STOKE 0-1 LIVERPOOL - MTIZAMO WANGU
LFC tumeshinda lakini hatukustahili kutokana na mchezo mbaya tuliocheza kwa mpenzi yeyote wa LFC ilikuwa ni mechi ambayo naweza kusema ilikuwa very disgusting to watch. Kilichoweza kutusaidia kushinda ni ile kitu inaitwa one moment of magic ambayo inachangiwa na uwepo wa wachezaji special kwenye timu. Lakini mchango wa utaalamu wa mwalimu kwenye mchezo wa leo ulikuwa ni zero. Zilch!
Udhaifu
Timu ilikuwa inacheza kama vile haina malengo: slow, no runners, no passion, no pressing, no tenacity, unnecessary forward punts (long balls) by Mignolet, predictable passing, totally pedestrian.
Backline haikuwa na protection kabisa, ndio maana kila Stoke wakipia long balls zilizokuwa zinadondokea mbele au ndani ya box la LFC zilikuwa zinawapa shida sana akina Skrtel.
Benteke hakupata huduma za kutosha na alikuwa isolated muda mwingi kiasi kwamba ikabidi wakati mwingine aanze kucheza deeper kidogo, kitu ambacho si sahihi kama target man ni mmoja tu kwani mashambulizi yanakufa!
Uzuri
Ibe aendelee kuwemo kwenye starting XI, ni dhahiri anaweza kuwa ni creative outlet nyingine tegemeo ukiwaondoa Coutinho na Firmino. Anahitaji improvement kwenye final ball lakini mtoto yupo vizuri.
Subs ambazo alifanya BR kipindi cha pili, ingawa zilikuja zimechelewa sana, kwa kiasi fulani zilibadili complexion ya mchezo na timu ikaanza kuwa more offensive, especially kuingia kwa Can ambaye aliongeza mobility na defensive stability pale kati. Na Firmino alipoingia niliona cheche zake kwa mbali backline ya Stoke ikajikuta busier all of a sudden.
Maoni yangu
Kilio cha wengi wetu humu siku zote kimekuwa umuhimu wa kuwa na anchor-man pale kati ili kuwa-protect akina Skrtel. Kama BR anaona Lucas hatoshi basi amchezeshe hata kiraka wetu Can. Vinginevyo, tukicheza na timu yoyote iliyopo top 6, tunaweza kujikuta tunabugizwa kapu la mabao!
Unnecessary long balls za Mignolet zikome kwani ni kama kumpasia adui mpira bure.
Benteke hatakiwi kuondoka eneo lake la kazi i.e asiende zaidi ya 6 yards nje ya opposition box. Kinachohitajika sasa ni kuhakikisha Firmino anacheza naye mbele kwenye 2-striker role lakini yeye (Firmino) awe ana-drift back and forth in and around the box for up to 12 yards or thereabouts.
Where has our pressing gone? Where is our mobility? Where is our accustomed pace? Hizi ni ingedients muhimu na ndiyo identity yetu lakini sikuona hata chembe yake leo vs Stoke timu iliyocheza leo haikuwa LFC in my view. BR anahitajika kurudisha ID hii haraka kama kweli anataka kuendelea kuwa Anfield beyond January 2016.
In my opinion, timu inayotakiwa kuanza siku zote ni hii
.Mignolet, Clyne, Gomez, Lovren/Sakho, Skrtel, Can, Henderson/Milner, Ibe, Firmino, Coutinho & Benteke.
Am sure hii proposed line-up yangu inaongea mengi kuliko hata niliyoyaandika hapo juu.