Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,104
- 43,357
- Thread starter
- #261
umetoa mfano wa nigeria na kutaka kuaminisha watu.kua ati elimu haitoweza.kuinua hali za watu bali itazalisha zaidi wasomi ambao mwisho watamalizia jela au kuikimbia nchi. mbona hutoi mifano ya nchi nyingi.ambazo zimefanikiwa kama uk malaysia singapore south korea na nyingi kwa kuweka mbele elimu kwanza.
Naomba nijibu hoja hii kwanza na utaona kwanini msimamo wangu ni sahihi na wa kwako umepotoka. Malaysia ni kweli inaonekana imefika mbali sana kiuchumi. Lakini sijui kama unajua kuwa sasa hivi ni nchi inayoongoza kwa ufisadi huko Asia. Malaysia unayoizungumzia wewe ni ile ya wakati wa Mahathir; ambapo ndio nchi ilijengwa hasa hasa. Hivi juzi tu (April) Mahathir mwenyewe amejitokeza na kukemea uongozi wa nchi yake kwa kuwa sasa Malaysia inatajwa kuwa ni nchi ya kifisadi zaidi duniani! SOMA HAPA HILO
Halafu wana elimu!!! Kama elimu ingekuwa ni tiba ya ufisadi Malaysia isingekuwa hapo. Leo hii Malaysia inavuna baadhi ya mbegu ambazo wengi wanaamini zilipandwa wakati wa Waziri Mkuu Mahathir mwenyewe.
Singapore nayo ni hivyo hivyo. Ni kweli ukiangalia kwa nje ni taifa lenye uchumi wenye nguvu sana Mashariki Kusini mwa Asia. Lakini nayo - pamoja na usomi wake wote - imezama kwenye mambo ya ufisadi. Hili unaweza kulifanyia utafiti wewe mwenyewe na utaona. Mwaka 2012 tu Indonesia imepoteza zaidi ya dola milioni 230 kwenye kashfa mbalimbali za ufisadi.
Umeitaja na Korea ya Kusini na hiyo utaona inathibitisha hoja yangu kuliko ya kwako. South Korea wanapambana na ufisadi kuliko hizo nchi nyingine ulizozitaja (ukiondoa UK). Lakini hata hiyo nayo imeshagubikwa na kashfa kadhaa kubwa tu za ufisadi. Lakini Korea imewashughulikia mafisadi wake bila kujali sura zao na kesi zilishaisha zamani. Kuanzia mawaziri na hata marais wa nyuma; tena wao hawana aibu hata kwa kesi za mambo yaliyopita wameyashughulikia. Mwaka juzi tu hapa maofisa wa uchunguzi walivamia ofisi ya Waziri wa Mambo ya Nje wakichunguza tuhuma za ufisadi - fikiria kitu kama hicho kuweza kutokea Tanzania!
Mtu wa Pwani, tunaposema tatizo kubwa letu ni ufisadi hatusemi kwa hisia tu. Na mnaosema ni elimu nadhani hamjakaa chini kufikiria vizuri maana yake nini. Elimu ingekuwa inapunguza ufisadi mafisadi wangepungua duniani!