Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Mmmhh potezea bana. Mie mwenyewe nilishushuliwa kweli kuhusu coutinho
We mjinga ndo ulinambia kuwa labdaJanuary nife mm ila sio Coutinho aende barca si ndiyo??????!! Naona yamekuwa vice versa.....ulikuwa unatumia nn kuongea ama kuandika hivyo??????!!!...sikulaumu saaaana coz yawezekana si kosa lako.......kunguru!!!!
 
Mhh!!! Kajitahidi sana magoli yote hayo....... Ni halali wamng'ang'anie...
 
Tungepata kama yupi mkali anae uzwa?
 
Kumpata zaidi ndo jasho sasa kwa sasa huyu ndo yuko juu ndoana wametoa kiasi kikubwa
 
Wachezaji Watano ghali zaidi duniani.

1. Neymar Jr
2. Coutinho
3. Dembele
4. Mbappe
5. Pogba
 
Reds wamethibitisha kuwa Coutinho atajiunga na Barcelona kwa kitita cha paundi milioni 142 mwezi huu, kumfanya Mbrazili huyo kuwa mchezaji wa pili ghali duniani wa muda wote baada ya Neymar.
Ripoti za muda mrefu zimedai kuwa bosi wa Liverpool Jurgen Klopp anataka kumleta Thomas Lemar kutoka Monaco kuziba pengo la Coutinho, lakini beIN Sports kimedai kuwa badala yake wanataka kumsajili Mahrez.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 amehusishwa kwa muda mrefu na tetesi za kutaka kuondoka King Power tangu alipowasaida Foxes kutwaa taji lao la Premier League 2016, ambako alitajwa kuwa mchezaji bora wa PFA wa mwaka.
Liverpool sasa wameripotiwa kuwa tayari kutumia paundi milioni 49 katika fedha watakazopata kwa kumuuza Coutinho kumsajili Mwalgeria huyo, ambaye yupo mbioni kusaini mkataba wa miaka minne na nusu Anfield.

Mahrez amefunga magoli nane na kutengeneza mengine saba katika mechi 26 alizocheza kwenye michuano yote msimu huu, ikiwa ni pamoja na magoli matano na pasi tatu za goli katika mechi 10 za mwisho.
 

Jurgen Klopp amekiri kuwa Philippe Coutinho aliweka bayana kwa kila mmoja, ikiwa ni pamoja na wachezaji wenzake kuwa anatamani kuondoka kujiunga na Barcelona, jambo ambalo isingewezekana kumbakisha Liverpool.
Uhamisho wa nyota huyo wa Kibrazili kwenda Camp Nou ulitangazwa Jumamosi, baada ya mchezaji huyo kukubali kusaini mkataba wa miaka mitano na nusu kufuatia malipo ya ada ya uhamisho ya €160 milioni na Barcelona wakiweka thamani yake kuwa €400 kwa klabu itakayomtaka.

Coutinho amekuwa shabaha ya miamba hao wa La Liga kwa muda mrefu lakini jaribio lao kumsajili liligonga mwamba mara kadhaa Julai na Agosti.
Jurgen Klopp hakufurahi kuona mchezaji huyo akiondok, ingawa hakuwa na namna ya kumzuia mchezaji huyo kwani alimweka wazi yeye na mmiliki wa klabu kadhalika na wachezaji wenzake kuwa anataka kuondoka.

Ni kwa kusita mno - sisi kama timu na klabu tunajiandaa kumuaga rafiki yetu mwema, mtu wa kipekee na mchezaji mahiri Philippe Coutinho," aliiambia tovuti rasmi ya Liverpool.
"Siyo siri kwamba Philippe alitaka kuondoka tangu Julai, mara ya kwanza nia ya Barcelona ilipofahamika.
"Philippe alinisisitizia mimi, wamiliki na hata wachezaji wenzake kuwa alitamani jambo hili litokee.

Licha ya kuwa tulifanikiwa kumbakisha mchezaji baada ya dirisha la uhamisho wa majira ya joto, tukiamini kuwa tungeweza kumshawishi kubaki na kuwa sehemu ya kile tunachotaka kufanya.
"Naweza kuwaambia mashabiki wa Liverpool kuwa, sisi kama klabu, tumefanya kila tulichoweza kumshawishi Philippe kubaki kama sehemu ya LFC, lakini yeye ndiye mwamuzi mkuu wa mustakabali wake - akaamua kwamba yeye na familia yake wanataka kwenda Barcelona.
"Ni ndoto yake na sasa nimeshawishika kuwa hakuna namna naweza kuibadili akili yake."
Coutinho alitua Merseyside mnamo 2013 na amecheza mechi 152 za Premier League, akiweka kimiani mabao 41, na Klopp amezisifia jitihada zake.

"Wachezaji watakuja na wachezaji wataondoka, huo ndio mpira, lakini kama klabu tupo thabiti na imara kuendelea na kazi yetu nzuri dimbani, hata kama tukimpoteza mchezaji muhimu.
"Hatujawahi kuwa katika nafasi nzuri kipindi cha hivi karibuni, kama klabu. Tutatumia idadi yetu na uthabiti wetu kukabiliana na hali kama hizi na bado tutasonga mbele.
"Nimekuwa hapa kwa muda mrefu kiasi cha kuifahamu vema historia ya Liverpool, wachezaji muhimu wameshaondoka - lakini klabu umesonga mbele. Huwezi kuhamisho moyo na roho ya Klabu ya Liverpool, ingawa natambua kwamba kuna klabu nyingi zinaitamani.
"Kwa hiyo tunapomuaga Philippe, tunaendelea kwenda mbele na kufanya maendeleo kwani tunapambana kutimiza lengo kuu la kuleta mataji Anfield."
 
Ni vicious cycle hata hao kina Keita,Salah,Mane wataondoka na utasema hakuna pengo wameacha,Coutinho anaondoka akiwa tayari amesha-mature tofauti na misimu yote aliyocheza angalia statistics zake kosa ni kumuuza katikati ya msimu while ni ngumu kupata replacement
 
Ni ukweli unaotuuma lakini ni ukweli na ukweli siku zote huwa unauma
 
Very nice speech.
 
Usiogope, Liverpool ni kubwa kuliko Coutinho, kwani mbona mechi nyingi tu tumeshinda pasipo yeye?
 
wakuu kwa Januari hii binafsi ningependa kuona Klopp akimsajili Lianzini wa Westham, kipa wa uhakika na strika mmoja pengine Surez arudi..
Maana hii pesa ya C10 isipotumika vzuri kwa kweli hata Klopp atachomoka
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji13] [emoji13] lini hiyo mkuu!??
Msimu ujao 2018/2019 mkuu ndio msimu wa EPL kutua kwa jiji la Anfield....Klopp amebakisha usajili wa wachezaji wanne tu kukamilisha kikosi cha kuchukua ubingwa wa EPL...
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…