SALAMU KWENU NYOTE HUMU
WAKUU naombeni kuuliza na mawazo yenu kidogo juu ya hili
Suala la Mane dhidi ya Cape Varde je tukio lile linafanana na lile la kwanza alilolifanya dhidi ya Man city?
Kuna mashabiki wametoa lugha chafu leo
Nani alikuwa na kosa kati ya mane na yule golikipa wa Cape Varde?
Samahanini Sana
Nawasilisha
Ujue hivi kuna foul zinaangalia
1. Nia ya wachezaji wote wawili,
2. Uwezo wa aliyechezewa foul kuufikia mpira na kuumiliki na mchezaji foul kuucheza ama kuumiliki mpira au kuuondoka kwenye umiliki wa aliyepigiwa au mwenye nao.
Nitoe mfano huu mechi ya Liverpool vs spurs hii ilikubalika 99.9% Kane alitakiwa kuoneshwa kadi nyekundu, kwa nini Hakua na uwezo wowote wa kuumiliki mpira au kuuondosha namna alivyoserereka niahaikua njema.
Sasa kwa foul ya Mane jana ile ni kadi nyekundu halali
1. Kipa hakua na uwezo wa kuumiliki ule mpira.
2. Kipa hakua na nia sawia zaidi ya kumzuia Mane asifunge kwa kumcheza yeye badala ya mpira. Kama Mane angeupata ule mpira angekua na 90% ya kufunga kuliko kukosa.
3. Wakati mpira umepigwa, Mane hakua anaangalia golikipa zaidi ya mpira ila kipa lengo lilikua kumzuia Mane kuliko mpira.
CASE YA PILI
Mane vs Ederson
Ile scenario labda tuchukulie high boot ishu ila Mane hakua na lengo la kumcheza kipa wakati mpira upo kwenye movement alikua amelipa goli la city mgongo wakati mpira umepigwa alianza safari ya kukimbia kwa kuutazama mpira na sio golikipa, kipa alimuona Mane akija hivyo akarisk kuweka kichwa bahati nzuri au mbaya mguu ukatua shingoni. Ederson alikua nje ya 18 sijui kisheria imekaaje lakini Mane hakustahili kadi nyekundu kwa kutizama nia yake na macho yake yalikua wapi?? Hii ni kwa mujibu wa wachambuzi na mahojiano na marefari wa zamani.
Matukio kama haya yapo na yamechambuliwa sana. Kwa maelezo haya katizame video zote mbili soma body language utaelewa mkuu.
Kuna vitu vingine kimaamuzi hua ni ngumu sana sana kwa scenario hizi mbili
USIWALAZIMISHE KUAMINI, KUAMINI NO CHAGUO.