Nimehisi naweza kushare hii kitu.
Wakati tulipokuwa na Coutinho/Milner/Gini/Hendo nilikuwa mkosoaji Mkubwa wa Hendo kutokana na uchezaji wake mbovu wa wakati huo! Lakini from the last season mpaka sasahivi simkosoi tena Hendo na nimeridhika aanze kila Game, unadhani namkubali ni bonge la mchezaji? Hapana! Bali ni kuwa yupo Fiti wengine ni Wagonjwa wazoefu.
Lakini ukiangalia huu Uzi (Hasa baada ya Matokeo haya) utagundua haya.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Gini tu haku akisia wengine.
- Kuna Washabikia kazi yao kumponda Firmino tu haku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Salah tu huku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Jones tu huku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Hendo tu huku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda Keita (Hakucheza) huku akisifia wengine.
- Kuna Washabiki kazi yao kumponda OX tu akisifia wengine.
Sasa hapo angalia hizo tabia za Mashabiki wetu wa Liverpool utagundua Wachezaji wote wanapondwa ambapo kila Mtu anamponda mmoja au wawili kati ya hao.
Na vilevile wote hao Kila mmoja hapo utakuta kuna Mtu humu anamsifia mchezaji husika hivyo wote hao pia wanasifiwa.
Ukija kwa wapondaji hapo siku zote hawamlaumu mchezaji kulingana na takwimu kwani hawaamini katika takwimu kitu ambacho huwezi kuwa mchambuzi au muelewa wa mpira bila ya kuwajadili kulingana na Takwimu.
Unapokuwa Beki basi msingi wa kupimwa kwako ni takwimu za duels won, tackle won and intercept.
Unapokuwa Mshambuliaji basi msingi wako mkubwa wa Takwimu utapimwa kwa Goal score + Assist. Mshambuliaji hawezi kupimwa kwa kupiga chenga na kukimbiza mipira, kama ni hivyo tungelimnunua Adama Traore badala ya Diogo Jota.
Hivyo huwezi kusema mchezaji fulani hata asipofunga anahangaika uwanjani!!! Yeye ni mshambuliaji hii kuhangaika tunaipimaje? Ni Stats? Ni lazima afunge wakati yeye ni Mshambuliaji.
Na hii ndiyo inayomfanya Salah ataendelea kupata namba game after game labda awe majeruhi. Hii ni kwasababu Takwimu zake za Ufungaji na Assist zinajieleza. Kamwe Klopp hawezi kumuweka Benchi Salah kutokana na anachokifanya kwani points hazipatikani kwasababu fulani kahangaika bali zinapatikana kwasababu Fulani kafunga.
SULUHISHO:
Wanaowashambulia wachezaji wanashindwa kuleta Facts (Takwimu) za weakness zao bali wanaishia kulalamika tu hii inaonesha wazi kuwa hawajui wanalalamikia kitu gani bali ni Haters tu kwa baadhi ya Wachezaji zilizotokana na Makala za Mitandao wanayotembelea.
Jones, Salah na Gini hawastahili lawama wanazopewa kwa Matokeo ya Jana.