Kwanini wanawake na wanaume hawachanganyikani msikitini?

Kwanini wanawake na wanaume hawachanganyikani msikitini?

wanakuwepo mkuu , hata kama ni kwa uchache
Kuna mtu kasema wanawake wanaruhusiwa kuswalia hata nyumbani tu sio lazima waende msikitini ndio maana misikiti mingine haina sehemu za wanawake,
Ni kweli?
 
Mkuu swala hilo linaitwa Ikhtilat kwa lugha ya kiarabu..
sasa nini faida yake:

1. Kulinda Unyenyekevu (Khushui')
Unajua swala ya kiislamu inavyofanyika kuna kugusana baina ya vidole vya miguu na kuna kulinganisha mabega na zaidi kuna rukuu na sigda inayomtaka muumini kuinama na kuinuka na kuinamisha kichwa chini jambo ambalo kama utaswali na mwanamke pembeni linaweza kuondoa utulivu kwa kuamka matamanio na kukuondoa kwenye swala (unajua tena wenzetu wameumbwa na magnnetism)

2. Kuepuka Vishawishi (Fitna)
Uislamu unasisitiza kuzuia mazingira yanayoweza kuleta vishawishi kati ya jinsia mbili katika maeneo ya ibada. Kwa kutenga sehemu za kuswali, jamii inajenga mazingira ya heshima ambapo kila mmoja anaweza kuabudu kwa uhuru.

3. Sunnah
Wakati wa Mtume Muhammad (S.A.W), wanawake waliswali msikitini lakini walikuwa nyuma ya safu za wanaume. Mtume alisema kuwa safu bora kwa wanaume ni za mbele, na safu bora kwa wanawake (katika mazingira ya pamoja) ni za nyuma. Baadaye, kadiri idadi ya watu ilivyoongezeka, kuta au vyumba maalum viliwekwa kwa ajili ya urahisi na faragha zaidi.

SASA mkuu nakurudishia swali kuwa je kwenye biblia au tamaduni za zmani hakuna hiki kitu namaanisha kabla ya uislamu yaani hiki kitu ni kipya ???

hapana sio ktu kipya
Katika nyakati za Wana wa israel na hata baada ya hapo, Hekalu la Yerusalemu lilikuwa na sehemu maalum iitwayo "Ezrat Nashim (עֶזְרַת נָשִׁים)" Yaani Court of the Women.

Wanawake hawakuruhusiwa kuingia katika maeneo ya ndani yaliyotengwa kwa wanaume wa Kiisraeli au makuhani. Huu ulikuwa mgawanyo wa wazi wa kijinsia katika ibada.

Japo kwenye Katika Hekalu la Pili la Yerusalemu (Hekalu la Herode), hili lilikuwa eneo la nje ambapo Wayahudi wote (wanaume kwa wanawake) waliruhusiwa kuingia kwa ajili ya ibada za kawaida na kusikiliza mafundisho. ila wanawake hawakuruhusiwa kupita eneo hili kwenda ndani zaidi kuelekea madhabahuni (eneo lililoitwa Ezrat Yisrael ambalo lilikuwa maalum kwa wanaume tu).

Hadi leo, katika madhehebu ya kiorthodox ya Kiyahudi (ambayo yanafuata sheria za kale za Torati), wanaume na wanawake hukaa sehemu tofauti, mara nyingi zikitenganishwa na ukuta au pazia liitwalo Mechitza.

katika ukristo kwenye Mila za Kale
Kwa karne nyingi, katika makanisa mengi ya kale (ikiwemo baadhi ya makanisa ya Orthodox na Katoliki ya Mashariki), wanaume walikaa upande mmoja wa kanisa na wanawake upande mwingine.

Ingawa Biblia haisemi waziwazi ila inasisitiza juu ya utaratibu na staha. Kwa mfano, katika 1 Wakorintho 14:34-35 na 1 Timotheo 2:11-12, kuna maelekezo yanayoweka mipaka ya ushiriki wa wanawake katika mazingira fulani ya ibada ya hadhara ili kudumisha utaratibu.

Ki ufupi Mgawanyo wa jinsia si jambo la kiislamu pekeeni utaratibu uliokuwepo katika dini zote za Ibrahimu (Uyahudi, Ukristo, na Uislamu) kwa lengo la kudumisha staha na heshima katika nyumba za ibada, ingawa Ukristo wa kisasa katika madhehebu mengi umeacha utaratibu huo.
Maelezo ni mazuri ila yanaeleweka sana kama utaayaweka katika muktadha wa kibaiolojia lakini yanaacha maswali lukuki katika muktadha wa uthabiti wa imani katika kumudu majaribu.

Kwenye ishu ya kumudu majaribu kwa njia ya imani huwezi kuweka excuse ya kwamba tunagusana, kusema hivyo ni kuthibitisha kwamba imani yako ni ya kutetereka.
 
Ni kweli Kuna makanisa mengi tu wanawake wanakaa upande tofauti na wanaume, nilikuwa nategemea jambo kama hili pia misikiti badala ya wanawake kutengewa kwenye chumba tofauti kabisa.

Hata hivyo mfano wako wa hekalu sio sahihi kwa sababu Ukristo na Uyahudi ni dini tofauti kabisa.
ukristo umetoka kwenye Uyahudi au umesahau mkuu hata biblia imetoka kwa wayahdi kasoro agano jipya..
ni sawa na wamormoni wakatae kuwa hawajatoka kwa wakristo
 
Halafu kwa nini wanaume ndio huswali sana na kujazana misikitini, ina maana wanawake allah hawahitaji wamswalie mtume? Wazee wanajazana misikitini kuswali swala zote utadhani hawana shughuli za kufanya, ni kuswali tu!
 
Hakika dini zina contradictions nyingi na kubwa sana, ila ndio hivyo binadamu nao wan cognitive dissonance ya hali ya juu sana.
Mimi nawaelewa watu wa dini wanapojitenga na wanawake kwa kutoa sababu za kibailojia na kimwili, ni kweli hizo sababu ni za msingi na zinaelezeka kisayansi.

Kwa bahati mbaya wao walipewa task ya kuepuka majaribu ili waweze kuiona pepo. Maana yake hizi sababu hazikutakiwa kuwa kikwazo cha kumfanya Muumini mwenye imani ya kweli aharibu swala yake.
 
Halafu kwa nini wanaume ndio huswali sana na kujazana misikitini, ina maana wanawake allah hawahitaji wamswalie mtume? Wazee wanajazana misikitini kuswali swala zote utadhani hawana shughuli za kufanya, ni kuswali tu!
Na wewe huna kazi za kufanya mpaka unawafuatilia wanaume wanaoenda Msikitini kuswali swala zote?

Unatafuta bwana?

Kwenye Uislamu,Mwanamke hana ulazima wa kwenda msikitini,Mwanamke ni bora zaidi kama atasali Nyumbani kuliko Msikitini,uislamu ndio umeamrisha hivyo.
 
Wanawake wanaweza kuswali chumba kimoja na wanaume ila wataswali nyuma yao
Kuna maeneo kama Msikiti wa Makkah wanawake na wanaume wanaswali eneo moja ila wanatenganishwa tu na na barriers kuonesha mipaka yao
Nia ni kuleta modesty na kutoleta temptation na distraction wakati wa swala

Ukienda mbali zaidi, mafundisho ya dini hayaruhusu mchanganyiko usio wa lazima kati ya wanawake na wanaume ambao hawana mahusiano ya kindugu au ukaribu (mahrim)

Kuna baadhi ya nchi hasa za kiarabu ambazo kwenye public transport kama taxi za mchangio,( kwa Tz ni kama ilivyo bajaj) bus, train wanatenganishwa, kwenye foleni za banks pia wanawake na wanaume wana foleni tofauti, kwenye public schools na colleges pia kuna vyuo au madarasa tofauti
Hata nyumba za waarabu wengi kuna sebule 2, moja ya wanawake na nyingine ya wanaume

Kwa upande mwengine, Makanisa ya Eastern Orthodox mf Ethiopia wanafanya hivyo pia na hata Dar kuna kanisa la Father Nkwera wanafanya hivyo, nimeshuhudia kwa macho yangu wanawake na wanaume wanatenganishwa maeneo
Kutenganisha wanawake na wanaume kwenye dalaladala kwa bongo ingefaa sana kuwadhibiti wanaume Dunga Dunga wanaombambia wanawake makalioni, ila kwenye sebule tofauti ya wanawake na wanaume kwenye nyumba moja sio mpango.
 
Binafsi nadhani waislam wapo sahihi kabisa kutenganisha wanaume na wanawake, kwanza ni ile nature ya ibada yao, kuinama na kuinuka multiple times wakati wa kufanya ibada kunaweza kuwa kigezo cha kwanza kabisa, lakini pia kuondoa vishawishi vya macho. Huku kwa wakristo hata humu watu wengi wamekiri kuondolewa utulivu na usikivu kwa muingiliano wa hizi jinsi mbili.
Sasa nini maana ya wanawake wa Kiislamu kuvaa hijabu, niqab au burka??
 
Waarabu wali copy sheria za kimila za kiyahudi za zamani zilizoitwa ( MOSEIC DRACONIAN LAWS) Ambazo kwa nyakati hizo jamii duniani zilikuwa zinazifuata ila zilikuja kuonekana ni sheria kandamizi za kijinga

Kwa sheria hizo mwanamke anaonekana kama sio binaadamu wa kawaida Bali ni kifaa kazi na burudani tuu na walimuweka kwenye daraja la kifaa kazi kinacho zungumza ( Instrument um voccale) Akiwa kwenye kundi la vigaa kazi vingine kama ngombe ( instrumentum semi- voccale) na vile visivyoongea kabisa kama majembe , tractor nk ( instrumentum muutu)

🔹 Hivyo kwa Mila za kiarabu katoto kadogo Cha Kiume kana haki na nafasi kuliko mtu mzima mwanamke

🔹 Mwanamke wa kiarabu na miafrika inayojifanya na menyewe ni miarabu humgandamiza mwanamke huku ikimpaka mafuta kwa mgongo wa chupa kuwa eti wanathaminiwa.
 
Uislamu ulianza kwa vita. Warlord Mohammed na wanamgambo wake wasingeweza kujichanganya na wanawake, wasije wakaona matako ya wake zao wakawa distracted kwenda kujitoa muhanga.

Nadharia ya pili, Mohamed alikuwa na tamaa sana ya wanawake..Kumbuka alimuoa mtalaka wa Zayd, kijana wake! Sasa imagine angekuwa anajichanganya na wake wa wanamgambo wake wanabinua matako mbele yake wakisujudu!
Itakuwa waliona watenge wake zao kuwalinda dhidi ya nyege za bwana mkubwa.
 
Halafu kwa nini wanaume ndio huswali sana na kujazana misikitini, ina maana wanawake allah hawahitaji wamswalie mtume? Wazee wanajazana misikitini kuswali swala zote utadhani hawana shughuli za kufanya, ni kuswali tu!
Nina swali kwenye maelezo yako, ina maana watu wanamswalia mtume au wanamwaslia Mwenyezi Mungu? Huwa hii statement siielewi!!
 
Hivi kwa muktadha wa dini, kipimo cha imani si ndio majaribu?

Hivi mtu huitwa mshindi kwasababu amemshinda mpinzani au kwasababu ameepushiwa mshindani?

Utasemaje una imani thabiti ikiwa ni muoga kuya-face majaribu?

Hii inaenda sambamba kwa moja kwa wale wanaomini funga zao zinaweza kuharibika ikiwa tu watu wengine watakuwa huru kula mbele yao.
Huo ni mtazamo batili . Majaribu yanayokujia na sio ya kutafuta makusudi

Kuepuka fitina ni bora kuliko kuifuata makusudi , sawa mtu uende kimboka au club kujipima Imani huo ni uchizi .

Hata wanajeshi kufa vitani ni sifa ya ushujaa lakini kamwe hawaitafuti vita kwa makusudi kisa kujipima ndio maana nchi nyingi zina majeshi na silaha ambazo hawajawahi kutumia kwa miaka mingi na wanajeshi wengine wengi wanaokufa na kustaafu bila kwenda vitani.
 
Kuna mtu kasema wanawake wanaruhusiwa kuswalia hata nyumbani tu sio lazima waende msikitini ndio maana misikiti mingine haina sehemu za wanawake,
Ni kweli?
naam hilo nalo lipo.

hapo middle east ukizingatia na muda wa wakati huo imani zote hizo mwanamke alikua na masharti kidogo, unaweza sema kazi za nyumbani, watoto na familia kiujumla ziende
 
Sasa nini maana ya wanawake wa Kiislamu kuvaa hijabu, niqab au burka??
Kujistiri, kutikukaa uchi. Ji utaratibu tu mkuu, na kila imani inakuwa na utaratibu wake.

Hivi wewe kama ni mkristo, unapenda namna baadhi ya wanawake wa kikristo wanavyovaa wakienda ibadani?
 
Binafsi nadhani waislam wapo sahihi kabisa kutenganisha wanaume na wanawake, kwanza ni ile nature ya ibada yao, kuinama na kuinuka multiple times wakati wa kufanya ibada kunaweza kuwa kigezo cha kwanza kabisa, lakini pia kuondoa vishawishi vya macho. Huku kwa wakristo hata humu watu wengi wamekiri kuondolewa utulivu na usikivu kwa muingiliano wa hizi jinsi mbili.
Wakristo wengine wana Mademu mpaka Kanisani sababu ya Mchanganyiko .
 
Sasa nini maana ya wanawake wa Kiislamu kuvaa hijabu, niqab au burka??
Reasoning capacity yako ni ndogo sana haswa kwenye mambo ya kidini.

Mwanaume kinamvutia sura tu kwa Mwanamke ?

Hapa Jf watu wanatongoza avatar fake bila kujua sura au jina , wengine kisa jina zuri romantic nk anatongoza bila kumjua mtu .

Mwanamke ni fitna hata awe vipi ukimchanganisha na Mwanaume ni kosa anaweza kumshawishi hata avue burka na akavua .

Sawa useme Leo watu walale bila neti kisa dawa za Malaria zipo dukani.
 
Kujistiri, kutikukaa uchi. Ji utaratibu tu mkuu, na kila imani inakuwa na utaratibu wake.

Hivi wewe kama ni mkristo, unapenda namna baadhi ya wanawake wa kikristo wanavyovaa wakienda ibadani?
Kama unajifunika kwa hijab, niqab au burka ina maanisha sio rahisi umbile la mwili wako wako kuonekana kwa hiyo hata matamanio ya wanaume yanapungua na inakuwa rahisi kujichanganya bila kuamsha hisia, japo ajabu pia ni kwamba kuna watu kama min -me anasema wanaovaa hivyo ndio huwa anawatamani zaidi!
 
Back
Top Bottom