CB patner wa VVD awe nani kati ya Lovren n Matip?
Sababu Aguero hachezi nadhani Lovren anamuweza Jesus
Kwa Kweli Hawa Lovren & Matip Ni Vigumu Sana Kujua Bora Ni Yupi Kati Yao Kwani Hata Klopp Mwenyewe Bado Hajajua Ni Yupi hasa bora kwa Kuanza.
Matip Baada ya Kuwa anakabiliwa na injury za mara kwa Mara basi Kapoteza Confidence na anafanya Makosa kadhaa ya kuweza Kuicost team!
Lakini Ubora wake dhidi ya Lovren unakuja Pale Katika Kucheza Mipira Ya Juu (Kwa Kichwa) jambo ambalo Matip anakuwa na Uwezo Mkubwa Wa Kucheza Mipira Hiyo.
Lakini Kuhusu Lovren Yeye Ni Mchezaji Katu Asiyefundishika na Asiyerekebishika! Anaweza Cheza Uzuri Michezo Mitatu lakini Akaja Akatucost Kwenye Mchezo Muhimu zaidi usiosahaulika! Kumbuka Kwa Everton, Sevilla na Man United.
Lovren Hajui Kukaba mtu wala kuintercept Mipira inayopenyezwa Ndani Ya Boksi kwa Mastrikers.
Udhaifu Mkubwa Wa Lovren Huyu Jamaa Hawezi Kabisa Kucheza Mipira Ya Juu Kiasi Ya Kwamba Hata Aruke na Mchezaji Wa Chandimu pale Mbagala basi Lovren hatoweza Kucheza kwa Kichwa Mpira huo. Hili Linasababishwa Kufungwa Magoli ya Kizembe Kwa Set-Pieces na Zile Cross.
Kwahiyo Mimi Nahisi Bora Game na Man City bora Aanze Joel Matip Kwani Anaonesha Ubora Kuliko Lovren.
Matip Hata Kuchezesha Mpira Kwa Viungo wake Ni Playmaker Mzuri sana Ukilinganisha na Lovren Ambaye Ni Mbutuaji tu anapopata Mipira.
Na mtu Hatari Mkuu sio Jesus! Ni Sterling na Leroy Sane!
Sterling akitokea Pembeni Basi Robertson Sina Wasi atamdhibiti, Na Akitokea Katikati Basi Ni Rahisi Zaidi VVD kumdhibiti..
Lakini Tatizo lipo Kwa Leroy Sane! Ukweli Ni Kwamba TAA hana Uwezo Wa Kumzuia Sane kwa njia Yoyote Hile.
• TAA alistruggle Kashindwa Kabisa Kumzuia Rashford.
• Pia Jana TAA kastruggle na Kashindwa Kabisa Kumzuia Wilfred Zaha Kiasi ya Kwamba Alikuwa Akimgeuza anavyopenda.
Sasa Nina wasiwasi na Leroy Sane atakuja Kutusababishia Madhara Makubwa Sana.