Ni kweli Liverpool wamepoteza mshambuliaji Sadio Mane ambae aliweza kufunga magoli 23 msimu uliopita, lakini Fabinho anatarajia wengine kuchukua nafasi kutoa mchango wao baada ya kuondoka kwake.
Fabinho amewataka Darwin Nunez na Luis Diaz kuongeza kasi ingawa alikiri kwamba mshambuliaji huyo wa Uruguay anaweza kuhitaji muda kuzoea Ligi ya Uingereza.
Liverpool walikosa nafasi ya kushinda makombe Manne, lakini lakini walishinda vikombe viwili vya ndani FA Cup na Carabao pia wakamaliza nafasi ya pili kwenye Ligi ya Uingereza na Ligi ya Mabingwa huku Mane akifunga mabao 23 katika michuano yote.
Msimu huu tumeshuhudia Jurgen Klopp akirekebisha safu yake ya ushambuliaji baada ya Mane kuondoka kwenda Bayern Munich, na kumsajili Nunez kutoka Benfica katika dili ambalo linaweza kugharimu hadi pauni milioni 85 (€100.5m), huku Diaz akiwa na matokeo chanya baada ya kujiunga na Porto mwezi Januari.
Ingawa Fabinho alikiri kuuzwa kwa Mane ni "hasara kubwa" kwa Liverpool, bado anasalia na imani kwamba safu mpya ya ushambuliaji ya Liverpool itawaweka katika kinyang'anyiro cha kupata mafanikio makubwa msimu ujao.
"Darwin anaweza kuhitaji muda kidogo kuzoea, ngoja tuone, lakini mchezaji kama yeye anaweza kubadilisha timu," Fabinho aliambia Athletic.
"Yeye ni nambari tisa halisi. Ni mfungaji mabao. Alifunga katika mechi zote mbili dhidi yetu kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya. Tunajua jinsi alivyo mzuri. "Ingawa tulimpoteza Sadio, bado naamini tunaweza kupigania kila kitu. Timu bado iko imara."
@thisisanfield @liverpoolfc_africa_swahili
LiverpoolFC @lfcynwanews @fabinho