Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Nyie Majogoo
vipi Hali uko?
IMG_20220817_183106.jpg
 
Naona m azidi kumalizana na Westham , niliwaambia kuwa sisi na nyie tupo jahazi moja tukizama na nyie mnazama na mkijitahidi saaana ni draw.
 
Nyie matakataka mkuje muone mpira wa kibingwa unavyochezwa angalau mpoze machungu
 
Mkuu Nunez ni poacher sio winga kama Mane hua actually anacheza lone striker kwa mafanikio, sasa tazama kwa Klopp leo alikua anacheza pembeni upande wa Diaz yaaani yeye mfungaji ndio anakua mtengenezaji... Sio rahisi... Mpaka pale Klopp atacheza mfumo unambeba Nunez ndio utaona uzuri wake. Lakini ukitazama ni kama bado main threat yetu ni Salah kwa namna ya upangaji wa mfumo... Lets Klopp adapt 4 2 3 1 huku Nunez akiwa lead striker utaona matokeo mazuri.

Kimsingi tatizo letu letu lipo pale pale kila mechi tunaanza tumepoza sana yaaani hakuna mpango madhubuti ya kusaka goli yaaani tupo tupo tu. Inafahamika vyema sasa 4 3 3 imeshajuliwa na timu pinzani ni muda mwafaka sasa tuodokane na huu mfumo kuleta ubora wa main target Nunez.

YNWA

Mkuu tukipoteza point kila mtu anasema lake tukishinda hawasemi chochote.

Kwa upande wangu nilichokiona elliot ndio tatizo au kwa maana nyingine Thiago anaweza kuchezesha timu vizuri tukiwa tunaenda kushambulia huyo elliot bado aisee.

Mipira mingi akipoteza huyo watu wa mbele hawata onekana tutaanza kuwa laumu wakina Nunez lakini Nunez yuko vizuri tu.
 
Hawa Waingereza ndugu yangu ni kuwaogopa sana. Umeona Klopp leo anatoa main creator wake Trent anaingiza Babu Millie... Form is temporary class is permanent hivyo japo Trent ana struggle kutengeneza klosi za nguvu lakini dogo bado ndio mchezaji hatari kwetu kwa kutupia klosi kali... Kumtoa na kuleta Milner najiuliza sana Klopp alitaka sare ama amevurugwa aisee...

Hili la Edwards sidhani kama angepata huyo MF kwanza Klopp kaamua hata huyo Melo baada ya jeraha la Henderson tofauti na hapo asingenunua kabisa.. Too much pride kwamba he can't swallow his words ni hatari sanaaa kua na mwalimu wa hivi...
Ki ukweli ndugu yangu naona kama Klopp ameshafika mwisho wa mawazo yake na msimu huu ajitadhimini sana hatuwezi kua wasidikizaji wa Pep kila msimu kwa kusema ooh oil money wakati wachezaji wao wamenunua kwa bei chee tu huku sisi tukiaminishwa eti tusubiri Bellingham 2023 June huku Klopp akijua fika hii MF yake inahitaji kufumuliwa yote na sio mchezaji mmoja tu...

Anakomaa na wagonjwa kwani analasimishwa au anataka mwenyewe. Tangu nisikie Kieta anaongozwa mkataba niliishiwa pozi..

Leo sijui atazingizi kipi maana kwa sasa hakosagi lawama.

YNWA
Umeongea/umeandika kwa uchungu sana kop...lakini sidhan kama wao (kocha na wachezaji) wanaumia kama sisi mashabiki tunavoumia....

Haihitaji kuwa na degree kuelewa kuwa kikosi chetu kina madhaifu ya kutosha....lakini ndo hivo tena, kocha kiburi kimemjaa....

Acha tusononeke tu...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom