Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Lowassa Hafai! Yes I said It - Sababu ya I

Cometh the season cometh the man, kudos MMM!!
Hapo hapo unapogonga huo msumari ongeza tu uzito wa nyundo yako kaka.
 
Kama ajenda ya kwanza ya kumpata RAIS BORA itakuwa "UFISADI" (Kupambana na ufisadi)

I bet my neck hutampata mgombea hata mmoja kutoka CCM. Unaweza kumpata kutoka UPDP au Jahazi Asilia lakini sio CCM!

UFISADI na CCM ni Chanda na Pete! Kasoro tu wana-CCM wanazidiana levels za UFISADI.
 
Sasa naona Mzee Mwanakijiji umegeuka kuwa Kijana wa mjini!! dont jump the gun please! naona kama unajaribu kukataa ukweli kwamba ELIMU ndio ufunguo wa maendeleo; Elimu ndio Urithi endelevu! Elimu ndio STOCK IN TRADE ya watu walio wengi nchini mwetu na duniani kote! (msome hayati Lee kuan Yew; Founding father wa Island state ya Singapore; Hayati baba wa Taifa akiita Singapura!; Taifa Mama la dhana ya Matokeo makubwa Sasa;BRN inayowachanganya viongozi wetu wengi!)

Ukimuhukumu EL na kujaribu kushawishi wana CCM; CC; NEC na mkutano mkuu wa CCM "wamchinjilie mbali EL" kisa tu hakutamka kwamba moja ya agenda zake pindi akiteuliwa na hatimaye kuwa rais wa tano wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ni "Kupambana na Ufisadi; Ufisadi na Ufisadi ni sawa na kutwambia kwamba "kutamka ni sawa na kutenda"!! aaaah wacha masihara Muzee; hiyo miujiza ni ya enzi za Nabii Issa Muzee mwanakijiji!! Wangapi wametamka na wakashindwa kufuatilia kauli zao kwa vitendo!! to talk is one thing; Mzee Mwana kijiji; BUT to walk the talk is quite a different creation Muzee wangu!!!

Hebu rejea kauli hizi: Ari mpya; Nguvu mpya na kasi mpya; tafsiri yake rahisi ni nini?!; Nina list ya Wauza mihadarati wote; wanapeta nje nje! Kinara wa ujangili yuko pale Arusha; lini alikamatwa?!; Tanzania bila Ukimwi inawezekana; Ukimwi uliisha lini?! Maisha bora kwa kila Mtanzania; yako wapi?! Kura ya maoni ya katiba pendekezwa ni April 2015; iko wapi?! Kura ya maoni iko pale pale; iko wapi?; tutakomesha mauaji ya watu wenye Albinism!; robo ya kwanza ya mwaka huu tumeshuhudia mauaji ya kutisha ya Albinos!

Nimetangulia kusema awali kwamba do not jump the gun! huyu EL ni wa kumsubiri kwenye campaign trail ikiwa atateuliwa kupeperusha bendera ya CCM: hapo abanwe kulia na kushoto kuhusu ufisadi na tuhuma mbali mbali za ufiadi zinazomzunguka yeye mwenyewe, wanahabari wacheze sehemu yao, wananchi kwenye mikutano ya kampeni; ndani ya midahalo na mitandao ya kijamii, atwambie kinaga ubaga agenda yake pana akiwa Rais; ufisadi included; mikakati ya utekelezaji wake na time frame.ni lazima pia atwambie mahusiano yake na watu wanaomzunguka ambao wana tuhuma lukuki za ufisadi pia na jinsi atakavyotnganisha kazi zake Ikulu na urafiki wakwe na watu hao!

tukifika mahali tukakubali as a nation mtu akatoa kauli tukashangilia tu kama mazuzu ili mradi katamka; bila kuhoji, kuuliza maswali magumu na kudai taarifa za utekelezaji na majibu husika tutakuwa tumekwisha kabisa na hilo ndilo lililotufikisha hapa tulipo!!

Elimu kwanza; yees! Elimu inajenga kujiamini kwa sababu mtu anakuwa anajua anachokisema kwa sababu amekifanyia kazi! anajua wapi kwa kupata taarifa sahihi; Elimu hiyo ndio itakayotuwezesha watu wetu kudai elimu ya uraia; kuhoji matumizi mabaya ya raslimali za umma; viongozi wetu kupenda starehe na kuishi nje ya uwezo wao (ostentation!); kudai nafasi yao sahihi katika uopngozi wa nchi yao; kukataa kufanywa watwana na viongozi wao; kusisitiza haki sawa kwa wanachi wote; kukemea usiginwaji wa haki za binadamu na demekrasia; watu wasio na elimu ya kutosha; elimu bora sio bora elimu katu hawawezi kuhoji ufisadi kwa sababu hawajiamini na hawana taarifa sahihi; kwa hiyo ni waoga ni rahisi kudanganywa na kukubali vizawadi zawadi vya kanga duni na fulani cheap na kazi yao ni kupiga makofi tuuu!

Muzee mwanakijiji; hebu vipange vipaumbele vyako vizuri zaidi, ufisadi ni mbaya ndio, EL huenda sio msafi ndio! lakini "wrong diagnosis leads to a wrong perscription"; dakitari akikosea kutambua ugonjwa lazima atatoa dawa ndivyo sivyo! mgonjwa atakufa mwana kijiji.
Mzee mwanakijiji; nina maoni mazito; (strong opinion) kwamba katika maswala nyeti ya nchi; You have your priorities TOP SIDE DOWN!!!!; hakuna kama elimu; it is second to none! Elimu hujenga kujitambua; kujiamini; kuweka vipaumbele sawasawa; kuwa na maono mapana kuhusu maisha na dunia kwa ujumla; not vice versa.

Hivi ushawahi kufikiria itamchukua Lowassa miaka mingapi kwa his 'education first policy' to yield results unazozungumzia wewe za kuongeza idadi ya watu wanaohoji ufisadi. Itamchukua not less than five years, ambayo ndio miaka ya Rais kukaa madarakani kabla ya uchaguzi mwingine.

Kwa maana hiyo, ndani ya huo mda tunategemea idadi ya watu 'almost' ileile watakaokuwa wanakemea ufisadi kwa mfano akiwa madarakani. Kwahy 'elimu kwanza' can never be an effective tool for fighting money laundering and corruption for five years'.

However this does not negate umuhimu wa elimu kwa wananchi. Pia the issue at hand ni ukosefu wa uadilifu kwa Lowassa. Lowassa anadhani watu wengi hawana uelewa na hawana elimu au ni wajinga ndio maana pamoja na historia yake ukosefu wa uadilifu bado anang'ang'ana kutaka kuwania uRais.


A message to Lowassa:

"You can fool all the people some of the time, and some of the people all the time, but you cannot fool all the people all the time" Abraham Lincoln
 
...Lowassa hafai hafai kabisa....na inasikitisha kama taifa mtu huyu ambavyo kuna watu wamejitoa ufahamu kumsafisha ili tu agombee urais...
....Huyu mtu hafai kuwa rais kwa kuchafuka tu pale alipoachia uwaziri mkuu kwa kashfa ya richmond....Inasikitisha leo eti anapata nguvu ya kutoka na kutaka kujisafisha eti hakuhusika na richmond!!....yaani mtu aachie uwaziri mkuu kwa kashfa alafu leo tumwone msafi???....eti anasema walimchafua...eti waliutaka uwaziri mkuu???...really???kwanini wautake uwaziri mkuu wake???...yeye nani hadi watu wautake uwaziri mkuu wake kipindi kile???....Inasikitisha sana watanzania wanavyofanywa wajinga kuwaamini hawa wezi wa mali za umma....

....Lowassa anasema eti yeye hapendi umaskini anapenda utajiri???.....yaani mtu aibe tu ili kuupata huo utajiri ...yeye kwake Lowasa hilo sawa tu....Ndio maana huwezi kumsikia Lowassa anakemea rushwa/ufisadi....maana yeye huo kwake ni njia ya kuupata utajiri anaoupenda yeye...Mtu wa fikra hizi akipewa urais si anauza nchi kwa gharama zozote....ili raia/watu wake wawe matajiri.....

....Kwa mtu makini anaemsikiliza Lowasa unaona kabisa ni mtu mchafu anaetumia nguvu nyingi kujisafisha ili kupata haki ya kugombea urais TZ...mtu wa namna hii hafai...maana mtu msafi hatakiwi kuhisiwa kuwa mtu wa rushwa/ufisadi....kwanini yeye Lowasa ahusishwe na ufisadi???kwanini yeye???who is he??..lazima maswali haya watanzania wahoji kabla ya kufanya maamuzi ya kumfagilia fisadi kuwa rais...

...kule ccm waliwahi kumhusisha Lowasa na kuvuana magamba....hili nalo limesahauliwa???..hili Lowassa atalisemeaje??

...Wanaosema eti kama Lowassa fisadi ashtakiwe....watanzania hawajiulizi ni mafisadi wangapi wameshtakiwa TZ???...kama mfumo waliojiwekea watawala wanashindwa kushtakiana vipi watu hawa waonekane wanafaa....

....Juzi wamepeana eti adhabu huko ccm wale walioanza kampeni....adhabu gani hizo wakati wote leo wanakubaliwa wagombee??....ni utaratibu gani huu ukubalike wakati watu hawaadhibiani pale wanapofanya makosa???

....Taifa hili linahitaji fikra za mabadiliko hakika...kabla ya kufikia kufanya maamuzi kama haya ya kutafta wagombea urais....Watu wanaowafagilia wezi kwenda ikulu hawana uwezo wa kuchagua viongozi bora....

...Mwisho...Mkiniuliza nani anafaa agombee urais TZ....nasema ni mtu mmoja tu..nae ni Mh.Tundu Lissu....maana lazima tunapotoa critics tuwe na mbabala....
 
Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. "

Hii kitu inashangaza sana sababu nae hajaenda hata mahakamani kuhusu kesi ya ufisadi
 
Tujipe matumaini tena kama elimu ya kweli imeepukwa, ufufuaji utaanzishwa tena na mizani mpya itapatikana baina ya elimu kama njia na elimu kama lengo la mwisho katika uzoefu wa kisiasa Tanzania. Muda na wakati ndio huu wa kuchagua kiongozi anayefaa kuongoza Tanzania kwa kuzingatia uwiano wa kitamaduni wa mtanzania (Tanzanian cultural compatibility), uungwana (propriety) na uhalali (legitimacy) wa kuwa raisi wa JMT.

1.Pamoja na Elimu lakini pia Ufisadi,Uchumi,Kupunguza matumizi yasiyo muhimu serikalini, kupunguza mzigo wa kodi kwa mwananchi , Kilimo (kuondoa bla bla za siasa kwenye uchumi), ziwe Agenda kuu kwa Rais ajaye.
2.Naomba unisaidie kufafanua una maana gani kwenye nyekundu.
 
edward-lowassa.jpg


watanzania wanajaribu kuaminishwa kuwa lowassa anafaa kuwa rais wa tano wa jamhuri ya muungano wa tanzania. Wanaaminishwa kuwa ana maono ya kiuongozi ambayo yakitumika yanaweza kulinasua taifa letu toka hapa lilipo. Wanajaribu kuaminishwa kuwa lowassa ni kiongozi bora ambaye watanzania wanapaswa kumwangalia kwa matumaini - ndio maana ya "safari ya matumaini".

Wapo kati yetu ambao wameshazugika na pendekezo hilo na wamekuwa kama waliorogwa hivi. Wapo baadhi yetu kwa muda wote wa uongozi wa lowassa (hasa baada ya kuwa waziri mkuu na baadaye) tuliona kile ambacho labda kimefichika kwa wengi - lowassa hafai.

Hii si hukumu juu ya utu wake, heshima au ubinadamu wake; ni hukumu juu ya uongozi wake na maono yake kama kiongozi. Kumkataa lowassa, maono yake, uongozi wake na fikra zake siyo kumchukia yeye kama mtanzania mwenzetu au kama binadamu. Ni kuwa na tofauti naye na vile anavyowakilisha kiasi kwamba tofauti hizo hazijawezi kupatana (irreconcilable differences).

Katika siasa ni lazima tuheshimu uwepo wa tofauti hizi na tuelewe ndio msingi wa kutafuta viongozi bora zaidi au chama bora. Kwa kadiri yeye atakavyojaribu kujiuza ndivyo na sisi wengine tutazidi kuonesha kuwa hauziki au zaidi hanunuliki. Hii si chuki ni tofauti tu ya msingi (fundamental difference).

Pendekezo langu linatokana na hili; kwamba zipo na zimedumu tofauti za msingi kati ya maono ya baadhi yetu na maono ya mgombea huyu mtarajiwa kutoka ccm. Tanzania haihitaji maono na uongozi wa lowassa kwa sababu nyingi tu; nitaanza na moja ya leo na nitaendelea kwenye mada hii hii kila ninapopata nafasi hadi jina lake litakapotupwa na nec na yeye akaendelea kuwa waziri mkuu wa zamani.

Mara kwa mara baada ya sakata lake na katika jitihada za kujirudisha katika umuhimu (relevance) lowassa amekuwa akizungumzia mwelekeo wa sera zake na kitu kitakachomuongoza. Aliamua kwenda kinyume na mwelekeo wa serikali ya chama chake ambayo iliweka mkazo kwenye "kilimo kwanza"; yeye ameamua kuja na hoja ya "elimu kwanza".

Alielezea kupinga kwake hoja ya kilimo kwanza miaka michache nyuma alipohojiwa katika kipindi cha dakika45 (kinachorushwa na itv). Alinukuliwa kusema "mpango huu wa kilimo kwanza umekosa nguvu kwa sababu kuanzishwa kwake hakukuzingatia dhana ya ukombozi wa mwananchi wa kawaida. Tangu awali ndani ya chama (ccm) nilieleza kuwa sitaunga mkono hoja hiyo mpaka kuongezwe mashiko na kuwa elimu kabla ya kilimo kwanza"

hoja hii ameirudia tena juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari ambao bila ya shaka wengi wamekuwa 'charmed' na wingu la umaarufu wa lowassa kiasi kwamba hakuna ambaye ameweza kumbana vizuri kwenye maswali. Anasema endapo atachaguliwa basi ataelekeza nchi kwenye "elimu kwanza"; kwamba hiki ndicho kipaumbele chake.

Ndio maana sisi wengine tunasema hafai; kwa sababu inaonekana siyo yeye wala chama chake ambao wamelielewa vizuri tatizo linaloikabili tanzania; tatizo ambalo limeielekeza (orient) tanzania kufuata njia ya nigeria. Kwamba tunaweza kabisa kutengeneza uchumi wenye nguvu lakini wa taifa lenye umaskini uliokithiri, lisilo na usawa na la wasomi wasioweza kulipeleka taifa mbele. Tutakishia kujisifia wingi wa wasomi ambao wengi wataishia kwenda nje ya nchi kutafuta maisha. Taifa ambalo litakuwa limegawanyika sana kama nigeria - licha ya kuwa na wasomi wengi.

Lowassa inaonekana ameshindwa kuelewa au hataki kukubali kuwa tatizo kubwa la tanzania ni la aina tatu:
1. Ufisadi
2. Ufisadi
3. Ufisadi

lowassa hatopambana na ufisadi kwa uzito unaostahili kwani haoni kuelewa kuwa ni tatizo la hatari zaidi kwa taifa "kuliko vita wakati wa amani" kama alivyosema baba wa taifa mwalimu nyerere. Kutokuelewa kuwa ufisadi ndiyo sekta haramu yenye nguvu zaidi katika nchi yetu ni kushindwa kuelewa tatizo letu hasa ni nini. Ufisadi umepenya (permeate) kwenye kila sekta nyingine zote (rasmi na zisizo rasmi). Umeathiri elimu, afya, usalama, na hata umoja wa taifa. Kutokulielewa tatizo hili kwa mtu anayetaka kugombea nafasi ya urais (haijalishi anatokea chama gani) ni kutokuelewa namna ya kukabiliana na changamoto nyingine zote.

Kwa sababu hii peke yake lowassa na mgombea mwingine yeyote ambaye haweki "ufisadi" kama ajenda yake ya kwanza na kubwa zaidi basi hafai. Kwa sababu atatuzungusha kwenye madudu mengine yote isipokuwa kwenye kumkoma nyani giledi.

Kikwete - kwa wanaokumbuka - alishabikiwa na wengi si kwa sababu ya "ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya" bali zaidi kwa kuwapa watanzania matumaini kuwa atashughulikia ufisadi vikali. Hotuba yake ya kulifungua bunge na ile ya ngurdoto na zile ziara zake za kutembelea wizara ziliwafanya watu waamini kidogo kuwa hatimaye "kipele kimepata mkunaji". Leo hii miaka tisa baadaye ripoti ya cag imeonesha kidogo tu kuwa tatizo hili la ufisadi halijapata mtatuzi ndani ya ccm na hata mtu anayeshabikiwa sana kuwa ati anaweza kuwa rais inaonekana tatizo hili limempita kabisa.

Nikisema "hafai" simsingizii; nasema kilicho dhahiri; i'm just stating the obvious.

wanaomtaka lowassa - wapenzi, mashabiki na waumini wake - watuambie vita dhidi ya ufisadi ina umuhimu na uzito gani katika agenda za lowassa. Wakituambia kuwa "ni mojawapo" ya mambo atakayoyashughulikia tuendelee kumkataa kwa sababu bado atakuwa hajaelewa tatizo letu hasa ni nini kama taifa.

Nitandelea...

Nb: Kwa wageni wa hoja hizi warejee mada yangu ya 2007: kikwete siyo safi, yes i said it


mleta mada umejaribu kujenga hoja na kuonesha vipaumbele,at the sametime kuonesha jinsi kikwete alivyoanza kwa pupa na kuishia ukingoni,kipaumbele ni dira ya mtu anachotaka kufanya,na hapa bila elimu tatizo la ufisadi haliwezi kuisha,so kumbe ni vizuri kuboresha elimu,watu wakaelimika,ukaongeza kwenye mitaala topic kuhusiana na rushwa/ufisadi ni adui wa taifa kumbe itaanza kujengwa kuanzia kwenye grassroot,then kwanini useme hawezi kupigana na ufisadi?
Nimekupa kwa kifupi nitaendelea tena ukija na part2 yako
 
Hivi Lowasa anataka kuwa prove wrong wapinzani wake kwa lipi hasa? Kumbukeni kisa cha yeye kutofautiana na Nape Nauye ni nini? Akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Umoja wa vijana wa CCM alipiga dili kulikodisha kama si kuliuza kabisa eneo la Umoja wa Vijana wa CCM pale Morogoro road bila idhini ya Baraza kuu la umoja huo akishirikiana na aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM Emmanuel Nchimbi na kupewa baraka zote na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM Mzee Yusuph Makamba. Inashangaza ni kwa nini Wahariri wa vyombo vya habari hawakumuuliza maswali haya ya msingi. huyu jamaa hafai hata kidogo.
 
EL DEFENCE agaist corruptin allegastions cant hold water by any means BUT since we tanzania are people of forgive and forget almost of voter will vote for him. Watanzania wengi vichwa tikiti maji na wataongozwa na tikiti maji majuto ni mjukuu, mashabiki wa El mitandaoni hawana la kujidaia zaidi ya kwakua wamenunuliwa. J k kasema vijana chungeni na kuwa makuwadi na madalali wa wagombea uraisi.WATETEZI WA LOWASA ALMOST NI MAKUWADI NA MADALALI WAKE HAKUNA ZAIDI YA HILI. What mwanakijiji wrote is nothing rather than truth itself. SITAFIKIRIA KUMCHAGUA MWIZI. My country get well soon on this.
 
Hivi Lowasa anataka kuwa prove wrong wapinzani wake kwa lipi hasa? Kumbukeni kisa cha yeye kutofautiana na Nape Nauye ni nini? Akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Umoja wa vijana wa CCM alipiga dili kulikodisha kama si kuliuza kabisa eneo la Umoja wa Vijana wa CCM pale Morogoro road bila idhini ya Baraza kuu la umoja huo akishirikiana na aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM Emmanuel Nchimbi na kupewa baraka zote na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM Mzee Yusuph Makamba. Inashangaza ni kwa nini Wahariri wa vyombo vya habari hawakumuuliza maswali haya ya msingi. huyu jamaa hafai hata kidogo.

Lowasa alishatoa maagizo ya kubomolewa kwa maghorofa mawili pale Masaki kwa masilahi yake binafsi hususan kulinda hadhi ya nyumba yake kwenye hilo eneo. Maagizo hayo tata yameligharimu taifa letu mabilioni ya shilingi kwa ajili ya kulipa fidia lakini kwake hilo haoni kuwa ni tatizo.

Kuna mengi ambayo Lowasa amefanya kwa masilahi yake binafsi na yameendelea kuligharimu taifa letu ikiwemo ubinafsishaji wa ranchi za taifa na kiwanda cha Tanganyika Packers. Kwa ujumla huyu jamaa hafai kabisa na ni mmoja kati ya watu wanaotakiwa kuburuzwa mahakamani kama mhujumu uchumi
 
mimi kwangu hamna jipya ulilolisema na ninajua fika ya kwamba bw.lowasa ni fisadi lakini bado nitampa kura yangu kama akigombea, na sababu ni rahisi tu sioni mbadala wake, kama ni mbowe pia aniaambie ni kwa nini alisema serikali inafuja mali ya umma kwa kununua mashangingi akarudisha lake na kulichukua tena na mpaka leo hii analitumia na juzi alikutwa nalo mombasa, kenya likiwa na namba za kiraia, je yeye siyo sehemu ya ufisadi unaofanywa na serikali aliokuwa analalamikia? Na kama akiwa raisi au chama chake atwezaje kuondokana na ubadhirifu huu kama sasa hivi ameshindwa?

Hilo la kwanza la pili serikali ya kifisadi ya ccm inaongeza mishahara na marupurupu kwa wabunge wote na wa upinzani sijasikia mbunge yoyote yule kuanzia wa upinzani wanaomuita lowasa fisadi mpaka wa ccm akilalamikia hii dhuluma siajabu kubwa kulko yote tanzania kwa maana majimbo ya akina tundu lisu haya zahanati wala dawa lakini yuko kimya kwenye hilo, hivyo maadamu mimi sipati majibu ya maswali kama haya basi mimi kura yangu mpaka sasa hivi ni fisadi lowasa tu angalau namjua kuliko hawa nisiowajua!


too low
 
kiatu cha Urais kinapwaya kwa Lowassa hata aweke na matambara hawezi vitembelea ni vikubwa kumliko atatucheleweshea maendeleo tunayoyalilia usiku na mchana.
 
Nikisoma hii thread na comment zake kichwa kinaniuma,,,,Hii nchi ngumu sana
 
Aliyeisha cheza ngoma, aisikiapo mabega hayaachi kucheza. Mtu huyu EL ameishacheza ngoma ya ufisadi utake usitake. Ikulu kuna uwanja mpana atacheza zaidi, nchi itaumia. Sikieni maneno yake. Utajiri alionao eti bado anasaka utajiri. Jamani atueleze nini? Huyu ni fisadi tu. Hataacha akiwa Ikulu ndiyo atazidi. Mashahidi wake ni mafisadi wenzake wa ng'ambo akina Hillary. Twafa. Mola ipe uoni CCM wasimchague mtangaza nia huyu EL.
 
Mzee Mwanakijiji ametimiza wajibu wake... kilichopo ni kwamba, endapo mathalani MM angepewa uwezo wa kupiga kura 25 million peke yake na kura hizo pekee kuamua mustakabali wa rais wetu, basi kwa mujibu wa MM ni kheri kura hizo zote aziharibu kuliko kumpa Lowasa! Kinyume chake, kuna wengine endapo wangepewa uwezo huo wa kuhodhi kura 25 million peke yao, basi haijalishi Lowassa anasimama na nani... zote hizo wangempa Lowassa! Haidhuru, kura hizo 25 million tunaweza kuziita a powerful veto vote yenye uwezo wa kuamua nani awe rais bila kuhitaji kura ya yeyote ya ziada... ni tofauti na ile ya UN yenye uwezo wa kukataa peke yake! Hapa ndipo unaposimama umuhimu wa hoja ya MM, haidhuru hata kama Lowassa, hatimae atashinda kwa kishindo hata kama ni kwa 95% na zaidi... bado haitaondoa ukweli wa Lowassa kwamba hafai; si tu kwa mujibu wa Mzee Mwanakijiji bali kwa mwingine yeyote yule ambae hana amtakae kwenye kinyang'anyiro hiki; iwe kutoka chama tawala au upinzani!

I hate to say this lakini ukweli ni kwamba, hata kama JK nae alikuwa fisadi kabla ya hata kuingia magogoni but JK was smart enough as compared to EL! He's smart enough coz' huku mtaani haikufahamika hivyo kwa wengi... Kama alikuwa na tuhuma zozote za ufisadi basi tuhuma hizo ziliweza ku-circulate only among few people... sina shaka hata chembe kwamba hili lilichangiwa sana na zama zenyewe... hazikuwa zama za free flow of information kama ilivyo sasa! Katika hali ya ajabu kabisa, Lowassa anaonekana kuwa the most stupid accused corrupt leader seeking the highest position in the country... YES, I repeat, the most stupid accused corrupt leader seeking the highest position in the country!!! He's top of the stupid accused as a corrupt leader because, pamoja na kwamba kila mtu anafahamu tuhuma za ufisadi dhidi ya Lowassa lakini bado ame-opt ku-side or team up with ALL other accused corrupt leaders! Sitamtaja Serukamba kwa maana yeye ni mganga njaa anayeweza kutumiwa na yeyote yule lakini hakuna nchi hii asiyefahamu tuhuma chafu za ufisadi dhidi ya Rostam Aziz lakini pamoja na yote hayo huyo ni one of the insiders or probably Master-minder wa Lowassa katika kuingia Ikulu! Hakuna hata mmoja Tanzania hii anayefuatilia siasa za Tanzania asiyefahamu tuhuma za ufisadi wa Andrew Chenge... lakini huyu nae ni insider au bila shaka ni Senior Tactic Team Member wa EL katika mbio zake za urais! Hakuna anayefuatilia siasa za nchi hii asiyefahamu tuhuma za ufisadi dhidi ya Nazir Karamagi! Huyu nae ni insider au bila shaka nae ni one of the Senior Tactic Team Member wa EL katika mbio zake za Ikulu! JK hata kama alikuwa na tuhuma za ufisadi, hakuwa mpumbavu kiasi cha upumbavu unaoneshwa na Lowassa na ndio maana wala hakuona taabu wala aibu kumkwepa EL na kumwacha afe peke yake kwenye tuhuma dhidi ya Richmond!

Swali ambalo sijapata ni jibu ni message anayokusudia Lowassa kui-deliver kwa Watanzania hususani wale wanaofuatilia siasa za nchi hii! Kwamba, yeye binafsi, Rostam Aziz, Andrew Chenge, Naziri Karamagi wote hawa kwa umoja wao wanasingiziwa na hivyo wameamua kusimama pamoja ili , pamoja na mambo mengine they mean to reveal their innocence to the public? Au labda anataka kutuma ujumbe kwa wafuatiliaji wa siasa za nchi hii kwamba, fuc'k ya'll (fuc'k ya Tanzanians) we don't care what you think or know about us na kwamba kwa umoja wetu we'll stand firm and fight for this post?! Ni ujumbe gani hasa EL anaokusudia kuuwasilisha kwa Watanzania?!

Akili, busara ukichanganya na uungwana wa kawaida hautamfanya mtu kuhoji kwamba, let's say huyu Mheshimiwa EL anasingiziwa... ni mazingira gani yanayosababisha awe ni yeye tu wa kusingiziwa tena wakati mwingine kwenye official platforms kama vile bunge!
Mkuu chige, asante kwa bandiko hili, very objective, ila kwa vile Mzee Mwanakijiji, aliwahi kusema hivi hivi kumhusu JK na JK ndie akawa rais wetu, na tukimtumia JK kama terms of comperative na Lowassa, Lowassa is much better 10 times kuliko JK.

Kama hoja dhidi ya Lowassa ni ufisadi wa Richmond, naomba kanisome hapa,
[h=3]Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa.[/h]Thanks.

Pasco
 
dah watanzania mna kazi aisee kama hizi ndizo arguments zenu kumsupport Lowasa!
 
Back
Top Bottom