Rajab_Omar
JF-Expert Member
- May 15, 2016
- 16,480
- 27,185
Mpira mzuri bila kombe hata la FA ni ujinga wa Tottenham na Liverpool
Kuna Kitu Huwa Munakijua Lakini Munababaisha Kwa Makusudi.
Mara Nyingi Makocha Wanaoshinda Makombe Katika Misimu Yao Ya Mwanzo Huwa Wanshinda Kupitia Foundation imara Za Wengine. Lakini Kocha Aliyekuta Timu Katika Foundation Mbovu Basi lazima imchukue Muda Kujenga Foundation iliyoimara ili aweze Kushinda Makombe.
Nitakupa Mifano.
√ Mtazame Conte ambaye Ni Kocha Mbovu! Last Season alibeba Kombe la EPL Katika Msimu Wake Wa Kwanza na Mashabiki Wa Chelsea Wakaona Wamepata Bonge la Kocha!
Kumbe timu aliyoshindia Kombe Kaikuta Kamili ambayo ilishatengenezwa na Na Foundation ya Mourinho. Alipoipangua Kwa Kutoa Key Players Matic & Costa na Kujenga Foundation Yake Ya Kina Drinkwater, Zappacosta na Bakayoko, muangalie Timu anapoipeleka.
√ Mtazame Wnger Miaka Ya Mwazo 1996 kuja Arsenal Na Kukuta Timu imeshajengwa Foundation imara alivyokuwa na Mafanikio ya EPL, Lakini alipoanza Kujenga Foundation Yake Ya Kina Abou Diaby na Welbeck nadhani unajua Kilichomtokea.
√ Ferguson Baada Ya Kuichukua Man United Mwaka 1986 aliikuta Katika Foundation Mbovu ikamchukuwa Miaka 6 kuijenga mpaka Mwaka 1992 akafanikiwa Kuijenga Foundation imara iliyodumu Kwa Miaka isiyopungua 20. Hatimae Foundation hile Watu Wa Mwisho Kabisa Walioimalizia Ni Paul Scholes, Garry Neville na Ryan Giggs.
Baada Ya Hapo Fergie Akaondoka Akawaachia Warithi Balaa lililopo.
Sasahivi ndiyo Mourinho anajitahidi Kutaka Kutengeneza Foundation imara.
√ Zidane Ni Kocha Aliyepata Mafanikio Kwa Haraka, Lakini angalia Timu imara aliyoikuta ya Kina Ramos, Marcelo, Kroos, Modric, Ronaldo, Bale na Benzema Je Ni Foundation Yake? Ukweli Ni Kwamba Ni Foundation ambayo Kwa 90% Mourinho anahusika. Lakini Subiri Imalizike Foundation Ya Wachezaji aliwakuta ambao wengi wao umri umeshawakimbia ikisha atengeneze Yake ya Kina Asensio na Vasquez uone Mafanikio Yake.
√ Barcelona ilianza Kupata Mafanikio Baada Ya Ridjkad Kuanza Kutengeneza Foundation yake (Ronaldinho, Deco, Eto'o, Yaya Toure) akisaidiwa na Foundation Ya La Macia (Xavi, Messi na Iniest) wakati Huo ikiwa inaanza Kuleta impact.
Hatimae Guardiola akawakuta La Macia Tayari Wameshafikia Katika Peak ndiyo Akafanikiwa Kwa Kiasi Kikubwa Kwa Kikosi Kilichodumj Takriban Miaka 10.
Sasahivi La Macia inaelekea Ukingoni basi Unaona Wanavyonyanyaswa na Hata Roma! Sasa Sijengi Picha Yule Mchawi Messi anaetumia Jitihana Zake Binafsi atakapofikia Ukingoni sijui itakuaje.
TUJE KWENYE POINT:
Na Yeye Klopp huu Ni Msimu Wa 3 tokea aje Liverpool! Lakini To be Honest iangalie Foundation aliyoikuta Ya Kina Mignolet, Henderson, Kolo Toure, Benteke, Lovren, Skirtel, Lucas, Can, Clyne, Moreno, Origi n.k. Ni Kweli anaweza Shinda Kombe?
Lazima imchukue Muda Kujenga Foundation Yake Imara itakayoweza Kuleta Mafanikio.
Na Sasahivi Ndiyo unaona Yupo Anaendelea Na Ujengaji Wa Timu.
Kwavile Timu Hakuikuta na Baadhi Ya Mapungufu tu Kama Atayaziba Kwa Msimu Mmoja Kama Alivyofanya Guardiola! itambidi achukue Muda Zaidi Ya Misimu 3 ili kuijenga Kwani Kaikuta Timu Yote Nzima ina Mchezaji Mmoja tu (Mtoe Coutinho) Anayedeserve Kucheza First XI ambaye Ni Firmino Peke Yake.
Klopp inambidi Ajenge Wachezaji Wote10 waliobakia na Benchi la Subs jambo Ambalo Haiwezekani Kununua Wachezaji Wa Timu Nzima Kwa Msimu mmoja au Miwili.
• Msimu Wake Wa Kwanza Alianza Kujenga Kwa Kumnunua Sadio Mane na Kumpandisha TAA kutoka Academy.
• Msimu Wa Pili Akamnunua Mo Salah, Robertson na VVD
• Na Msimu Huu Kamnunua Keita na Fabinho na Huenda Akamnunua Nabil Fekir, CB na GK.
Sasa Hapo itakuwa Tayari ameshajenga Foundation Yake Mwenyewe na Ndiyo anaweza Kushindania Makombe.
