Before klopp… ucl ilikua ya kubahatisha…. If we can’t see his value Basi tuna tatizo kubwa
Hakuna mtu anayebisha juu ya alichofanya Klopp labda unajitoa ufahamu tu.
I myself im among who still believe he will give us trophies. Ila ukweli lazima usemwe. Klopp amezingua mara nyingi sana hata kwenye ukweli.
Hivi unataka makombe unahangaika kubaki na
Henderson
Milner
Keita
Ox
Gomez
Jones
For years, hata kama quality yao imeshuka? Hapana hapa Klopp katudanganya sana. Ishu ya TAA iliongelewa last two seasons amekomaa naye na ameiathiri timu sana maa alikuwa exposed mno, shida sio TAA shida Klopp. As coach lazima ujue namna ya kumtumia mchezaji wako pamoja na mapungufu yake ili akupe alicho na uwezo nacho. Na baada ya hapo tuliona last 10 matches vile TAA alileta utofauti kwenye timu, akiwa as inverted MF.
Pep anayabeba makombe kwa sababu hana ubaba ana ukocha haswa . Sifa moja ya kocha ni kuweka nidhamu kwenye timu na kuondoa upendelo na imemlipq hasa. Enzi za Sir Fergie, kina Mou tuliona even stars of the timu wakisugua bench au kuuzwa kama mchango wao na Klabu utaonekana kushuka.
Lakini hii imekuwa na utofauti sana kwa Klopp, kiasi cha kuzidiwa kete na wachezaji.
Hivyo basi, utambue Klopp ana heshima zake ila kwa misimu minne katudanganya sana. Timu kukaa bila kusajili quality players kwa yeye kusema ana kikosi, kumbe ni (quantity over quality). Haiwezekani timu iliyocheza 70% mwaka 2018 mpaka leo uwe nayo, kuwa nayo sio tatizo bali wameshakwisha uwezo wao. Na hii ndio imefanya tuone mwaka huu tunahitaji usajili mkubwa.
M. Edward alitofautiana mtizamo na Klopp hakutaka kina Henderson, Gomez waongezewe mkataba mrefu kwa sababu ya umri na kiwango chao. Plus Milner kuongezewa mkataba, akaamua kuondoka kwan Klopp aliwang’ang’ania.
Huyu huyu Klopp, alitudanganya kwa Melo, kasajiliwa kacheza less than 30 min tena kutokana na kulazimishwa na majeruhi. Ilikuwa mechi vs Napoli. Klopp huyu huyu alitaka Milner aongezewe mkataba Klabu ikamchomolea nje, alitaka Bobby aongezewe mkataba Bobby akamchomolea nje.
Sasa kwa madhaifu kama haya ya kocha kwa nini asilaumiwe????
NB
Klopp amefanya makubwa, lawama anazoshushiwa ni kutokana na alikuwa na uwezo wa kufanya zaidi ya hapo ila kiburi na ubishi kimefanya asifikie huko.
YNWA