Wewe utakua na matatizo kichwani mwako. Ama sijui unatumia nini sijui kufikiri.
Mtu mwenye akili timamu hawezi kushabikia mabaya yampate binadamu mwenzie, haijalishi ana ubaya kiasi gani,
Huo sio utamaduni wetu waafrika, hasa Tanzania
Mtu kapata minor road accident mnasema kanusurika kufa........! Hii maana ya kunusurika kufa sasa inapotoshwa
kanusurika kufa kwa sababu amepata minor road accident,sasa sijui ulitaka heading iweje ebu tusaidie.
Mhe. Mbunge wa Monduli na aliyewahi kuwa. Waziri Mkuu Bw. Lowassa amenusurika na ajali akiwa anaenda kwenye harambee mjini Morogoro. Kwa mujibu wa ITV, Mhe. Lowasa amenusurika baada ya basi lililokuwa likifukuzia jingine kutaka ku"overtake" kulikwangua gari alilokuwemo Mhe.Lowasa ambae amekiri kwa sura ya unyonge kuwa kupona kwake ilikuwa ni mipango ya Mungu. Kauli hiyo ya Lowasa inaashiria uenda kulikuwa na mkono wa mwanadamu kwenye ajali hiyo ambapo kwa kuwa mkono wa Mungu ulikuwepo husingeweza kufua dafu!!
Pole sana mhe Lowasa.
Gari imeoneshwa kwenye tv imepigwa pasi kidogo tu maneno mengi utafikiri ilikuwa ajali ya kutisha
Mkuu Makamuzi,
Heshima mbele. Shule imebana sana Mkuu wangu. Huwa nachungulia tu humu mda wa kuchangia huwa sina. Hapa nilipo sasa hivi kuna desa nalikamua kimtindo nilipoona stimu zimepotea nimeamua nizifutue humu nikiendelea kulisoma. Pamoja sana Kamanda.
Salamu nyingi kwa Watanzania wenzangu.
Ujumbe: Endeleeni kuitwanga serikali, kuanzia Mtwara hadi Arusha. Kuanzia Kigoma hadi Morogoro. Kuanzia Mwanza hadi Mbeya, nk.
Duh...hiyo kali kuliko!!Kama hujui hiyo tofauti basi ww pia umenusurika kufa
Wewe utakua na matatizo kichwani mwako. Ama sijui unatumia nini sijui kufikiri.
Mtu mwenye akili timamu hawezi kushabikia mabaya yampate binadamu mwenzie, haijalishi ana ubaya kiasi gani,
Huo sio utamaduni wetu waafrika, hasa Tanzania
Kama Mungu angehesabu maovu yako usingekuwa na dakika hata moja ya kuishi, kwanini ufurahi kifo cha mwingine Mungu mwenyewe hataki watu wafe katika dhambi wewe unani kumnyoshea kidole mwenzako hukumu hiyo si ya haki,tubu kwa Mungu.Pole mheshimiwa tunashukuru umepona na wengine.Du hilo basi lingefanya kweli tungepunguza fisadi mmoja mkubwa na hatari! Mungu atusaidie ipatikane fursa nyingine ya kuondokewe na fisadi huyu mnafiki anayejifanya kuchangia makanisa wakati akiwaibiwa watanzania. May you perish fisadi!