Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

HIVI MWANAKIJIJI, kwani mtu akisema kipaumbele chake ufisadi inamaanisha kuwa vitu vingine havitafanyika?

Tukuulize wewe! Kwani Mwanakijiji hakusema kama wewe unavyotaka kusema. Au labda nikusaidie. Kipaumbele ni kitu utakachokipa umuhimu zaidi. Na hii haimaanishi kuwa vingine havina umuhimu...
 
Ukimuona mtu mchafu ukasema ni mchafu utakuwa umemchafua au umeeleza kilicho dhahiri. Kumchafua mtu kuna presume kuwa mtu huyo alikuwa msafi kwanza. Vinginevyo, asingejitahidi sana kujaribu "kujisafisha". Ukiona mtu anaenda mtoni kuoga mara kwa mara ujue...

HIVI MWANAKIJIJI, kwani mtu akisema kipaumbele chake ufisadi inamaanisha kuwa vitu vingine havitafanyika?
Kwahiyo atakaekuja na kipaumbele cha ufisadi, hatashughulika na elimu? Kwani elimu haiwezi ikatumika kuelimisha watu wakaacha kupokea au kutoa rushwa? au wakafunzwa kutokuwachagua mafisadi katika ngazi mbalimbali za uongozi?
 
Ndugu labda nnaomba unisaidie kitu kimoja katika maisha yako yote toka umfahamu Lowassa ni lini umesikia kawahi kukemea ufisadi!!?

That the point ambayo nimeipata humu" kwakweli sijawahi msikia ata akitamka hilo neno" si kwamba mi ni mfuasi wake sna au mkereketwa sana wa sera zake. To me I think katika wote ambao ad sahivi wamejitokeza naona bora yy sijui labda atokee mwengine mana muda bado.
 
Asante sana mkuu. Wanasema eti kipaumbele kitakuwa elimu wakati ufisadi umetanda kila kona! Hizo fedha watatoa mbinguni? NI SAHIHI kabisa kusema umaskini wetu unasababishwa na ufisadi! Ona wanatudanganya wataweka vipaumbele kwenye elimu wakati wanazidi kuongeza majimbo ya uchaguzi kwa wabunge wasiokuwa na mchango wowote katika maendeleo ya nchi yetu bali hasara tupu!

Hao wabunge wengi ni hasara tupu. Ingekuwa amri yangu, kila wilaya na mbunge mmoja tu. Tunaongeza wezi tu.
 
hatuwezi kutatua matatizo yetu kwakujidanganya kuwa hayapo kama hatukubali kuwa lowasa ni fisadi hembu tuwaangalie wanaozunguka mfano rostam,chenge,karamagi n.k utaona jinsi watu wengine hum wanavyojitoa faham finally be the men who can see tommorow msiwe charmed na vihela vyake jiulizeni akifika ikulu atazirudishaje? na ndio maana Lowasa anaona ufisadi kama sihoja kwake
RAIS JK TUTAKUKUMBUKA SANA KAMA UKIKATA JINA LA HUYU KIUMBE.
 
Think big! Utamalizaje ujinga bila nyenzo? Jibu ni huwezi. Hivyo yabidi uwe na nyenzo ndio uushinde ujinga! Fedha zilizopotea kwenye kashfa zote zilizotokea kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita (zilizojulikana na zisizojulikana) zingetumika kwenye elimu tungekuwa na shule bora kabisa. Wewe unaona logic, kwa mfano, ya kuongeza majimbo ya uchaguzi wakati hatuna shule za kuridhisha? Again think big!

Nimeshangaaa sana post ambayo mwanakijiji ameiandika,ningemwona wa maana kama angesema tumchague Membe wake. Povu linalomtoka si bure. MSOMI GANI ANAEJIITA MCHAMBUZI anaetaka kutuaminisha kuwa kama jipaumbele cha mtu ni kitu fulani basi vitu vingine havitakwenda. Hivi mtu akisena mwaka huu kipaumbele changu ni ujenzi wa nyumba basi hatakula, hatawapeleka watoto shule, hatalala,hatajilinda na wezi, hatasali.
Ama kweli Mwanakijiji ni mchumia tumbo kama wachumia tumbo wengine.
 
Utasemaje hoja za kumchafua wakati yeye mwenyewe keshajichafua tayari? Tunaowashangaa mpaka sasa ni wale wanaotaka kumsafisha wakati yeye mwenyewe keshamaliza kazi ya kujichafua na kibaya zaidi anaendelea kujichafua hadi sasa hajakoma. Kitendo cha kusema serikali ilikosea kuweka kipau mbele Kilimo kwanza ni kutoheshimu maoni ya wenzake katika baraza la mawaziri. Viongozi wetu walijadili na wakaamua kwa pamoja kuwa serahii ndiyo bora kuliko zote ikiwa ni pamoja na elimu. Hoja ya kusema kama angalibakia kuwepo kwenye serikali maendeleo ya shule za kata zingekuwa bali zaidi ni kubeza juhudi za wenzake na kujitwisha sifa za wengi peke yake. Ni ubinafsi zaidi kuliko uwajibikaji wa pamoja kama serikali. Hivi tu alikuwa waziri mkuu je atakapokuwa rais itakuwaje? Hata kazi za wahandisi atasema kafanya yeye. Kila kitu atakuwa kafanya yeye. Nchi gani inajengwa na mtu mmoja asipokuwa yeye haliwi jambo? Anazidi kusiliba maji taka yenye harufu kali
Mada za kumchafua EL zimekua nyingi sasa. Inanifanya nijue yy ni bora kwa jinsi mnavyokesha kumchafua
 
That the point ambayo nimeipata humu" kwakweli sijawahi msikia ata akitamka hilo neno" si kwamba mi ni mfuasi wake sna au mkereketwa sana wa sera zake. To me I think katika wote ambao ad sahivi wamejitokeza naona bora yy sijui labda atokee mwengine mana muda bado.

Japokuwa mie sio mwanachama wa chama chechote kwa hali ilivyokaa nnaomba sana kama ikitokea Rais akiwa ni kutoka CCM hasiwe mmoja kati ya waliojitokeza... Vinginevyo ni bora hata Ukawa wakachukua
 
Sijui kipi unataka mzee!! Mtu anayesema sema hapendi ufisadi huku yeye anafanya huo ufisadi au mtu asiyezungumzuia ufisadi huku anakabiliana nao vilivyo. Naona umezeeeka mzeee, nenda zako mzeee, upumzike mzeeee..... Hizi ni zama za matumaini mapya na Jemedari karudi dunia nzima inamkubali kasoro wewe tu!!!! Jitathimini upya mzeeee.
 
Vijana humu kazi ni kushambuliwa watu binafsi badala ya hoja. Lakini hii imetokana na mfumo mzima uliolitengenezwa kutetea na kuhalalisha ufisadi. Huko nyuma watu na vyama pinzani walipoanzisha hoja ya ufisadi watawala walikuwa wakali sana kupinga wakawaita waongo, wachaohezi n.k. Hata hivyo baada ya kuona kuwa watu wameanza kuelewa na approach yao haiungwi mkono wakabadilika. Wakaanza kujionyesha wanapigana na ufisadi na mafisadi wakati huo huo wakiwatafutia wasemaji wa ufisadi nao waonekane mafisadi hili wakose 'moral authority' ya kuukemea ufisadi. Kwa hiyo kama alivyosema Mzee Mwanakijiji kiongozi hasiyejipambanua tangu awali kupinga ufisadi hatufai na wala hastahili kuvuka hatua ya awali.
 
Mwanakijiji ni team membe lazma ampinge lowassa kwa kila namna... hawa ndio walikuwa waanzilishi wa CCJ na kina Sitta... hana jipya huyu mtu ni mchumia tumbo tuu..
Lakini si CCJ ilikuwa na dhamira nzuri hata kama haikufanikiwa? yaani wapambanaji wa ufisadi ndani ya CCM. Nia ilikuwa njema lakini mbinu iliuwa hafifu na isokuwa na utashi wa kutosha. Kwa hivyo kama MK alikuwa na uelekeo huo, sio mchumia tumbo bali ni mzalendo wa kweli (naomba utofautishe uzalendo wa kweli na ACT-wazalendo).
 
Back
Top Bottom