Captain Marvelous
JF-Expert Member
- Jul 25, 2017
- 15,313
- 32,605
Kabisa ndugu hili janga linatisha kwa kasi hii upo uwezekano Euro 2020 kutofanyika ama hata EPL kutomalizika kwa wakati hii yote ni kuepesha vifo na maambukizi zaidi...Point nzuri sana kwa hii post ya kiuungwana uhai wa mtu ni muhimu toka moyoni nawaombea liverpool mchukue ubingwa tu
Mpaka sasa Arsenal, Chelsea, Manchester City, Leicester huu ugonjwa umewagusa, hivyo ni muda tu utasikia na kwingine... We forbid kwa kweli..
Hiki kirusi hakichagui maskini wala tajiri, Leo hii mke wa Waziri Mkuu Wa Canada amegundulika ni mgonjwa na upo uwezekano alipata virusi hivyo akiwa Uingereza wiki iliyopita.. Hayo na mengine ya natoa picha namna ya hatari tuedako,..
Hispania, USA, Italia wamesimamisha shughuli zote za kimchezo kwa sasa.
Waziri Mkuu Boris anasema bado Uingereza haijapata maambukizi ya kuwa fanya EPL isimame, hivyo sasa wanaongeza juhudi kwenye ku contain corona kuenea zaidi..
Otherwise hongera kwa ushindi mnono wa jana aisee...
YNWA

