Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Duu Minamino.....

Dakika nne awe cult hero...

PPanic sub by Klopp

YNWA

Nilichokiona mkuu hatuna Mido za maana Aisee ushindi wetu unategemea mida kacheza nani.

Kama leo Mido zetu ni Henderson tu ndio alikuwa anakaa mipira hao wengine wanasubiria wapewe mipira tu waipoteze.
 
Mwaka Juzi tulipoteza mchezo mmoja tu lakini Ubingwa akabeba Man City.

Kilichotuathiri ni Draw ndugu
kwa beki hii hakuna ubingwa hapa, mechi vs bretford tuliongoza 3 zikarudi zote point 2 droped, vs City tulitupia 2 zikarudi , 2points droped, leo tena 2 zimerudi 2points droped jumla point 6 ambazo tulikua kwenye nafasi ya kuzibeba, timu haijui kukaba hii kabisa inawapa wapinzani mianya mingi sana ya kufunga ni wao tuu kukosa
 
Mwisho wa Msimu tutaweka Kikao cha dharura hapa kujadili mechi hii ya leo na ile ya Brentford.

Ni mechi tulizopoteza points kwa uzembe kabisa
Kuna mianya mingi sana pale MF na pale nyuma sijui wanategeana ama niaje...

Klopp sijui hua haelewi kwamba hivi vitimu hua havina vya kupoteza vyenyewe vinapambana kubaki Ligi Kuu period hivyo lazima kua na plan A na B na ajabu sasa hawa Brighton mpaka sasa mfumo wao kwetu ni ule ule sasa unajiuliza huko mazoezini wiki hii Klopp alikua anafanya drill zipi kwa hii gemu..

Wenzetu wamefanya home work yao vizuri ndio maana hakuna kilichowasumbua walijua fika hata tukitangulia hakuna ku panic watakuja mazima na kweli wametoka na pointi muhimu kwao..

YNWA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom