So far hatuna beki stable mpaka VVD atakaporudi.Hata tukifanya usajili wa beki January bado nae atakuwa anahitaji muda kwenda na intensity ya epl.Hata beki mwenye profile kama Silva alistrugle kwanza mwanzoni.Hakuna mtu reliable wa kupartner na fabinho.Huyo Williams ambae ni Klopp favourite hawezi kudefend,bado anahitaji muda na gem zake zilitakiwa kuwa FA na carabao huko ajenge kwanza uzoefu.Ilikuwa tupigwe goli la pili jana bila Becker kufika na kumsaidia dogo Williams,alishapoteana.Simrate huyu dogo kifupi.
At least huwa namwelewa Nat Phil lakini bahati mbaya Klopp kamweka nyuma ya Williams!!Kwahiyo kwa msimu huu wote tutastruggle Sana na hii backline.Ni Kwasababu hiyo siiweki Liverpool kwenye ubingwa msimu huu.Ushakuwa ngumu aisee.Tutafute mtu established wa kuja kupartner na VVD msimu ujao.Hata huyo Gomes nae kabla ya kuumia alikuwa uchochoro tu.Ni aina ya beki ambae muda wote anakucost.
Bado kule mbele kuna tatizo ambalo linakua siku hadi siku.Ukiondoa Firmino,waliobaki wanagombania kufunga.Hawachezi kwa ushirikiano,Kila mmoja anataka kufunga yeye.Kuna muda dakika za mwisho jana Salah anaopt kudribble akiingia kwenye box bila kujali mbele yake kuna mabeki na wakaichukua kirahisi tu,nafasi ikawa wasted kirahisi pia.Alikuwa anaweza kufanya kitu kingine kujenga shambulio la uhakika zaidi.
Midfield na mabeki wetu wa pembeni(chance creators) ambacho walikuwa wanakifanya mostly ni kupiga tu mikrosi ya curving ambayo kwa asilimia kubwa huwa ni mipira ya kipa.Wakaendelea hivyohivyo hata baada ya kugundua hazina mafanikio.Watu wakishaweka msitu na wewe ukaendekea kutuma curves huwezi kufunga ukizingatia wachezaji wazuri kwenye vichwa(VVD,matip) hawapo uwanjani!Bado kufanya mashambulizi kupitia katikati pale pembeni kunapokuwa kugumu ni changamoto nzito.Wachezaji wazuri kwenye role hiyo ni marafiki wakubwa wa injuries!