Liverpool ya kuchukua treble ilikuwa ni hii..👇
View attachment 3267535
Hii ingeweza kuchukua hata makombe yote manne, sema walikuwa wana bahati mbaya ya kukutana real madrid baba mwenye nyumba wa UCL, na pia huku EPL walikuwa wana compete na man city..
...kwanza hakuna timu ambayo iliweza kuwa outplay anfield kama alichokifanya PSG jana... nakumbuka hata kwenye EPL baada ya kudroo na chelsea mwezi january wakaja kudondosha point dhidi ya city mwezi April kwenye mechi ambayo iliamua hatima ya ubingwa, kwenye mzunguko wa pili hawakupoteza mechi.
Sidhani kama Liverpool watakuja kupata timu yenye ubora ule 21/22 kwa hii miaka ya karibuni hapa... hii ya sasa ni merely above average wala hata sio tishio, angali hata jinsi walivyoteska dhidi ya United hii mbovu, angalia wakikutana na timu imara kama Nottingham wanavyohaha... hii hata Arsenal hawawezi kutufunga si tuko hapa.
Kilichofanya hii liverpool iwe hapo ilipo na kuwadanganya pundits wengi kuwa ndio timu bora kwa sasa ni inconsistency ya Arsenal ambayo imetokana na game approaches mbovu za Arteta, ila kimsingi Liverpool alipaswa kuwa nafasi ya pili akitofautiana kidogo na Arsenal.... nimemaliza.