Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Adjustments.jpg
 
Mkuu kwanini unaihofia sana Man utd?hahaha au chuki tu

Hapa hatuongei kwasababu ya hofu Mkuu, Mtu kama Mimi naiombea mabaya Manure kwasababu ya Chuki tu za waziwazi! Yani kila nikiona wanapata shida basi ndiyo Mimi kwangu ni furaha kubwa.
 
Haya bhana! Heshima kwako bingwa wa FA mara nyingi kuliko Timu yoyote ile.

Fanya sasa utinge Fainali uwaziuie Manure au Chelsea wamalize msimu bilabila ili nije nikurarue kwenye Ngao.
Unaniraruaje wakati nishakurarua tayari
 
Soma vizuri nilichoandika, Point sio kutoka Midtable team! Point ni kuwa mchezaji mwenyewe ni wa Midtable.

VVD alikuwa Midtable lakini hakuwa Mchezaji wa Midtable.
Karius yupo Top Team (Liverpool), lakini ni mchezaji wa Midtable.

Nadhani nimesaidia.
Kwani kukana maneno yako shilingi ngapi? 😂
 

Attachments

  • Screenshot_20200719-200015.jpg
    Screenshot_20200719-200015.jpg
    67.1 KB · Views: 5
Kwani kukana maneno yako shilingi ngapi? 😂

Sijakana maneno yangu bali nimefanya Clarification kwenye maneno yangu.

Nilisema ni wachezaji wa Midtable teams sikumaanisha kuwa wanatoka Midtable teams, bali wao uwezo wao ni wa Midtable teams.
 
Unaniraruaje wakati nishakurarua tayari

Sasa umegeuka Utopolo naona! Utopolo walitembea na goli lao 1 mfukoni mpaka ikawa balaa unapowakuta wanakutajia goli 1 la tarehe 8 hatimae wakaumbuka kwa migoli 4.

Sasa na wewe naona unatembea na goli zako ulizowafunga Man City na Liverpool huku ukisahau yote waliyokusababishia kwa miaka ipatayo mitano.

Haya tembea na magoli yako mfukoni mpaka siku yatakayokukuta kama Utopolo.
 
Problem kubwa ya Rodgers ni defensive schemes, muda anaotakiwa kucheza defense hachezi.

Hata alipokuwa kwetu, ule ubingwa tuliukosa kwa sababu hatukutaka kudefend hata kidogo.

Mimi nina tabia ya kukariri tabia na uwezo wa Mtu katika kufanya jambo.

Tokea msimu wa 2013/14 Rodgers alipotukosesha Kombe kijinga kwenye vs Chelsea ambayo hakuwa na chakupoteza basi nimeamini kuwa kamwe hawezi kuipatia Timu yoyote mafanikio unless spate Timu kama Celtic iliyokuwa haihitaji ubora wa kocha kushinda Ligi bali nguvu yake ya kiuchumi tu ukilinganisha na Timu nyengine ndiyo inampa mafanikio.

Hata mwanzo mwa huu msimu ambapo baadhi ya Washabiki walijiaminisha kuwa Leicester ni title contender basi nilipinga na kusema mwisho wa msimu Rodgers atagombania Top Four.

Rodgers Timu aliyonayo haina uwezo wa kushindana na Timu za Top Four kwahiyo anapoingia uwanjani kupambana nao anapaswa awe na Plan B ya defensive minded lakini yeye akili hizo hana.
 
huyu brendan wamarekani walikua na haki kumtimua, kocha gani unapohitaji ushindi unapigwa kizembe vile?


manure kwenda cl itaniuma sana,....... na inavoelekea wataenda hawa!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom