Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Kwa nilichokiona mimi vs Naples

Wanatufunga kwasababu Plan yao ya kwanza ni Kidhibiti Midfield (Due to our incompetent Midfield) kuhakikisha Kati wanatawala wao ili waweze kuwa na 3 alternatives za kufanya Mashambulizi.
Kutokana na kudhibiti Mido yote basi Mido zao wanaweza kuanzisha mashambulizi upande wa kulia, au upande wa kushoto, au kupitia kati moja kwa moja.

Pia sababu nyengine ya kutufunga ni kwamba kila game wanakuwa na game plan ya kumshut down completely TAA kwani wanajua ndiye threat kwa mpinzani! So, leo wamefanikiwa tena kumzima kama last season asiweze kupanda juu na kitengeneza nafasi.

Pia jambo jengine ni kwamba leo Bobby hakuwa katika ubora wake na huku Koulibaly alikuwa anakwenda na Salah toe to toe pale anapokaribia kwenye 18..
Kutokana na kutokuwa vizuri kwa Bobby pamoja na kukabwa kwa Salah, basi na Mane akawa anapotea kirahisi.
well said...pale kati walipakamata vyema...

they knew when to tackle, kujazana kati, when to press, when to sprint, and in the same time aware of our counter balls., bila Fabby being at his best we were doomd

Bobby ws underperfoming and when he does we rarely win....

TAA pinned at his own half and aware of Insigne he couldnt attack...


Carlos game plan worked so so well...thrice he has got an upper hand now its tym for Klopp to come up wt counter measure...



we got our chances bt we werent clinical enough..
 
Tulipiga kelele kwenye usajili kuna watu wakatushambulia kuwa eti tuna kikosi kipana cha kina Brewster.

Tukawambia ukitoa kikosi cha kwanza ni mchezaji gani anaweza kuingia sub akabadili matokeo? Wakatuambia yupo Origi, Lallana na Brewster.
Lallana vs Naples unless Klopp awe amepiga Budwiser...

huo ndio ukweli, when our LB and RB are pinned to our own half we turn to Firmino to bring some magic pass sasa leo hata mipira kukaa mguuni ilikua ishu kwake...

we need a real last pass wizard kwa occasion kama leo...

TAA and Robbo closses were poor today, the corners msimu hui bado hataji click...

Defending Corner we were SUPERB and very amazed...

well leo ndio mwanzo tujipange kwa yajayo
 
Ok mi naona kama hizo Plan B na C unazosema tungeanza na mbele kwanza ..mpira ni magoli nafasi zimetengenezwa tumeshindwa kutumia ...angekwepo striker(s) lenye uwezo wa kuscore kama yakina lewandoski ...etc ndo ingekuwa plan B na C ya leo ...pale mbele napo hatukuwa makini..(mtazamo)
Mkuu Klopp alisema hakuna mchezaji anaetaka kuja kusugua benchi hivyo kumpata Strika level ya Lewandoski lazima moja wapo wa hao ma front three ale kona mazima...

Napoli are damn compact and stubborn...how they win back the balls,block passes, put tnier bodies on the line is just a challenge and a puzzle we got to find answers by the tym waje kwetu...
 
Kama hauna mood kutokana na tokeo sio kila mtu lazima ureply comment yake jichukulie kimya.

Moja ya mechi nimetoka bila maumivu makubwa we played very well. Na hii itafanya umakinifu uongezeke
Hii mechi ni tofauti na last season hapa hapa kwao, kwan tulikua tunakabia sana chini ila leo tumefunguka (nikajiuliza wamepungua kiwango au tumeongezeka kiwango au ni game plan tu).
Mbali na yote we failed to convert created chances into goals, kama utashindwa kuscore unampa opponent wako energy ya kuendelea kupambana.
Goli la pili ile blunder niliipenda hhhhhhh muda mrefu hatujacheza blunder hivyo itaongeza umakiminifu sana.
Sijui lile zimwi la away matches kama la last season litatuandama au vp (sitarajii)
Kingine kuhusu klopp kutosajili tuliweke pembeni kwanza nahisi mambo mawili kwenye hili
1.)Hakuona wa kumfaa (refer ishu ya vvd,becker).
2.)Anataka kuprove mpira sio pesa tu hata off the matches (training) inakupa wachezaji wazuri
Credit kwa wote ila Andrian bado naendelea kusema ninaamini uwepo wake golini.Credit kwa fabby huwez kuamini millie na hendo walikua wakitesa tesa pale kati.

Napoli wapo vizuri na hua smart sana hasa wakicheza na sisi.

YNWA
 
Uliliona kama nililoliona

Milner na Henderson ni wachezaji ambao kama anawafanya starters anaifanya Liverpool kama midtable team

Nilipitia baadhi ya Comments kuna nyengine zinasema Hendo na Milner walikuwa wanatesa pale kati! Dah kweli tunatofautiana kwenye kuangalia mpira!
Yani Napoli wamezuia dimba la kati kwa dakika zote 90 halafu anatokea Mtu anasema tulikuwa tunatesa pale kati???
 
Kwenye hili Group tunapita ila concern yangu ni je tutaongoza hili kundi?

Kuongoza kundi kuna faida yake pale utakapoingia 16 bora na mpinzani utakayekutana nae! Kama hukuongoza kundi manake utakutana na kigogo atakayeongoza kundi.
 
Kwenye hili Group tunapita ila concern yangu ni je tutaongoza hili kundi?

Kuongoza kundi kuna faida yake pale utakapoingia 16 bora na mpinzani utakayekutana nae! Kama hukuongoza kundi manake utakutana na kigogo atakayeongoza kundi.
Kwa bahati mbaya hakuna tena timu vigogo za kutisha kivile...mpira umebadilika sana
 
Mwaka jana tulicheza vibaya kuliko jana na tulifungwa goal moja jana japo tumefungwa 2 lakini tumecheza vizuri kuliko mwaka jana. Mimi sioni kitu cha kupanick katika hili. Ni kweli kuna mapungufu lazima yafanyiwe kazi lakini usajili kwa sasa sio issue ni tuwatumie nani na nani kutegemea na game. Mwaka jana mechi zote za away tulifungwa. Kwa mechi ya jana kwa maoini yangu sio kwamba tulikuwa wabaya sana tumecheza vizuri kiasi sio kama mwaka jana ilikuwa hovyo. Team nzuri bado hatuwezi kuwa wiki hii team nzuri wiki ijayo team mbaya hapana tunacheza na team nzuri pia. Kwa mwaka huu mimi kama mshabiki wa Liver tukitoka CL wala sitakosa usingizi natamani Liv mwaka huu watupe karata zote PL ni lazima tubebe ubingwa home halafu tutakuja tena CL.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom