Uncle bright
JF-Expert Member
- Feb 9, 2023
- 1,040
- 4,080
Mida ya jioni nikiwa nimetoka kwenye shughuli zangu nilifika nyumbani, nikaenda sebleni kupumzika, paka wangu nae alikuja miguuni kujizungusha zungusha kama kawaida yake nadhani huwa ni salamu yake kisha akarudi zake kupumzika kisehemu chake.
Ghafla nikaona paka anaenda mlango wa kuingia ila sikuona mtu yeyote nikapuuza, baada ya muda naona kama kuna kitu kakizingira anakidadisi kwa muda mrefu huku akiwa anajaribu kukigusa kwa tahadhari, nikapuuza
baada ya muda kidogo naona paka yupo bize anakipiga piga na mkono, kwenda kuangalia karibu nakuta ni vita kali sana baina ya paka na nyoka lakini paka alikuwa kaimudu vema mno, nyoka alikuwa anapigwa sana kucha za kichwani, paka anaweza kumsogelea nyoka ana kwa ana lakini huwezi amini nyoka kwa speed yake ya kudonoa hakuweza hata kugusa sharubu za paka, yani paka ana kasi kubwa mno ya kukwepa kiasi cha kunishangaza.
Sikujua kwamba paka wana uwezo mkubwa kiasi hiki.