Bruh, yanayoendelea sahiv huko ni balaa, nasemaga kila siku hii rodgers era itaisha vibaya sana, kama FSG wasipokuwa makini, kwa mfano mpaka sasa kishaigawanya Fanbase katika makundi makundi, mashabiki wenyewe tu hawaelewani, tunaweza tukawa tunalaumu sterling kaondoka kwa dharau lakin tusijue yaliyojili behind the scenes, kwanza kuna hili la sahiv, jamaa hawataki Balotelli, Borini na Enrique NA amewatenga na wenzie, yaan kina Balotelli wanatrain peke yao (manager anaejielewa hawez fanya huo ujinga hata kidogo)..jana kina Bascombe, Paul Joyce and Echo wanasema Sakho and Moreno watakuwa BackUp tu, na inawezekana Moreno huyohuyo na mwenzake Markovic wakauzwa au kutolewa kwa mkopo, sasa kuna maana gani ya kununua vijana na kuwachezesha msimu mmoja kisha kuwaona hawafai na kutaka kuwauza? Moreno katokea spain na Lazar katokea ureno, na ukiangalia bado ni wadogo wana mengi ya kujifunza, lakin baada ya msimu mmoja tu rodgers anataka kuwauza na FSG wanaangalia tu..
Tunaweza tukasema Markovic na Moreno hawakucheza vizuri msimu uliopita, lakin our worst player wa msimu uliopita Lovren anapewa nafasi msimu huu kwanini kina moreno nao wasipewe nafasi? Lucas ni SENIOR player wa 3-4 anaondolewa na Rodgers, FSG wanaangalia tu..Lallana kafanya kipi cha maana? Mbona anampa nafasi? Na Bascombe anasema eti Firmino bado hayupo fit kwa game ya bournemouth, sasa Asipomuanzisha Firmino hiyo game inayokuja ndo atawaelewa vizuri LFC fans..na uzuri itakuwa ni Anfield..