Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

1000096720.jpg

Academy imepata mfungaji hodari kazi kwake Page kumsuka mapema atue Team ya wakubwa aanze mishe. Dogo ana miaka 17 hivyo hayupo mbali sana kutua timu ya wakubwa.

YNWA
 
Tetesi za Soka Ulaya Jumatano: Je, Man Utd kumsajili kipa wa New Castle?
Dakika 54 zilizopita
Manchester United ina mpango wa kumsajili kipa wa England Nick Pope, 33, endapo Newcastle itakamilisha dili la kumsajili mlinda lango wa Southampton 27 Aaron Ramsdale, 27. (Sportsport)

Newcastle imekubaliana na Southampton kumsajili Ramsdale kwa mkopo na chaguo la kufanya mkataba huo kuwa wa kudumu mwishoni mwa msimu huu. (Athletic - usajili unahitajika)

Manchester United pia ina nia ya kumsajili mlinda lango wa Paris St-Germain na Italia Gianluigi Donnarumma, lakini inasita kujitosa kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 na Manchester City . (Sun)

Arsenal bado inamtaka winga wa Uingereza Eberechi Eze, 27, lakini haiko tayari kutimiza masharti ya kulipa ada ya zaidi ya £60m hadi Crystal Palace itakapopunguza bei ya mchezaji huyo. (Athletic - michango inahitajika),

Manchester City imekataa dau la pauni milioni 25 lililowasilishwa na Nottingham Forest kumsajili kiungo wa Uingereza James McAtee, 22. (Sky Sports)

Paris St-Germain imepiga hatua katika juhudi za kufikia mkataba na Bournemouth kumsajili beki wa Ukraine Illia Zabarnyi, 22. (Fabrizio Romano)

Borussia Dortmund inafuatilia hali ya winga wa Arsenal Leandro Trossard, 30, lakini mshambuliaji huyo wa Ubelgijy pia anasakwa na vilabu viwili vya Ligi ya Premia. (Sky Sports Germanu)

Klabu ya Lyon ya Ufaransa inavutiwa na kiungo wa Uingereza Tyler Morton, 22, na tayari imewasiliana na Liverpool. (Times)

Manchester United iko tayari kukubali punguzo la ada ya £17m kwa Jadon Sancho, 25, huku klabu za Borussia Dortmund na Juventus zikimuwania winga huyo wa Uingereza. (Mail)

United imesitisha mpango wa kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Nicolas Jackson, 24, kwa sababu mchezaji huyo wa kimataifa wa Senegal anataka mshahara mkubwa kupita kiasi. (Mirror)

Napoli inamtaka kiungo wa kati wa Manchester City Jack Grealish, 29, lakini inakabiliwa na changamoto ya kufikia mshahara ikizingatia orodha ya wachezaji inaowalenga kama winga wa Chelsea na Uingereza Raheem Sterling, 30, na mshambuliaji wa Manchester United wa Argentina Alejandro Garnacho, 21. (Gazzetta dello Sport - kwa Kiitaliano)
 
Right now we need CB than DM

Anayelinda ni DM, CB yeye kazi yake ni kuokoa tu pale ulinzi wa DM unapopitwa.

Sasa unataka DM iwe dhaifu ili muda wote mabeki wawe wanokoa tu kama msimu uliopita?

Imarisha DM kuzuia mashambulizi ili mabeki iwe rahisi kwao kuokoa yake mashambulizi machache tu yanayopita kufika kwao kama ilivyokua wakati wa Fabinho.

Hivyo sisi hatuhitaji kuimarisha kuokoa mashambulizi bali tunahitaji kuimarisha kuzuia mashambulizi
 
🚨
𝗡𝗘𝗪 - @Tanziloic: Lyon have reached an agreement with Tyler Morton but are still negotiating with Liverpool. Talks with the club remain ongoing and complex as OL look to secure the England U21 midfielder.
 
Liverpool: Mamardashvili, Van Dijk, Konate, Szoboszlai, Salah, Gakpo, Gravenberch, Ekitike, Kerkez, Wirtz, Bradley.
 
UJUMBE WA LUIS DIAZ

Miaka mitatu na nusu ambayo nitaithamini milele. Nilikuja nikiwa na ndoto zote za dunia, na sasa ninaondoka nikiwa na fahari kwa yote tuliyofanikisha pamoja.

Nimekutana na watu wa wazuri, wachezaji wenzangu wa kuvutia, makocha waliyonisaidia sana, na mashabiki wa kipekee. Liverpool ni timu ya kipekee kweli, na nitawahifadhi wote moyoni mwangu. Safari yangu inaishia hapa, na ni jambo la kuridhisha sana kuangalia nyuma na kutambua furaha tuliyokuwa nayo.

Sio tu kwa sababu ya makombe tuliyoshinda, bali kwa mshikamano na urafiki uliotuwezesha kufanikisha kila kitu. Kulikuwa na nyakati nzuri na mbaya, kama kawaida ya maisha, lakini daima kulikuwepo na ukweli. Kama inavyopaswa kuwa kwenye familia. Inatia moyo kuondoka nikiwa na hisia za kutimiza wajibu, na zaidi ya yote, kuondoka nikiwa bingwa. Ingekuwa kwaheri kamilifu kama tusingempoteza mmoja wetu kwa njia ya kusikitisha sana.

Kama nilivyosema, na narudia, nawabeba nyote moyoni mwangu, lakini mmoja hasa: Diogo. Sitamsahau kamwe. Hatutamsahau kamwe. Asanteni kwa kila kitu.
YNWA🔴

CHANZO: LUIS DIAZ
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom