We mjinga ndo ulinambia kuwa labdaJanuary nife mm ila sio Coutinho aende barca si ndiyo??????!! Naona yamekuwa vice versa.....ulikuwa unatumia nn kuongea ama kuandika hivyo??????!!!...sikulaumu saaaana coz yawezekana si kosa lako.......kunguru!!!!
Hhhhhhhh......haya bhana it's okay..Mmmhh potezea bana. Mie mwenyewe nilishushuliwa kweli kuhusu coutinho
Mhh!!! Kajitahidi sana magoli yote hayo....... Ni halali wamng'ang'anie...Baada ya tetesi nyingi kumuhusu mshambuliaji wa klabu ya Liverpool, Philippe Coutinho kuhamia Barcelona, sasa sio tetesi tena bali ni rasmi mchezaji huyo amejiunga na mabingwa hao wa Hispania.
Coutinho amejiunga na Barcelona kwa dau la Euro milioni €160 na tayari ametua nchini Hispania kwa ajili ya vipimo.
Coutinho (25) amesaini mkataba wa miaka mitano na nusu ambao unadhani ya Euro milioni 400 na leo jumapili atakuwa uwanjani kuishuhudia timu yake mpya ya Barcelona ikiivaana na Levante katika mchezo wa Ligi kuu nchini humo (La Liga).
Hadi kuhama kwake, Coutinho akiwa Liverpool amecheza mechi 201 na kuifungia magoli 54, na alijiunga na Liverpool akitokea Inter Millan kwa dau la Euro milioni €8.5 .
Kwa mujibu wa mtandao wa Klabu ya Barcelona umesema kuwa kesho jumatatu mchezaji huyo ataungana na wachezaji wenzake kwenye mazoezi .
Tungepata kama yupi mkali anae uzwa?Hapa mkuu timu za uingereza ndipo zinapofeli unamuuza coutinho una mnunua mahrez wa nn? Barca wameuza neymar nunua coutinho manchester uza ronaldo sajili valencia na owen liverpool uza suarez sajili banteke chelsea fukuza costa chukua morata hatar sana.
Kumpata zaidi ndo jasho sasa kwa sasa huyu ndo yuko juu ndoana wametoa kiasi kikubwaKwa pesa liverpool waliyoingiza wanaweza sajili mchezaj yoyote aliekamilika kama akikubali kujiunga na liverpool isipokuwa Ronaldo,mess,neymar, isco mkataba wake mpya £800 nahisi na mbape na coutinho mwenyewe mana ilikumuachia kwa sasa lazima ziwepo mezan £400
Kwa hiyo liverpool wanatakiwa wasake mtu zaidi ya coutinho sio mahrez tena.
Hivi Mahrezi akishain pale si vilevile tu muhimu nikua na mwalimu mzuri tu sasa hivi Salah mimacho inawatokaNdio ubovu wa timu za EPL
Mahrez sitaki hata kumsikiaHivi Mahrezi akishain pale si vilevile tu muhimu nikua na mwalimu mzuri tu sasa hivi Salah mimacho inawatoka
Timu ni kocha, hivyo Klopp ni cocha mwenye uwezo, Liverpool itakuwa vizuri tu hata pasipo CoutinhoCoutinho nilikuwa namkubali tangu zaman2
Ni vicious cycle hata hao kina Keita,Salah,Mane wataondoka na utasema hakuna pengo wameacha,Coutinho anaondoka akiwa tayari amesha-mature tofauti na misimu yote aliyocheza angalia statistics zake kosa ni kumuuza katikati ya msimu while ni ngumu kupata replacementNi Kusahau au Kutokuijua Liverpool Lakini Ukweli Ni Kwamba Impact aliyoiacha Xabi Alonso Liverpool ilikuwa Kubwa Zaidi Kuliko Anayoiacha Coutinho Kwani ilitucost Kuanzia Siku aliyohama Mpaka Kuzibika Kwa Kuja Klopp Hapa Liverpool kuanzia Last Season.
Impact Ya Coutinho kama Kuwepo itasalia Miezi hii Mitano Ya Msimu huu tu! Lakini Next Season 2018/19 hakuna impact Yoyote itakayoonekana kama ilivyofichilika ya Gerrard Kufikia Hadi Leo Hakuna anayezungumzia Mchezaji wake.
Kuwa Mimi Ndiyo Klopp Basi Nisingesaini Lemar wala Draxler msimu huu! Bali Ningemkubalia Can Kumuekea Release Clause Katika Mkataba Wake kama anavyotaka.. Ningembakisha Na Kumchezesha DM Na Keita Nikamkabizi Majukumu ya Coutinho! Halafu Nikasajili Kipa Na Striker tu... Hapo Pasingelitokea Timu ya Kuizuia Liverpool.
Ni ukweli unaotuuma lakini ni ukweli na ukweli siku zote huwa unaumaNi vicious cycle hata hao kina Keita,Salah,Mane wataondoka na utasema hakuna pengo wameacha,Coutinho anaondoka akiwa tayari amesha-mature tofauti na misimu yote aliyocheza angalia statistics zake kosa ni kumuuza katikati ya msimu while ni ngumu kupata replacement
Very nice speech.View attachment 670332
Jurgen Klopp amekiri kuwa Philippe Coutinho aliweka bayana kwa kila mmoja, ikiwa ni pamoja na wachezaji wenzake kuwa anatamani kuondoka kujiunga na Barcelona, jambo ambalo isingewezekana kumbakisha Liverpool.
Uhamisho wa nyota huyo wa Kibrazili kwenda Camp Nou ulitangazwa Jumamosi, baada ya mchezaji huyo kukubali kusaini mkataba wa miaka mitano na nusu kufuatia malipo ya ada ya uhamisho ya €160 milioni na Barcelona wakiweka thamani yake kuwa €400 kwa klabu itakayomtaka.
Coutinho amekuwa shabaha ya miamba hao wa La Liga kwa muda mrefu lakini jaribio lao kumsajili liligonga mwamba mara kadhaa Julai na Agosti.
Jurgen Klopp hakufurahi kuona mchezaji huyo akiondok, ingawa hakuwa na namna ya kumzuia mchezaji huyo kwani alimweka wazi yeye na mmiliki wa klabu kadhalika na wachezaji wenzake kuwa anataka kuondoka.
Ni kwa kusita mno - sisi kama timu na klabu tunajiandaa kumuaga rafiki yetu mwema, mtu wa kipekee na mchezaji mahiri Philippe Coutinho," aliiambia tovuti rasmi ya Liverpool.
"Siyo siri kwamba Philippe alitaka kuondoka tangu Julai, mara ya kwanza nia ya Barcelona ilipofahamika.
"Philippe alinisisitizia mimi, wamiliki na hata wachezaji wenzake kuwa alitamani jambo hili litokee.
Licha ya kuwa tulifanikiwa kumbakisha mchezaji baada ya dirisha la uhamisho wa majira ya joto, tukiamini kuwa tungeweza kumshawishi kubaki na kuwa sehemu ya kile tunachotaka kufanya.
"Naweza kuwaambia mashabiki wa Liverpool kuwa, sisi kama klabu, tumefanya kila tulichoweza kumshawishi Philippe kubaki kama sehemu ya LFC, lakini yeye ndiye mwamuzi mkuu wa mustakabali wake - akaamua kwamba yeye na familia yake wanataka kwenda Barcelona.
"Ni ndoto yake na sasa nimeshawishika kuwa hakuna namna naweza kuibadili akili yake."
Coutinho alitua Merseyside mnamo 2013 na amecheza mechi 152 za Premier League, akiweka kimiani mabao 41, na Klopp amezisifia jitihada zake.
"Wachezaji watakuja na wachezaji wataondoka, huo ndio mpira, lakini kama klabu tupo thabiti na imara kuendelea na kazi yetu nzuri dimbani, hata kama tukimpoteza mchezaji muhimu.
"Hatujawahi kuwa katika nafasi nzuri kipindi cha hivi karibuni, kama klabu. Tutatumia idadi yetu na uthabiti wetu kukabiliana na hali kama hizi na bado tutasonga mbele.
"Nimekuwa hapa kwa muda mrefu kiasi cha kuifahamu vema historia ya Liverpool, wachezaji muhimu wameshaondoka - lakini klabu umesonga mbele. Huwezi kuhamisho moyo na roho ya Klabu ya Liverpool, ingawa natambua kwamba kuna klabu nyingi zinaitamani.
"Kwa hiyo tunapomuaga Philippe, tunaendelea kwenda mbele na kufanya maendeleo kwani tunapambana kutimiza lengo kuu la kuleta mataji Anfield."
Usiogope, Liverpool ni kubwa kuliko Coutinho, kwani mbona mechi nyingi tu tumeshinda pasipo yeye?Ni vicious cycle hata hao kina Keita,Salah,Mane wataondoka na utasema hakuna pengo wameacha,Coutinho anaondoka akiwa tayari amesha-mature tofauti na misimu yote aliyocheza angalia statistics zake kosa ni kumuuza katikati ya msimu while ni ngumu kupata replacement
Msimu ujao 2018/2019 mkuu ndio msimu wa EPL kutua kwa jiji la Anfield....Klopp amebakisha usajili wa wachezaji wanne tu kukamilisha kikosi cha kuchukua ubingwa wa EPL...[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji13] [emoji13] lini hiyo mkuu!??
Wazia hata carabao next season....EPL parefu mno kwako mkuuMsimu ujao 2018/2019 mkuu ndio msimu wa EPL kutua kwa jiji la Anfield....Klopp amebakisha usajili wa wachezaji wanne tu kukamilisha kikosi cha kuchukua ubingwa wa EPL...
Madrid nao wanataka kumchomoa salah