Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Naona hutaki stress Miss Liverpool ni mapicha tuuu...

Liverpool timu wachezaji pekee wanaoweza kuja kuturudisha makali ni wale wasiojengewe ubora na magazeti ya Malkia kiasi utadhani wenyewe wana hisa mle tangu Jack Grealish anunuliwe £100m ki ukweli nilitoa macho kama fundi saa yaaani Grealish huyu huyu ama mwingine hatujakaa sawa wakatua BvB Manchester United kumng'oa Sancho kwa £70m hapo ndio nikachoka kabisaaaa.... Wachezaji wengi wa Uingereza ni overrated na Liverpool chini ya FSG hawana huo uwezo hata kidogo kwamba wanunue Jude, Jaoa, Kone na beki mmoja bila Liverpool kuuza hata mchezaji mmoja hio itakua ndoto ya mchana kabisaaaa.

YNWA
 
Sijui kwanini klopp anataka kumuweka Caoimhin Kelleher sokoni wakati hii ni backup ya Allison na anatakiwa ampe game time.
Simple dogo ame out grow position ya kua back up goal keeper ni wakati anapambana kwingine akiwa chaguo la kwanza.. Namna ya kufanya hapa ni klabu waweke sell back clause wakimhitaji endapo atakua sokoni.

Sababu nyingine ya kuuzwa ni kwa sababu hawa ma dogo Marcelo Pitaluga na Davies watakua wamemshawishi Klopp kwamba wapo tayali kua nambari 2 kumsaidia Allison.

Kingine mkataba wa Alison unaisha hukoo 2026/27 na dogo mpaka sasa anacheza kiwango cha juu sana haonyeshi kushuka hata chembe hivyo Kelleher mapema asepe.

Kingine Kelleher ni chaguo la kwanza timu ya Taifa ya Ireland na kama ujavyo timu ya Taifa inahitaji mchezaji anaecheza mara kwa mara ili kua bora hivyo itakua kocha wake wa timu ya Taifa amemshauri ni wakati sahihi achukue hatua muhimu kusaka timu ya kucheza mara kwa mara akiwa chaguo la kwanza.

Na mwisho akiwa chaguo la kwanza kuna ma bonus ya ku mwaga kama vile clean sheet, kombe, nk hivyo hata kipato kitaongezeka

YNWA
 
Dogo akwende tu
Timu yetu ni kubwa kuliko mtu yeyote.


Tupate ugali kidogo.
Mbeya hatuna hiyana,tunemkirimu bro Ramsdale Ugali.
 
Hivi kwanini huyu mtoto hawepi Airtime jamani?
Alitupa ushindi fainali dhidi ya wale maporomokoni darajani.

Kuna mechi kunafeli,hadi huwa nawaza pengine angedaka dogo tungeshinda.
 
Huyu anayekufundisha hizi lugha aisee😂🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Dah!😂😂😂😂😂
Bado kidogo utaanza kwenda vibanda umiza🤣🤣
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Vibada umiza wanajazana mashabiki wa Manjesta, Arsenal, Chelsea aafu sasa wengi wao ni full ku bet na kuwapa Liverpool ushindi itokee sasa tumechapwa wanavyonuna sasa yaaani utadhani wao ndio Liverpool aafu sie wao 🤣🤣🤣

YNWA
 
Hivi kwanini huyu mtoto hawepi Airtime jamani?
Alitupa ushindi fainali dhidi ya wale maporomokoni darajani.

Kuna mechi kunafeli,hadi huwa nawaza pengine angedaka dogo tungeshinda.
Allison is way toooo good kwa huyu dogo hata Allison akiingia uwanjani amekunywa mbege glasi 3 hivi bado atakua bora tu.

Kelleher ana kipaji lakini levo za Allison bado sana.

YNWA
 

Huyu ndio Le Kapteni mtarajiwa Liverpool baada ya kizazi cha wale wa over 28 years wakishasepa.

YNWA
 
Cheka uongeze siku ili tukianza kurudisha makali yetu msimu ujao uwe na afya njema kushangalia.

Pedro Goncalves aliefunga lile goli ni full loaded na kipaji na huyu ni EPL bound

YNWA
Kumbe ndio huyo?
Nilikuwa hata sijui😂mie nimeona goli tu.

Msimu ujao aisee nitanyanyasa sana wanaotunyanyasa sasahivi.
 
Kumbe ndio huyo?
Nilikuwa hata sijui😂mie nimeona goli tu.

Msimu ujao aisee nitanyanyasa sana wanaotunyanyasa sasahivi.
🤣🤣🤣🤣Aaaaa msimu huu hatuna raha maana ushindi na vipigo havituachi kabisa unakamata pop corn mechi ya Nottingham au Bournemouth ukiamini kadada safi na pointi safi unajikuta unanuna hata kabla ya mechi kuisha kwa kuangalia tunavyohenyeshwa...

Msimu huu uishe tu kwa kweli tu sahau yote lakini sio ule ushindi wa 7 juu aaaa that sooo sweet to be forgotten 🤣🤣🤣

YNWA
 
Bora Jacky Grealish unaona kabisa alikuwa na ubora na takwimu nzuri Tena kaonesha akiwa epl kwa kikosi Cha kawaida na alikuwa ni main man wa Aston villa binafsi na tatizo na Grealish kabisa hata sifa alizokuwa anapewa alistahili labda zinatofautiana kwenye kiwango Cha basi Lakini as individual player Grealish ni mtu na nusu ana. Uwezo wa kutengeneza nafasi nyingi, mzuri kwenye dribbling pia ana uwezo wa kuchezesha team but kwa huyo Jude bellingham ni utumbo kabisa sio mbunifu, sio mkabaji mzuri, sio good scoring hana hata kitu kinachombeba inakuwaje thamani yake iwe paund million 100? Na kilichonikera zaidi wachambuzi wa kiingereza wakawa wanamlinganisha na Enzo Hernandez serious?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…