapelekea mushindwa kufanya kazi ilivyopaswa kwa kuwa ili jambo A liende na kupata nafasi ya kuzalisha jambo B, aliwezi kwenda kuwa PESA/RUSHWA inatakiwa ili kulifanya lifanyike.Je ni mamilioni ya Watanzania wangapi wenye mifuko ya kutosheleza UTOAJI wa RUSHWA?

Kwani tuwe TAIFA la RUSHWA NA UFISADI...WHY?...Elimu yetu inamakosa gani?isiyoweza kuonyesha MORALS na UBINADAMU wa Dunia ya karne ya 21.
 
Mkuu

Kukaa kimya Watanzania wakilishwa peremende badala ya mlo si kuwatendea haki.

Jana nilikuwa naangalia BBC nikaona mgao wa mafuta katika taifa mwanachama wa OPEC Nigeria.

Sababu kubwa ni kutokana na ufisadi ambao umefikia mahala pa kuiweka serikali mateka
Kwa wasioona wanaweza kudhani hilo lipo Nigeria na kwingine.

Guess what! anayedhani hivyo anahitaji msaada wa wataalamu wa macho, masikiona ubongo. Tatizo lipo nchini na linaimarika kila siku

Ukubwa wake nchini ni zaidi ya Nigeria. Kule Nigeria tunafahamu ufisadi na utapeli ni sehemu ya maisha (norm)

Hapa kwetu limeingia kwa kasi kiasi kwamba, mafisadi wananunua na kuchagua nani aende Ikulu nani awe nani

Katika mkutano wa juzi Lowassa amesaidia wasiomjua. Ameeleza, pesa anazopata zinatoka kwa marafiki zake.

Utaratibu wa nchi yetu vyama hudhamini watu wao na kuendesha kampeni kwa niaba ya mgombea wao.

Ndilo chimbuko la ruzuku za vyama vya siasa. Sasa Lowassa anapotuambia anachangiwa na marafiki zake, je huo ndio utaratibu wa CCM wa siku hizi? Kwanini hakusimama ili sheria ya mgombea binafasi kama yeye ipite? Marafiki zake ni akina nani, wanamchangia ili iweje?

Kuhusu suala la Elimu, akiwa mbunge hakuna kumbu kumbu zinazoonyesha kama aliwahi kupingana na chama chake ndani ya vikao kuhusu kilimo kwanza au elimu kwanza.

Pengine ushahidi mzuri ungekuwa yeye kujiuzulu nafasi za uongozi kupinga sera zisizo sahihi. Hakufanya hivyo. Leo anaingia na sera yake

Hapa anatuambia, anachotaka kufanya si sera za wana CCM bali ana zake.

Ukichanganya na hoja ya kuchangiwa na marafiki, hakuna shaka kuna 'kachama' kake pembeni kanakohitaji 'label' au logo ya CCM

Lakini pia, tunataka EL atuambie, anasimama vipi katika ufisadi ambao ni tatizo linalodumaza Kilimo kwanza na Elimu kwa upana wake?

Huwezi kufanikisha sera ya elimu akiwa umefungwa mikono na miguu na mafisadi waliowekeza kumpeleka Ikulu

Tuna mahali pa kuanzia na si kutekwa na wafanyakazi wake wanaoaminisha umma, anafaa bila kutueleza kivipi.
 
Mimi naenda mbali zaidi na kusema kuwa CCM yote haifai kuchaguliwa tena.

Swali ni je, ni nani anayefaa zaidi ya CCM?
Kamwe hautapata jibu...

Nimefuatilia mijadala kila kona leo watu wanasema Lowassa hafai lakini hakuna hata mmoja amependekeza anayefaa. Ni sawa na mzazi kuwaambia wanaye ugali na maharage ni chakula kibaya lakini hajanunua chakula mbadala. Nani anafaa jamani? Ina maana aliyepo Lowassa peke yake? Na kwa kuwa hafai tunamchagua hivyo hivyo?
 
kwakua wew umeelewa tatizo ni ufisadi katafute chama ugombee then tukutane october
 
Ikulu siyo pango la mafisadi.
VOTE FOR UKAWA.
 
Saa inakuja ambayo mabakuli yote yatafungwa please waiting time is loading.....................................................................................................................
 
Mkuu

Kukaa kimya Watanzania wakilishwa peremende badala ya mlo si kuwatendea haki.
Jana nilikuwa naangalia BBC nikaona mgao wa mafuta katika taifa mwanachama wa OPEC Nigeria.

Sababu kubwa ni kutokana na ufisadi ambao umefikia mahala pa kuiweka serikali mateka
Kwa wasioona wanaweza kudhani hilo lipo Nigeria na kwingine. Guess what! anayedhani hivyo anahitaji msaada wa wataalamu wa macho, masikio, akili na ubongo. Tatizo lipo nchini na linaimarika kila siku

Ukubwa wake nchini ni zaidi ya Nigeria. Kule Nigeria tunafahamu ufisadi na utapeli ni sehemu ya maisha (norm)
Hapa kwetu limeingia kwa kasi kiasi kwamba, mafisadi wananunua hata hivyo, wakichagua nani aende Ikulu nani

Katika mkutano wa juzi Lowassa ametusaidia sana hasa wasiomjua. Ameeleza kuwa pesa anazopata zinatoka kwa marafiki zake. Utaratibu wa nchi yetu vyama hudhamini watu wao na kuendesha kampeni kwa niaba ya mgombea wao. Ndilo chimbuko la ruzuku za vyama vya siasa. Sasa Lowassa anapotuambia anachangiwa na marafiki zake, je huo ndio utaratibu wa CCM wa siku hizi? Kwanini hakusimama ili sheria ya mgombea binafasi kama yeye pite? Marafiki zake ni akina nani, wanamchangia ili iweje?

Kuhusu suala la Elimu, akiwa mbunge hakuna kumbu kumbu zinazoonyesha kama aliwahi kupingana na chama chake ndani ya vikao kuhusu kilimo kwanza au elimu kwanza. Pengine ushahidi mzuri ungekuwa yeye kujiuzulu nafasi za uongozi kupinga sera zisizo sahihi. Hakufanya hivyo. Leo anaingia na sera yake binafasi

Hapa anatuambia, anachotaka kufanya si sera za wana CCM bali ana zake. Sasa ukichanganya na hoja ya kuchangiwa na marafiki, hakuna shaka kuna 'kachama' kake pembeni kanakohitaji 'label' au logo ya CCM
Hii ndiyo CCM tunayoambiwa?

Lakini pia, tunataka EL atuambie, anasimama vipi katika ufisadi ambao ni tatizo linalodumaza Kilimo kwanza na Elimu kwa upana wake? Huwezi kufanikisha sera ya elimu ukiwa umefungwa mikono na miguu na mafisadi waliowekeza kukupeleka Ikulu

Tuna mahali pa kuanzia na si kutekwa na wafanyakazi wanaoaminisha umma, anafaa bila kutueleza kivipi.

Kuna sheria inaitwa ya Gharama za Uchaguzi 'Election Expences Act 2010' hivi Lowassa inamhusu ama haimhusu maana iliweka viwango kabisa vya gharama za kutumiwa ....au sasa kwa kuwa shilingi imeporomoka na sheria imeporomoka ?
 
Nadhani ni wakati sasa wa kutupa ushaidi wa kisheria unaomtia hatiani EL,maana siasa za afrika zimekuwa za kinafiki tofauti na wenzetu wa dunia ya kwanza,ss ni matusi,kashifa,kejeri badala ya kutueleza nini mtalifanyia taifa hii,kuamini hii angalia wanapokuwa kwenye majukwa 95% kejeri 5% sera.
 
Back
Top Bottom