Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Wala pensheni FC

Jumapili mna kibarua, huyu jamaa ataendelea alipoishia
20230120_204218.jpg
 
Hilo Jina nimelikuta kule jukwaa la Chelsii wanamwita🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Siyo mimi kabisaa


Leo ntakua nacheck marudio ya mechi huku nasoma comments za wadau darajani huko
Wana matusi kama yote 🤣
Jana wametukana timu yao hadi basi
Hakuna kocha pale aliejua kumtumia vyema Kai yaaani mara MF mara false 9 dogo ana siku zake lakini na yeye ni Timo Werner mwingine hana jipya... Wasubiri preseason na msimu mpya kama watampata Enrique wataeleweka.

Tetesi Enrique yupo London kusaini mapema tu ili awashughulikie Real Madrid...

YNWA
 
Hv kwann Klopp anakomaa na usajili wa mount?
Klopp anaishi kwa kukariri ndugu huyu mzee anachokiamini yeye anataka na wengine waamini hivyo hivyo bila kuuliza hapa niaje...

Eileweke mapema huyu dogo akitua Liverpool mshahara wake utakua sio pungufu ya £280k hukoo kwa wiki sasa unajiuliza huyu dogo anastahili huo mpunga...

Kama lazima awe ni mjukuu wa malkia kutua Liverpool wapo wachezaji wazuri tu kama Bowen, Gallagher, Rice nk ambao

Muda utasema yetu macho.

YNWA
 
Hivi alikuwa anamfokea Allison kwa kosa gani? Sijamuelewa huyu muingereza aisee....
Ile ni PR show hana lolote... Aliesema mpira unachezwa kwa kukalipiana ni nani jamani... Tunahitaji tuone Kapteni akitutoa kwenye hili tope sio zile bla bla zake za camera hatuhitaji zile drama kwa sasa.

Bila Allison msimu huu tungekua alipo Everton lipo wazi aafu anatokea Kapteni wa mchongo anaanza kum diss... Sisemi Allison ni immune kukosolewa la hasha lakini ifike mahala Henderson ajue nafasi yake ya kutoa lile domo lake kusaka sympathy from kops wala haipati alikua wapi tangu tunaanza kupoteana.

Ilikua ishu ndogo tu kwamba Allison hakumstua mapema Matip aliepiga mpira wa kichwa ukatua kwa Felix ambae hata hivyo hakufunga... Sasa pale Henderson akaamzukia Allison kwamba hajafanya majukumu yake ipasavyo... Baada ya mechi Le Kapteni kwa kucheza na camera huyooo akatua kwa Allison wakiongozana kutoka uwanjani... Henderson hua ana tafuta salama huruma kwa mashabiki kwamba aonekana yeye ndio ananya kinachoeleweka...

YNWA
 
Developing gossip.

Bye bye Nunes wa Wolverhampton tetesi ni kwamba kile kipengele kinachomruhusu kujiunga Liverpool kwa ada chini ya £60m tayari kimeshatolewa na hakipo tena.

Hii ni taarifa mbaya kwetu kama kweli Liverpool walionyesha nia unless wawe wameshajitoa kumnunua huyu dogo kwa kuwasiliana na wakala wake.

Ina maana mpaka sasa hatuna Bellingham na hatuna Nunes.

YNWA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom