Ni gemu zuri kutazama kwakuwa inakutanisha timu mbili zilizo kwenye top Four ya Epl.Mbali na hilo timu zote mbili zinapenda mpira wa kushambulia.Hii inadhihirishwa na magoli timu zimefunga.Liverpool wamefunga magoli mengi zaidi mpaka sasa,magoli 45 huku city wakifuatia kwa kuwa na magoli 39 sawa na Arsenal.
Kuta za timu zote mbili zinaruhusu magoli.Liverpool clean sheets ni 28% huku city wakiwa na 22%.Kati ya timu zilizo kwenye top six kwa sasa kwenye table City inaongoza kwa kuruhusu magoli mengi zaidi,21, huku liverpool wakifuatia kwa kuruhusu 20.Kwahiyo hizi ni timu mbili zilizoruhusu magoli zaidi kati ya timu sita za juu.Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na staili ya uchezaji wa timu zote mbili kuwa ni wa kushambulia zaidi.So ni rahisi kufungwa magoli ya transition pale viungo wote wanapokuwa kwenye move kupeleka mashambulizi mbele na ghafla dispossession kutokea,mabeki wanakuwa exposed hapa.
Pia makocha Klopp na Guardiola wote ni wazuri wa kusoma mchezo na kuiadjust timu icheze kutokana na jinsi mpinzani wake anavyoonekana kuwa hatari.Sio makocha wa technic moja kama kocha wa manchester united ambaye plan A ikifeli basi plan B yake huwa ni kupiga teke chupa za maji na kuwakoromea waamuzi.
Kwahiyo tutegemee mchezo mzuri wa kufungia mwaka na timu ambayo itatumia nafasi za kufunga vizuri ndiyo itaibuka na ushindi.