Yaani msimu huu mimi nimeshaandika maumivu, ikiwa tofauti basi nitafurahi tu. Yaani timu inacheza unaitafuta Liverpool huioni, unajiuliza hivi hawa wachezaji ni wa Liver kweli au kuna wahuni tu wamevalishwa jersey zetu? Zamani kidogo niliwahi kumsikia mwenye timu mmoja nadhani ilikuwa timu kutoka Arusha, jina silikumbuki... alisema kwa hasira kwenye radio kuwa anavunja timu, mtangazaji akamuuliza sasa na wale wachezaji wafanyeje kama mnaifuta timu yenu? Jamaa akajibu; kila mtu aende kwa baba yake na mama yake! Yaani isingekuwa mikataba ya wazungu, hii michezaji yetu yote ilikuwa ya kuitoa baru tujue moja.