Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Tetesi

Liverpool wameandaa mkataba wa miaka mitatu kwa ajili ya mchezaji wa safu ya kati wa Manchester United Mbelgiji Marouane Fellaini, huku Paris St-Germain na Monaco pia wakionyesha kumtaka kijana huyo mwenye umri wa miaka 30 ambaye mkataba wake katika Old Trafford unamalizika mwisho wa msimu. (L'Equipe -kwa Kifaransa)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema pendekezo la Manchester City kwamba klabu hiyo inaweza kutumia uwanja wake wa mazoezi kwa maandalizi ya mechi ya marudiano ya robofainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Jumanne lilitolewa kwa kuchelewa.

Manchester United pia walikataa ombi kutoka kwa Liverpool wa kutumia uwanja wao wa timu ya wachezaji chipukizi. (Telegraph)

Kiungo wa kati wa Liverpool Mjerumani Emre Can, 24, ambaye mkataba wake wa sasa unafikia kikomo mwisho wa msimu huenda akaamua mustakabali wake katika kipindi cha wiki mbili zijazo, kwa mujibu wa mkuu wa Juventus Beppe Marotta. (Mediaset Premium, kupitia Express)
 
Tetesi

Liverpool wameandaa mkataba wa miaka mitatu kwa ajili ya mchezaji wa safu ya kati wa Manchester United Mbelgiji Marouane Fellaini, huku Paris St-Germain na Monaco pia wakionyesha kumtaka kijana huyo mwenye umri wa miaka 30 ambaye mkataba wake katika Old Trafford unamalizika mwisho wa msimu. (L'Equipe -kwa Kifaransa)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema pendekezo la Manchester City kwamba klabu hiyo inaweza kutumia uwanja wake wa mazoezi kwa maandalizi ya mechi ya marudiano ya robofainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Jumanne lilitolewa kwa kuchelewa.

Manchester United pia walikataa ombi kutoka kwa Liverpool wa kutumia uwanja wao wa timu ya wachezaji chipukizi. (Telegraph)

Kiungo wa kati wa Liverpool Mjerumani Emre Can, 24, ambaye mkataba wake wa sasa unafikia kikomo mwisho wa msimu huenda akaamua mustakabali wake katika kipindi cha wiki mbili zijazo, kwa mujibu wa mkuu wa Juventus Beppe Marotta. (Mediaset Premium, kupitia Express)
This will b a joke! Maruwani Fellaine kuvaa uzi wa Liverpool. Wapo wachezaji ambao ni top class na wa bei nzuri. Sako la Amerca kusini na baadhi ya nchi za ulaya kuna wachezaji wazuri tena wenye ndoto ya kucheza Liverpool.

France, Serbia,Croatia na Belgium na hata German huko kina vijana wachezaji wazuri tu sio kutuletea migalasa iliyojichokea.

Hivi liver hawana scout?

Plz Klopp usituletee huyu mtu tafadhali.
 
This will b a joke! Maruwani Fellaine kuvaa uzi wa Liverpool. Wapo wachezaji ambao ni top class na wa bei nzuri. Sako la Amerca kusini na baadhi ya nchi za ulaya kuna wachezaji wazuri tena wenye ndoto ya kucheza Liverpool.

France, Serbia,Croatia na Belgium na hata German huko kina vijana wachezaji wazuri tu sio kutuletea migalasa iliyojichokea.

Hivi liver hawana scout?

Plz Klopp usituletee huyu mtu tafadhali.


Mkuu Usiumishe Kichwa Kwa Habari Za Udaku Kama Hizi!

Key Points:

• Klopp Hajadadisi Wala Kuzungumzia Kuhusu Kumtaka Fellaini.

• Liverpool na Manchester United Hazihamishiani Wachezaji Kwani Mchezaji Wa Mwisho Kuhamishiana Timu Hizi ilikuwa Mwaka 1964.

• Chanzo cha Hii Habari Ni Gazeti moja la Ufaransa Ambalo Halikusema Habari hii weitoa Wapi.

Kwahiyo Habari Hizi Ni Za Uongo.
 
7078109f-9a3d-4f01-8f9c-53abec599965.jpg

Mind game
Salah ana anza leo!
 
Leo katika Uwanja wa Etihad mjini Manchester, vijana wa mji huo Manchester City wanawakaribisha vijana kutoka mjini Liverpool.
Ni katika mchezo wa marudiano robo fainali ya mabingwa Ulaya ambapo kwa hakika Man City wana kibarua kizito sana kwani wanatakiwa kuifunga Liverpool bao 4-0 maana mechi iliyopita, Man City walibamizwa 3-0 pale Anfield mjini Liverpool.
Kiungo wa City, Fernandinho mwenye umri wa miaka 32 anasema lile juma gumu lililowakabili la kuchapwa kila walikoenda sasa limeisha na ni wakati sasa wa wachezaji wazoefu kuchukua nafasi yao na kuliongoza Jahazi.
Tangu Man City walipopoteza pale Anfield jumatano, pia katika ligi walichapwa 3-2 na Manchester United.
Liverpool ilifunga mara tatu ndani ya dakika 19 za kipindi cha kwanza katika mzunguko wa kwanza.

Ikiwa upande wa Jurgen Klopp utaweza kushinda katika Uwanja wa Etihad, City watalazimika kushinda angalau mara tano ili kuendelea kufikia nafasi ya nne.
Ni Timu mbili pekee katika historia ya Champions League ambazo zimewahi kujikwamua kutoka katika deni la magoli matatu au Zaidi katika kipindi cha mtoano. Sawa na deni analokabiliana nalo Man City.

Deportivo La Coruna ikiwa nyuma ya AC Milan 4-1 mwaka 2004 walifanikiwa kupindua matokeo kwa 4-0 in katika mechi ya marudiano.
Katika siku za hivi karibuni, ni Barcelona iliyobadilisha matokeo ya 4-0 dhidi ya Paris St-Germain kwa kushinda 6-1 katika mechi ya marudio uwanja wa Noe Camp msimu uliopita.
Katika mchezo mwingine wa marudiano robo fainali ya mabingwa Ulaya, Roma itashuhudiwa wakikwaana na Barcelona katika uwanja wa Stadio Olimpico.
Meneja wa Roma Eusebio di Francesco amekiri kwamba kwa hakika kukutana na Barcelona anakutana na alichokiita Mashine lakini anabaki na matumaini makubwa.

Waitaliano hao wanakutana na Wahispania huku waitaliano wakiwa na hasira za kuchapwa bao 4-1 katika mzunguko wa kwanza.
Pia Roma walichapwa 2-0 na Fiorentina aliyeko nafasi ya saba na sasa wana point 21 nyuma ya viongozi wa Seria A Juventus
Katika hali ya tofauti, Barcelona wakiwa na Lionell Messi wako pointi 11 juu na bado Meneja wao Ernesto Valverde pamoja na kuwa watakuja na faida ya magoli matatu kibindoni bado amesema mechi hii dhidi ya Roma hawataichukulia kawaida na kwa hakika wataingia Uwanjani kama vile matokeo ni 0-0.
Katika upande wa Championship Cardiff City wataondoka katika nafasi ya pili kama watashindwa kuwapiga Aston Villa na iwapo pia Fulham itawachapa Reading wanaopambana kujiokoa kushuka daraja.
 
Wale nyuki mliowachokoza mkitegema watatung'ata sasa leo mnao.. watieni moto tu kabisa wafe vinginevyo watawafedhehesha...

All the best watani


Huenda Nyuki Wakatutafuna Lakini Wasituache Mahututi...

Kwahiyo Kutufunga Leo it doesn't matter! Kilichomuhimu Ni Je Wataweza Kututoa???

Kutufunga Wanaweza Lakini Kututoa Hawawezi.
 
Huenda Nyuki Wakatutafuna Lakini Wasituache Mahututi...

Kwahiyo Kutufunga Leo it doesn't matter! Kilichomuhimu Ni Je Wataweza Kututoa???

Kutufunga Wanaweza Lakini Kututoa Hawawezi.
Ndio kaka mi nakukubali sana analysis zako japo leo kuna uwezekano mkubwa tusishinde lakini kututoa hawawezi...
YNWA
 
Eithad hua tunapata ushindi hata ile mechi kabla ya kadi ya Mane tulikua tunakwenda sawa na hawa the Blus....naamani leo ushindi upo haijalishi magoli mbali semi final tukwendaaa...YNWA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom