Leo Tupo Uwanjani Tunakipiga Na Roma!
Wengi Kati Yetu [HASHTAG]#Scousers[/HASHTAG] Wameshaamini Kuwa Tayari Tumeshamaliza Ligi na Tunabeba Kombe!
Lakini Mimi Mwenzenu Mawazo Yangu Ni Tofauti! Ninachoamini Mimi Kazi Hasa Ndiyo inataka Kuanza na Kwenye Mpira lolote laweza Kutokea pale usipopatarajia.
Kwahiyo siwezi kurelax Kwa Kutegemea Roma Tutamgonga Fasta na Final Tutapiga Mtu Kiulaini ili Tubebe Kombe Kibwegebwege.
Its too Early Kujiproud Kwa Ubingwa Kwasasa! Wacha Niangalie Upepo Unavovuma Kwani Klopp Ana Rekodi Mbaya Zaidi Ya Kupoteza Fainali.
Mkuu kwa game ya Liverpool na Roma hii match ya kwanza ni ngumu kujua nani anafungwa .
Kwa walipo toka huko hizi timu inakuwa ngumu kusema nani anapoteza,watu wanashindwa kupima uwezo.
Hii inatokana kwamba hizi timu zote mbili watu walikuwa wanazichukulia poa,ila ndio hivyo zimetinga hapo nusu fainali nakuzitoa timu zilizokuwa zinaaminika ni kubwa.
Ila mtazamo wangu mimi Liverpool tunashinda leo bila wasiwasi .vijana wanacheza kwa morali ya hali ya juu sana.
Game za roma nilibahatika kuziona game ya kwanza na shaktah donesk walifungwa roma 2-1,wakaja kupindua matokeo Italy wakashinda goli moja lililofungwa na dzeko
Mechi iliyofuata ilikuwa na barca hii niliiona yote barca alishinda 4-1,walivyokuja Barca Italy jamaa wakapindua matokeo wakashinda 3-0,
Nilichokiona kwenye mechi za roma wanatumia sana mipira mirefu wakiwa wanaitaji matokeo ,mfano wa mechi ya barca ya pili kuanza tu mchezo mtu katoka pass ya goli yupo katikati ya uwanja yanii kwenye ule mshari wa kati piga hatua moja kuelekea golini kwa barca.
wachezaji wa roma wenyewe wanatuogopa walikuwa wanataka tusikutane nao Maana wakikutana na sisi wanajua safari yao imeishia hapo
Gary Mcallister alipohojiwa na hata management yote ya Liverpool wanakuwa wanawachukulia Roma kama timu kubwa sana wanakuambia wamewatoa barca sio timu ndogo kwa hiyo najua kabisa leo tunaingia uwanjani tukijua tunacheza na timu kubwa