Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mimi naona kama wote wawili wanashinda.

Halafu kuna level fulani ya imani nimeshaipoteza juu yetu, kwamba hata yeyote au wote wasipopata matokeo, bado sisi hatupati matokeo mazuri.

Sasa hivi ni kama tu naombea top 4.

Considering Manchester Clubs form and also our form we are competing for top four

If some things get done to get our team back to winning ways and banging goals again may be we may be not late but that should be earlier and not later
 
Kuna makocha shida yao si usajili bali Walihitaji muda zaidi wa kujifunza kuliko kubeba majukumu waliyonayo.

Mfano Lampard:
Msimu uliopita Mashabiki wa Chelsea walilalamika kuwa wanafanya vibaya sababu wamefungiwa usajili! Tukawaambia sababu sio usajili bali uwezo wa kocha ni mdogo basi hawakuamini.
Hatimae Timu ilimaliza Ligi ndani ya Top Four.

Msimu huu wametumia takribani £220M kwenye usajili lakini ndiyo wamekuwa wabovu zaidi kuliko msimu uliopita, Lampard analalamika wachezaji Wavivu but nani responsible na uvivu wa Wachezaji? Jibu ni Kocha mwenyewe.
Kashindwa kuwatumia Harvertz na Werner, pia Joginho aliyeonekana ndiye Muhimili ambao Sarri alikusudia kutengeneza Timu kumzunguka yeye basi Lampard amemuua kiwango kwa 100%.

Lakini kwa Liverpool hali ni Tofauti, Sera ya Matajiri wetu ni Sell to buy!
Hivyo tunaweza kukaa na useless Player kwa muda mrefu na hatutoweza kununua mwengine mpaka tumuuze huyu useless player.
Na ndiyomana ni Vigumu kwa sasa kusajili CB na Mido mpaka tuondoshe Matip na Nat Phillips pale kwenye Backline yetu, na ni vigumu kusajili Mido mpaka tuondoshe Gini au OX au Keita while Milner his time inahesabika.
 
Ingawa MosDef mara nyingi anaelezea hapa kuwa sababu ya kutokufunga magoli ni kuumia kwa VVD na GOMEZ but kwahili sijakubaliana na mtazamo wake, mimi mtazamo wangu hatufungi magoli kwasababu kuu mbili.



YA KWANZA:
Kushuka viwango kwa mabeki wetu wa Pembeni (TAA na ROBBO), au Makocha wameshawajua uchezaji wao sasa wanawadhibiti! Hii imepelekea Timu yetu kukosa ubunifu wa kutengeneza nafasi za kufunga kwani ndiyo mbinu pekee kwa misimu Mitatu sasa ndiyo tunayoitumia baada ya kuondoka Coutinho.

YA PILI:
Kushuka kiwango kwa Front 3 yetu! Huu ni ukweli usiofichika kuwa Front 3 yetu siyo ile tuliyoizoea, haiwezekani mchezaji kama Sadio Mane akabwe na Boya kama Wan Bissaka asifurukute halafu tulaumu kuumia kwa VVD how?
Bobby kashuka Kiwango lakini at least akili ya mpira bado anayo, Salah yeye kashuka kiwango lakini na hata ile akili ya mpira pia hana hata moja.
Mane kashuka kiwango na akili ya mpira pia inaanza kupotea huenda akawa kama Salah.
Mbona Jota alikuwa anafunga bila ya VVD?
Mbona zamani Bobby na Mane walikuwa wanafunga bila ya VVD wakati nyuma kuna Lovren na Skirtel?
Hii Front 3 yetu tukubali tu kuwa kwasasa haimtishi Mtu.

Kuhusu Mido siiongelei kwani haijawahi kutusaidia kwenye kufunga.
 
Kila nikiangalia aina ya Timu kama Fulham na West Bromwich zinavyonyanyaswa wakati zilitukazia sisi basi huwa napata mashaka sana.
 
Nakumbuka kipindi cha msimu uliyopita wakati tunalalamikia usajili na tunaletewa Vitoto huku tukidanganywa future Plan haikujulikana kama tulishaona kuwa yatatokea haya tunayoyashuhudia sasa! Baadhi ya Comments za washabiki wenzetu hapa zilikuwa ni hizi:-

  • Do not disturb Midfielders yetu
  • Do not disturb Front 3 yetu

Sasa kutokudisturb kwetu ndiyo tunashuhudia sasahivi Timu nzima imechoka kwa wakati mmoja.
 
Leo nikiri tu kuwa mimi ni Mmoja wa Wahanga niliyefanikiwa kuaminishwa na Klopp kuwa hizi Mickey Mouse Cups hana mpango nazo!
Nasikitika sana kuwa Klopp alifanikiwa kunidanganya kwa hili kama alivyowadanganya Washabiki wengine wa Liverpool.

Kwakweli Klopp ametufanganya na kutuaminisha kuwa hana mpango na Mickey Mouse Cups.

Ukweli usiofichika ni kwamba Klopp anazitaka sana hizi Mickey Mouse Cups lakini sababu kubwa ya kuzipoteza ni kwamba hana Depth ya kutosha kushiriki mashindano yote, ili aweze hivyo ni lazima awe na kikosi B jambo ambalo kwake yeye kikosi B ni U23.

Hivyo aliamua sacrifice Makombe yote ili abaki na EPL na CL kwani kikosi chake kisingehimili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom