The Magnificent
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 2,694
- 1,250
Msimu uliopita Emre Can alichanganywa sana kupangwa maeneo tofauti tofauti ndani ya muda mchache na kuathiri maendeleo yake. Markovic pia alipangwa wing back upande wa kushoto na kulia wakati alikotoka alikuwa anacheza nyuma ya striker.
Pia Adam Lallana ambaye hana pace lakini alimtumia karibia maeneo matatu msimu uliopita katika kipindi kifupi jumlisha na majeruhi hivyo kumzuia kusettle.
Philippe Coutinho alicheza pembeni baadhi ya game wakati eneo analoweza kucheza na kuleta mafanikio namba 10 na kidogo akicheza kiungo deep.
Jordan Henderson naye alicheza katika namba tofauti msimu uliopita kadili alivyoagizwa na kocha.
Mkongwe Gerrard naye aliishia kuhangaishwa asijue eneo gani anaweza kutulia ukizingatia na umri wake na hata waliomzunguka walikuwa wakibadilika badilika nafasi zao.
James Milner ambaye anatarajiwa kuziba nafasi ya Gerrard ambaye man city alipangwa maeneo asiyopenda naye anakuja kwa BR anayebadilisha position za wachezaji.
Mateo Kovacic ambaye hajijui kama seheme anayoweza kufanikiwa ni namba 10 au acheze kama Andrea Pirlo naye anahusishwa kusajiliwa nasi.
Kuwa na wachezaji wanaoweza kucheza maeneo tofauti tofauti ni jambo jema lakini ukifanya mabadiliko mara kwa mara inaleta shida kwa sababu timu inakosa umoja na maelewano.
Mfano Wenger naye anao viungo wanaoweza kucheza maeneo tofauti tofauti lakini hakuwabadili mara kwa mara na kubadili formation na hii ilisaidia kujenga umoja na maelewano uwanjani. Kwa upande wa BR alikuwa tofauti hasa akitangulia kufungwa au akitaka matokeo angeweza kubadilisha position na subs na kupunguza maelewano.
Tumeshuhudia BR akishindwa kujua mfumo gani autumie msimu uliopita. Pamoja na ukweli kwamba mtindo huo ulisaidia sana msimu wa 2013-14 ni kwa sababu alikuwa na muda wa kutosha maandalizi kujenga maelewano kabla ya mechi.
BR OUT
Naunga mkono hoja