Sijui mpira kihivyo Ila sidhan kama minamino ni bora kuliko Henderson
Sent using
Jamii Forums mobile app
Henderson wanasema na leader of men, vocal, real professional maana hua hasikilizi maneno mbal anatekeleza majukumu yake ndani na nje ya uwanja..
Minamino ni dynamic flexible kind of player anacheza kati na pale mbele.
Ni ngumu kumlinganisha ubora wake na Henderson kwa vile mpaka sasa Klopp hajampa gemu za kutosha na hii inatokana kwamba kwa sasa anapambana na hawabFirmino, Jota, Origi kupata namba pale mbele hivyo amejikuta muda mwingi anacheza aidha FA ama Carabao.
Minamino na Elliott ni wachezaji fulani vilaka kokote kambi.
Nilisema acheze kati ni kwa sababu kabla ya leo waliokua wamecheza tuliambulia kipigo na sare hivyo wakati mwingine ni muhimu kubadilia askari vitani waje na mbinu mpya kama waliopo wanakwama.
Leo Brentford shot on target wameipata dakika ya 90+, hii imetokana na tulishinda mipira ya pili almost yote yaani hata tuki misplace pass basi wachezaji wetu walikua aggressive kuhakikisha wanawapokonya Brentford mpira na kuanza move... Hii ni tofauti kabisa akiwepo Milner kwa vile miguu inataka mwili unagoma. Jones leo anamiliki, ni msumbufu haswa ana miguu ya kukimbia, ana hold mpira nk..
Leo Oox,Firmino na Jota walishuka huku chini kusaka mpira na huu ndio mpira wa Liverpool ninaojua mimi. Tukicheza hivi hakika ushindi upo.
Hua nasema narudia tena Liverpool tukicheza kama Unit basi ule uzembe ambao umesababisha kupoteza pointi 10 msimu huu wala huuoni...
Tupo unstoppable pale kila mchezaji anaelewa na kutekeleza majukumu yake na leo bila hata kucheza in full throttle tumetoka salama na pointi 3 murwa sana. Leo pasi nyingi tumepoteza na kipa upande wa Brentford kakomaa sana kutuzima.
Clean sheet ya kumi amekuja wakati mwafaka. Tulihitaji upya tupate utamu wa ushindi mzee baba maana wanasema winning is addictive hivyo tutarajie mazuri kuanzia kwenda mbele..
YNWA