Kwanini wanawake na wanaume hawachanganyikani msikitini?

Kwanini wanawake na wanaume hawachanganyikani msikitini?

Uyahudi na Uislamu unafanana kwa kiasi kikubwa(japo sielewi kwa nini Waarabu na Wayahudi huwa wanatwangana muda wote), hata hivyo Ukristo uko mbali sana na Uyahudi pamoja na Uislamu japo zote ni Abrahamic religions.
Tukianza na,
1. Uungu- Sehemu kubwa ya Ukristo wanaamini mungu wa nafsi tatu ambapo kwa Waislamu na Wayahudi wanaona ni upotovu.
2. Yesu Kristo- Ukristo umejengwa juu ya msingi wa kifo na kufufuka kwa Yesu Kristo, Waislamu wanasema Yesu hajafa na Wayahudi wanasema Masihi Kristo hajaja kabisa
3. Vyakula- Wakristo tofauti na Wasabato hawana Sheria za vyakula,
4.Ibada-Wakristo hawana Sheria za mwilini kuhusu Ibada kama za kutawadha, kusujudu n.k kama ilivyo kwa Waislamu na Wayahudi
5.Ndoa- Ukristo hauruhusu ndoa za mitaala
hapo sasa umenielewa kabisa
 
Hakuna sheria za Kikristu zilivyo hivyo. Hapo itakuwa umesoma vitabu vya historia vilivyojaa Mila ,tamaduni na sheria za kiyahudi za again la kale. Hapa ndio watu wengi Huwa wanakwama . Maelekezo sahihi soma agano la kale kwani Yesu alikuwa kutenganisha mambo ya kitamaduni yaliyokuwepo kwenye agano la kale na ndio maana wayahudi walimuua kwa sababu aliwakosoa kwenye masheria kama haya. Agano kipya ndio mpango.mzima hata kitimoto na bia lakini tunashushia saaafi maana alikosoa zile Mila za walawi za kutoka kula mdudu na lutakasa vyakula vyote
Nasikitikita kukwambia kuwa maandiko haya hapa chini ni agano la kale.. 😀 😀 😀 😀 😀
tuanze na 1 Wakoritho 14:34-38

Screenshot 2026-04-08 152311.png


agano la kale hili??

okay sawa huenda paulo mkono Uliteleza mpaka akatoa amri hii ya ukandamizaji na akasema ni amri aliyopokea kutoka kwa Mungu vipi hapa? 1 Timotheo 2:8-14

Screenshot 2026-04-08 151949.png


Tena kabisa anasisitiza kwenye mstari wa 12 simpi ruhusa mwanmke kumtawala mwanaume wala kumfundisha.. umeona??
au nalo hili ni agano la kale?

vipi kuhusu haya hapa chini?

Waefeso 5:22-24: "Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana. Kwa maana mume ni kichwa cha mke, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa... Basi kama vile Kanisa limtiivyo Kristo, vivyo hivyo wake na wawatii waume zao katika kila jambo."

Wakolosai 3:18: "Enyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana."

Tito 2:4-5: "...ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao... watii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe."

1 Petro 3:7: "Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kidhaifu..."

1 Wakorintho 11:7-9: "Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunika kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu; lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume. Maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke katika mwanamume. Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume."


mkuu haya mafungu ni ya Agano la kale??
 
Kama unajifunika kwa hijab, niqab au burka ina maanisha sio rahisi umbile la mwili wako wako kuonekana kwa hiyo hata matamanio ya wanaume yanapungua na inakuwa rahisi kujichanganya bila kuamsha hisia, japo ajabu pia ni kwamba kuna watu kama min -me anasema wanaovaa hivyo ndio huwa anawatamani zaidi!
Mno bwashee
 
Nimezaliwa huko hiyo dini imejaa vitisho ubinafsi na ukandamizaji hasa kwa jinsia ke
Tabia za hovyo na za kishenzi za familia yako,usifanye kua ndio ikawa kua ndio tabia za watu wote wa dini hiyo,usihukumu dini yote kwa tabia za familia yako,

Yani hicho kifamilia chako cha hovyo ndio kikufanye uhukumu watu wote wa dini hiyo Dunia nzima?
 
Mkuu swala hilo linaitwa Ikhtilat kwa lugha ya kiarabu..
sasa nini faida yake:

1. Kulinda Unyenyekevu (Khushui')
Unajua swala ya kiislamu inavyofanyika kuna kugusana baina ya vidole vya miguu na kuna kulinganisha mabega na zaidi kuna rukuu na sigda inayomtaka muumini kuinama na kuinuka na kuinamisha kichwa chini jambo ambalo kama utaswali na mwanamke pembeni linaweza kuondoa utulivu kwa kuamka matamanio na kukuondoa kwenye swala (unajua tena wenzetu wameumbwa na magnnetism)

2. Kuepuka Vishawishi (Fitna)
Uislamu unasisitiza kuzuia mazingira yanayoweza kuleta vishawishi kati ya jinsia mbili katika maeneo ya ibada. Kwa kutenga sehemu za kuswali, jamii inajenga mazingira ya heshima ambapo kila mmoja anaweza kuabudu kwa uhuru.

3. Sunnah
Wakati wa Mtume Muhammad (S.A.W), wanawake waliswali msikitini lakini walikuwa nyuma ya safu za wanaume. Mtume alisema kuwa safu bora kwa wanaume ni za mbele, na safu bora kwa wanawake (katika mazingira ya pamoja) ni za nyuma. Baadaye, kadiri idadi ya watu ilivyoongezeka, kuta au vyumba maalum viliwekwa kwa ajili ya urahisi na faragha zaidi.

SASA mkuu nakurudishia swali kuwa je kwenye biblia au tamaduni za zmani hakuna hiki kitu namaanisha kabla ya uislamu yaani hiki kitu ni kipya ???

hapana sio ktu kipya
Katika nyakati za Wana wa israel na hata baada ya hapo, Hekalu la Yerusalemu lilikuwa na sehemu maalum iitwayo "Ezrat Nashim (עֶזְרַת נָשִׁים)" Yaani Court of the Women.

Wanawake hawakuruhusiwa kuingia katika maeneo ya ndani yaliyotengwa kwa wanaume wa Kiisraeli au makuhani. Huu ulikuwa mgawanyo wa wazi wa kijinsia katika ibada.

Japo kwenye Katika Hekalu la Pili la Yerusalemu (Hekalu la Herode), hili lilikuwa eneo la nje ambapo Wayahudi wote (wanaume kwa wanawake) waliruhusiwa kuingia kwa ajili ya ibada za kawaida na kusikiliza mafundisho. ila wanawake hawakuruhusiwa kupita eneo hili kwenda ndani zaidi kuelekea madhabahuni (eneo lililoitwa Ezrat Yisrael ambalo lilikuwa maalum kwa wanaume tu).

Hadi leo, katika madhehebu ya kiorthodox ya Kiyahudi (ambayo yanafuata sheria za kale za Torati), wanaume na wanawake hukaa sehemu tofauti, mara nyingi zikitenganishwa na ukuta au pazia liitwalo Mechitza.

katika ukristo kwenye Mila za Kale
Kwa karne nyingi, katika makanisa mengi ya kale (ikiwemo baadhi ya makanisa ya Orthodox na Katoliki ya Mashariki), wanaume walikaa upande mmoja wa kanisa na wanawake upande mwingine.

Ingawa Biblia haisemi waziwazi ila inasisitiza juu ya utaratibu na staha. Kwa mfano, katika 1 Wakorintho 14:34-35 na 1 Timotheo 2:11-12, kuna maelekezo yanayoweka mipaka ya ushiriki wa wanawake katika mazingira fulani ya ibada ya hadhara ili kudumisha utaratibu.

Ki ufupi Mgawanyo wa jinsia si jambo la kiislamu pekeeni utaratibu uliokuwepo katika dini zote za Ibrahimu (Uyahudi, Ukristo, na Uislamu) kwa lengo la kudumisha staha na heshima katika nyumba za ibada, ingawa Ukristo wa kisasa katika madhehebu mengi umeacha utaratibu huo.
Yoda umepata majibu yako sasa
 
Imagine umeinama kuswali,mbele yako unamuona mwanadada mashaallah kainama tako lote kaacha nje,si utawazia doggie style? Ile namna yako ya kuswali kwa kupiga magoti na kusujudu ni mbaya kuwa wote chumba kimoja.
 
Tabia za hovyo na za kishenzi za familia yako,usifanye kua ndio ikawa kua ndio tabia za watu wote wa dini hiyo,usihukumu dini yote kwa tabia za familia yako,

Yani hicho kifamilia chako cha hovyo ndio kikufanye uhukumu watu wote wa dini hiyo Dunia nzima?
Platinum member 😳
Kwanini una hasira kali just relax bro👍
Maoni yangu sio sheria ishi humo mkuu🤝
 
Back
Top Bottom