Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Yupo sokoni au ndo hayo mambo ya kufika dau?
Ujio wa Neymar na Mbappe umemuumiza, anataka kuondoka. Kombe la mabara ndo alikuwa team captain na kikosi karibu kipya kabisa na walichukuwa ndoo. Ana kazi ya kutetea nafasi yake Russia.
 
Tetesi
Liverpool na Arsenal watalazimika kulipa takriban £90m kumsajili mshambuliaji wa Monaco Thomas Lemar, 22. (Mirror)

Lakini kulingana na mwandishi wa Ufaransa Julien Laurens, huenda akachelewesha uhamisho wake Liverpool kutokana na michuano ya kombe la dunia (5 live's Euro Leagues podcast)
 
usajili wa keita na VVD jumla yake ni paund mill 125..huku countinho akiuzwa kwa paund mill 145...hivyo kilichobaki ni paund mil 20..sitarajii usajili wowote wa kuzid hicho kilichobakia...au tupambane na vilivyopo..ni mawazo tuu ya kichaga yamenipeleka huku..
 
We inaelekea unamchukulia keni kama unavyomchukulia bakayoko
Umeshawahi kumuangalia rackit unazijua faida zake katika team? Anapiga mbali anakaba na Ku attack usiwe mtumwa wa mpira wa UK nenda kamuangalie usifanye mahaba ya kijinga mchezaji wako can team yake ya taifa hana ata namba utamlinganisha na Ivan?
 
Umeshawahi kumuangalia rackit unazijua faida zake katika team? Anapiga mbali anakaba na Ku attack usiwe mtumwa wa mpira wa UK nenda kamuangalie usifanye mahaba ya kijinga mchezaji wako can team yake ya taifa hana ata namba utamlinganisha na Ivan?
Ivan German anaweza kupata namba?
 
Kweli haya mahaba rakitic unamlinganisha na can?

Kweli mashabiki wa liver hamna ubongo au mpira huwa mnaangalia kwa kutumia makalio?


RAKITIC & CAN

Ni Wachezaji Wawili Tofauti Wenye Kucheza Position Tofauti na Wana Majukumu Tofauti.
Bila ya Kueka Biase mbele basi Kila mmoja Namsifia Kwa Kuwa Bora Kwa Position Yake.

EMRE CAN
Ni natural DEFENSIVE MIDFIELDER ambaye Ana Sifa kuu Kama Vile:

I) Ni Destroyer
II) Anacheza Box-2-Box midfielder
III) Holding midfielder
IV) Not Good enough Creative Midfielder
V) Pace
VI) Not injury Prone
VII) Young boy

IVAN RAKITIC
Ni natural Central Midfielder ambaye anasifa Kuu kama vile:

I) Creative Midfielder
II) Holding Midfielder
III) Can't blay Box-2-Box
IV) Pace
V) Not destroyer
VI) Age problem
VII) About injury not too bad.

Kwahiyo Hapo Kila mmoja Ni Mzuri Kuliko Mwenziwe Kwa Sifa Zake na Position anayocheza!
Messi Ni Mzuri Lakini Ubora Wake Huwezi Mlinganisha na UMTITI.... Katika Position ya Ulinzi basi Umtiti atakuwa Bora Kuliko Messi.
 
IMG_20180111_180614.jpg
 
£17m Just for 4 months?

Katika Mzungumzo Yanayoendelea Ya Liverpool na RBL kuhusu Kumchukua Nabby Keita Katika Mwezi huu Wa January Kuna jambo sijaliafiki bado..!

RBL ili wamruhusu NK Kuna Liverpool Katika Mwezi huu Wa January wametaka Ni lazima Liverpool ilipe nyongeza ya £17m...

Nahisi Haina Haja ya Kuongeza Hela Yoyote bora Tusubiri Mpaka Summer aje manake Wameziona Hela alizouziwa Coutinho basi Wanachachawa.

Intact Timu inamatatizo mengi lakini Kwasasa Baada Ya Kusawazisha Beki tatizo Kubwa lililobakia Ni Kipa na si Midfielder.
Then Striker Wa 20+ goals per season.
 
Arsene Wenger anatuharibia Deal letu Kwa Thomas Lemar

Kiukweli Jamaa Kaweka Wazi Kuwa Anataka Kujiunga na Liverpool Kuliko Timu Yoyote hile Ya Premiere League!

Lakini Wenger anachokifanya Ni Kumpandisha Bei siku hadi siku Mchezaji Huyo Mpaka Sasa Kashamfikisha £90m huku akijua Wazi Kuwa Hawezi kujiunga na Arsenal
jambo ambalo litatufanya tushindwe kumnunua Kwani Wanaweza kumfikisha £100m.
 
MORENO vs ROBO

• Moreno: Ana Pace na Ni very Accurate attacking full back! Cross Zake Zinakamilika kwa 90% na Ni mbora Katika Mashambulizi ukimlinganisha na Robertson.
Lakini Katika Kulinda Moreno amekuwa Akifanya Makosa Yenye Kujirudia Mara Kwa Mara yakiwemo Kucheza Careless tackles Katika Maeneo Hatari Yanayosababisha Set-Pieces au Penalty.
Na vile hayuko Makini Katika Kukaba ukilinganisha na Robertson.

• Robertson: Ni Mzuri Katika Kukaba Kuliko Moreno na Huwa Makini anapocheza Tackles Katika Maenero Hatari Kiasi Ya Kwamba sio Maranyingi Kusababisha zile Dangerous Set-Pieces wala Penalty.
Lakini Hayuko Vizuri Katika Kushambulia Kwani Cross Zake hufanikiwa Kwa Asilimia isiyozidi 10%... Pia Hana Pace kama ya Moreno.

MY TAKE:
Moreno Ni Offensive Full back, But Robo Ni Defensive Full back.

So, Tunapocheza Na Timu ambayo Inashambulia Zaidi Kuliko Kulinda Kama Man City, Spurs au Arsenal Basi Ni Bora Kumchezesha ROBERTSON.

Lakini Tunapocheza na Timu ambayo inalinda Zaidi Kuliko Kushambulia kama Man U na Baadhi ya Midtable Teams basi Ni Bora Tukamchezesha MORENO.

[HASHTAG]#JustMyOpinion[/HASHTAG]
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom