Kwenye msitu wangu kuna black mamba/ koboko natafuta njia za kumwangamiza bila kuleta madhara kwenye jamii

Watu wengi wamependekeza Hivo kuwa niruhusu wachoma mkaa ila Kwa sharti la kuwaambia waache baadhi ya miti pakiwa peupe hawezi kaa.

Kabla sijafanya hiyo njia nikawaza nililete humu lengo nikuwa mazingira yataharibika iwapo nitaruhisu wachomaa mkaa najua Fujo za wasukuma katika kukata miti Huwa wanaichimba Hadi visiki
Achana na mambo ya mkaa endelea na shughuli zako, kugongwa na nyoka ni bahati mbaya mkuu na kwake nyoka hapendi kugonga mtu (ni matumizi mabaya ya sumu ambayo anatumia kuwinda)

Mkianza shughuli atahama au atakuwa anapita usiku mchana anapotea. Kelele na mishe za raia zitamdogeza mbali

N.B. Tunakuhakikishia akikugonga na ukafariki MKE WAKO HAOLEWI kama jina lake (jokes)
 
Huyo nyoka ni hatari kama wengine tu ila story zake za wasukuma ndio zinafanya aonekane ameshindikana
Watu wakienda huko unyamwezini na usukumani kutembea, hurudi na story hizi wanazopigiwa na wenyeji wao wa huko. Alaf na wao hukimbilia kuzileta hapa JF bila kuzifanyia uchunguzi wa kutosha.
 

Attachments

  • Screenshot_20240327-121449.jpg
    Screenshot_20240327-121449.jpg
    298.5 KB · Views: 3
Naona unataka kuleta ubishi usiokuwa na maana. Lakini pia haujajua ni kwanini huyu alipewa jina la King Cobra.
Huku Afrika hatuna King cobra ndugu, wapo Asia. Hapa Afrika tuna Mozambican spitting cobra (anatema mate na kusimamisha shingo) na forest cobra (hatemi mate ila anasimamisha shingo), ambao ni wadogo kiumbo kwa king cobra.
 
Usijal mkuu, najua katika dunia ya leo hakuna anaeweza kujua kila kitu. Hata wewe leo kuna vitu ambavyo wewe unavijua, lakini mimi na ujanja wangu wote sivijui. Halikadhalika na mimi kuna vitu navijua lakini wewe na ujanja wako wote hauvijui.

So ndo dunia ilivyo. Ni Mungu pekee ndio mwenye uwezo wa kujua kila kisichojulikana duniani na mbinguni.

Nilishangaa ulipoandika eti umeona magamba ya King Cobra shambani kwako 😂😂😂

Aisee King Cobra uone magamba yake na ubaki salama 😂😂😂

Tuko pamoja mkuu.
Nadhani wapo aina tofauti lakini kuhusu magamba huwa tunayaona mara nyingi na hata kuwua

hawa nao wazungumzia mimi ni weusi tii na wakati mwingine hadi hung'aa kwa weusi wakena anatema mate. hawa kwetu wala sio tishio kitu nilikuwa sijui kwamba anaweza kumla black mamba hapo sikuwahi sikia wala kuona. kupitia bandiko hili nimejifunza mengi. Ahsante sana
 
mkuu kama hatuelewani basi tuachane. ulipo sema kuwa cobra ndo huwa ana mla black mamba nikakujibu sio kweli kwa sababu hata hao wamo humo pori na magamba huwa tunayaona wao ni weusi na wanatabia ku mwaga mate pindi mnapokutana nae. hao kwetu si tishio huwa wanauliwa mara nyingi tu
Ni kweli King cobra anamla koboko ila ukiambiwa kati ya cobra na koboko, Nani ufungiwe nae chumba kimoja, chagua cobra
 
Nadhani wapo aina tofauti lakini kuhusu magamba huwa tunayaona mara nyingi na hata kuwua

hawa nao wazungumzia mimi ni weusi tii na wakati mwingine hadi hung'aa kwa weusi wakena anatema mate. hawa kwetu wala sio tishio kitu nilikuwa sijui kwamba anaweza kumla black mamba hapo sikuwahi sikia wala kuona. kupitia bandiko hili nimejifunza mengi. Ahsante sana
Mozambique spitting Cobra common sana hao!
King Cobra hawarushi mate wanapatikana Asia tu,hakuna NYoka Africa anaweza kumuwinda black mamba kirahisi!
Yuko kwenye top of the food chain ya nyoka
 
Nadhani wapo aina tofauti lakini kuhusu magamba huwa tunayaona mara nyingi na hata kuwua

hawa nao wazungumzia mimi ni weusi tii na wakati mwingine hadi hung'aa kwa weusi wakena anatema mate. hawa kwetu wala sio tishio kitu nilikuwa sijui kwamba anaweza kumla black mamba hapo sikuwahi sikia wala kuona. kupitia bandiko hili nimejifunza mengi. Ahsante sana
Shukran mkuu, ila hao unaosema wewe kuwa umeona magamba yao ni cobra wa kawaida ambao wanapatikana sehem mbali mbali nchini.

King Cobra ni habari nyingine aisee. Kwanza mkorofi, mtemi na haogopi.

Tatizo hapatikani Africa... Kule juu nilikuwa nakutania tu lakini najua kiuhalisia hauwezi kumpata 🙏
 
Shukran mkuu, ila hao unaosema wewe kuwa umeona magamba yao ni cobra wa kawaida ambao wanapatikana sehem mbali mbali nchini.

King Cobra ni habari nyingine aisee. Kwanza mkorofi, mtemi na haogopi.

Tatizo hapatikani Africa... Kule juu nilikuwa nakutania tu lakini najua kiuhalisia hauwezi kumpata 🙏
PAMOJA MKUU. Ndo faida ya kuwa jf
 
Koboko ninamuogopa sana. Niliwahi kutaka kununua shamba, wakati yule mzee ananitembeza tukakutana na Koboko amekufa shambani. Mzee ananiambia huyu tulimuua alikuwa kwenye hiki kichuguu. Kwa theory ya koboko ninavyoifahamu niliahirisha hapo mahala.

Nashauri uwaone wataalam wa nyoka wa vijijini achana na maliasili. Kuna jamaa huwa namuona tiktok amekamata hao koboko wengi sana. Watu wa namna hiyo unaweza kuwatafuta na kuwapa mpunga wamsakue humo shambani at their own risk.
Na wilaya ya Urambo kama ana fahamiana na mtu amuulizie kuna vichwa hadi hao jamaa wa maliasili wanavitumia kuwadaka hao wapuuzi.
 
Koboko ninamuogopa sana. Niliwahi kutaka kununua shamba, wakati yule mzee ananitembeza tukakutana na Koboko amekufa shambani. Mzee ananiambia huyu tulimuua alikuwa kwenye hiki kichuguu. Kwa theory ya koboko ninavyoifahamu niliahirisha hapo mahala.

Nashauri uwaone wataalam wa nyoka wa vijijini achana na maliasili. Kuna jamaa huwa namuona tiktok amekamata hao koboko wengi sana. Watu wa namna hiyo unaweza kuwatafuta na kuwapa mpunga wamsakue humo shambani at their own risk.
Mkuu nawewe umezidi sasa
 
Jf salaam🙏

Ni muda sasa tangu aanze kuonekana huyu nyoka hatari koboko na inasemekana wapo wawili.

Taarifa zilianza kunifikia kutoka Kwa wazee wangu maana huo msitu ukweli sio wangu ni wa mzee ila kaniruhusu kufanya shughuli zozote za kujiingizia kipato.

Mara kadhaa amekuwa akionekana na muda wa usiku kupiga kelele flani Hivi.

Nakumbuka baada ya kupata mapumziko mafupi nilienda kijijni kwa wazee wetu. Nikafika na nikaenda mlimani(msituni) lengo nikufanya research kwa kina Ili niwekeze ufugaji wa nyuki (asali).

Nilimchukua dogo mmoja ambae Huwa anachunga mbuzi wangu tukaenda naye huku akinifotoa picha za kila aina na Kila Rangi.

Mwisho tukafika kwenye mti mzuri wenye kijani kibichi wenye matawi mazuri akanipigia picha za kutosha pale.

Baada ya hapo tukakaa chini ya mti huo kwenye jiwe huku nikipitia picha nilizopigwa na kufuta zile sikuzipenda

Tukiwa hapo tunapiga story ghafla tukasikia kelele za ndenge flani juu ya mti Mimi kelele zile nazijua huwa ni Alert ya hatari fulani wameiona wale ndege.

Kuinua macho juu sikuamini nilichokiona ni yeye koboko mtesa ametulia tulii Wala hatikisikii kama amekufa.

Dogo(muha) kumuona akapanic akaanza mbio nikamwambia simama hapohapo akasimama huku nami nikitoka eneo la tukio hadi kwa dogo.


Nyoka ni mkubwa na anaogopesha na kwa mazingira yale huwezi mshambulia kwa kutumia njia zetu hizi za asili(fimbo)

Maana ni mstuni vinginevyo anakuua ndani ya muda mfupi tu hakuna sehemu ya ku escape asikudhuru.

KUMBUKUMBU ZANGU

Miaka ya nyuma tukiwa wadogo nilishuhudia maiti za Watoto wenzetu watu na ng'ombe 7 zikiwa zimelala Chali (kufa).

Ni baada ya Hawa Watoto kuona huyo nyoka aina ya koboko na kumshambulia ndipo alipowageuka na kuwauma wote wawili na ng'ombe zao zote Saba na zilikufa hapohapo!

Nakumbuka kipindi hicho hicho nikiwa primary mtoto mwingine darasa letu Moja akiwa anaenda kuokota maembe kwenye mti wa mwembe akamuona koboko Kasimama wima naye pasina kujua alianza kumshambulia.

Hapo hapo alimgonga na kufa mama yake alisikia kelele za mwanae akilia Kwa uchungu Kwa sababu ilikuwa mbali na mwembe na mara zote walikuwa wanaenda Watoto kadhaa kuokota maembe pale. ile anatoka akamsaidie alimkuta tiyari kashafariki na nyoka amepanda juu ya mtu flani mfupi.

Ndipo alipo piga yowe kuomba msaada na walifanikiwa kumuua.

Inavyosemekana na Mimi naweza kuwa shahidi wa hili ni kwamba....

Nyoka aina ya black mamba ni wapole kupita kiasi pale anapokuwa katika Hali yake ya kawaida.

Pia anasikia kuliko kawaida anaupeo mkubwa wa kuhisi hatari na hata harufu na hivyo kujiweka tiyari Kwa ajiri ya mapambano.

Akiona mazingira aliyopo sio salama kwakwe kufanya shambulio hujiondokea kabla hujamfikia Wala kumuona.

Lakini pale ukimuona wewe jua kakusubiri na amejiandaa Kwa muda mrefu sana amegojea tu ulianzishe upate unachostahili.

Kwa matukio hayo mawili ambayo siyo ya kusimuliwa na hili langu Mimi mwenyew Tena mwezi 2 tu mwka huu nakubaliana na hili kuwa Hawa nyoka ni wapole na ni hatari.

Tukio la wale watoto wawili na ng'ombe wao. Sisi ndo tulikuwa wa kwanza kumuona yule nyoka na ilikuwa Hivi.....

Siku Moja tunaenda machungani katikati ya njia kulikuwa na mti flan Hivi kama kichaka (ipo miti Ina randa na kutengeneza kichaka kizito)

Tulipitisha mifugo yetu yote salama na sisi wenyewe tukapita salama mtu wa4 ndo akatumbia oneni yule nyoka tukarudi kumtazama asee alikuwa mrefu sana na ametulia kama hajui kinachoendelea...

Tulichokifanya ni kwenda kuwambia wakubwa wetu karibu na eneo lenyewe. Na walipokuja wakamuona na kumtambua walitumbia ondoeni ng'ombe na mifugo yenu hapa tukafanya hivo.

Nao walipoona tumeondoka waliondoka pia bila kumfanya chochote.

Bahati mbaya sana Kwa wenzetu siku chache mbele wao walipo muona tu ujasiri uliwaingia na kuanza kumshambulia huo ndo ulikuwa mwisho wao na ng'ombe wao pia.

Yowe lilipigwa nyoka huyo akauliwa.

Nimekuja kuomba ama kufundishwa njia/mtego Ili nimuue bila kuathiri watu wa maeneo hayo.

Msitu huu nimepanga kufugia nyuki Kwa wingi lakni kinacho niogopesha ni uwepo wa black mamba kwenye eneo hili.

Eneo ni zuri sana Kwa nyuki kwani maji yapo si zaidi ya mita250 na nyuki ni wengi sana hasa kwenye mapango ya miti,mawe na wengine hujitengenezea asali juu ya mti tu.

Najua humu Kuna watu wa maliasili na wataalamu wa maswala haya naombeni namna ya kumuondoa huyu mdudu na nimeambiwa wapo wawili.

Wapo walio waona Kwa nyakati tofauti na maeneo tofauti na usiku hupiga kelele zao Kwa kupokezana wasi wasi wangu zaidi watazaliana na kuongezeka zaidi.

Ahsanteen sana.

View attachment 2945391
Muue kabla yeye hajakuwahi; ni ama zake au zako
 
Back
Top Bottom