Kwanini wanawake na wanaume hawachanganyikani msikitini?

Kwanini wanawake na wanaume hawachanganyikani msikitini?

Chukua mfano wa mjane mwenye senti chache.
Hapo ndiyo utajua kwenye sinagogi wanaume na wanawake waliabudu pamoja na walikuwa wanaonana.
hamna haja ya maelezo mengi. ni sheria tu za kibinadamu.
Mkuu unaifahamu Ramani ya Sinagogi au ramani ya Hekalu??
tuanze hapo kwanza..

ngoja nikuweke sawa kabisa ...
Mjane huyo alikuwa ndani ya lile eneo la "Ezrat Nashim" (Uanja wa Wanawake) kama nilivyoeleza awali..

kwenye uwanja huu wa Ezrat Nashim kulikuwa na sanduku 13 za sadaka ambazo zilikuwa zinaitwa Shofarot na kama nilivyosema masanduku haya yaliwekwa ndani ya Uwanja wa Wanawake (Ezrat Nashim), ina yaliwekwa hapa kwa sababu lilikuwa eneo ambalo kila Myahudi mwanamume au mwanamke alikuwa na ruhusa ya kuingia yaani wote walikuwa na acces nalo.

kwahyo Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamekaa hapo, na hapo ndipo walipowaona watu wa jinsia zote wakipita kutoa sadaka.,,

unaweza ukauliza kwanini kama ulikuwa uwanja wa wanawake yaaani Ezrat Nashim... waliweka masanduku ya sadaka na wanaume waliingia??

kwanza kabisa eneo hili Linaitwa Ezrat Nashim (Uwanja wa Wanawake) si kwa sababu wanaume walikatazwa, bali kwa sababu hicho ndicho kilikuwa kiwango cha mwisho kabisa ambacho mwanamke aliruhusiwa kuingia ndani ya Hekalu.
kwahyo Wanaume Walipita katika uwanja huu ili kuelekea sehemu za ndani zaidi (kama Uwanja wa Waisraeli na Uwanja wa Makuhani).
ila Wanawake Huu ulikuwa uwanja wao mkuu wa ibada hawakuruhusiwa kwenda mbele zaidi ya hapo kuelekea Madhabahuni.

Sijui kama umenielewa Mkuu? ukitaka ufafanuzi zaidi sema turudi kwenye vitabu vya Musa torati kabisa nikuonyeshe zaidi..

swali jingine kwanini Masanduku 13 ya Sadaka (Shofarot) yaliwekwa hapa?
Masanduku haya yaliwekwa katika eneo hili kwa sababu ya urahisi wa kila mtu kuyafikia Kama yangekuwa ndani zaidi (kwenye Ua wa Waisraeli), wanawake wasingeweza kutoa sadaka zao, Kwa kuyaweka kwenye Ua wa Wanawake, ilimaanisha mwanamume tajiri, mwanamume maskini, mwanamke mjane, na vijana wote wangeweza kufika na kutumbukiza sadaka zao.

ngoja nikupe mfano mdogo tu..
Hebu piga picha ya uwanja mkubwa wa Hospitali ambapo kila mtu mgonjwa na asiye mgonjwa anaruhusiwa kuwepo. Lakini, kuna mlango wa kuelekea ofisi za daktari, na wodini ambapo ni wagonjwa tu na wahudumu wa afya na madaktari ndio wanaruhusiwa kuingia, Ule uwanja wa nje ndio ungekuwa "Ezrat Nashim." Watu wote wangemuona mjane akitoa sadaka yake kwa sababu sote tuko uwanjani.
Lakini punde tu ibada za ndani (kama kutoa dhabihu ya mnyama madhabahuni) zilipoanza, wanaume waliondoka uwanjani hapo na kuingia ndani zaidi, huku wanawake wakibaki uwanjani hapo kuomba....
 
Hivi wewe kama ni mkristo, unapenda namna baadhi ya wanawake wa kikristo wanavyovaa wakienda ibadani?
Mimi napenda zaidi wanawake wakivaa skirts, suruali au nguo za size zinazowakaa na kuwatoshea vizuri. Iwe kazini, kanisani, msibani, msikitini n.k
Ambacho huwa kinanishangaza tu ni wanaovaa sketi fupi halafu wanaanza kuivutavuta chini au wanaovaa manguo yaliyowazidia wanaanza kutumia mikono tena kushikilia.
 
Waarabu wali copy sheria za kimila za kiyahudi za zamani zilizoitwa ( MOSEIC DRACONIAN LAWS) Ambazo kwa nyakati hizo jamii duniani zilikuwa zinazifuata ila zilikuja kuonekana ni sheria kandamizi za kijinga

Kwa sheria hizo mwanamke anaonekana kama sio binaadamu wa kawaida Bali ni kifaa kazi na burudani tuu na walimuweka kwenye daraja la kifaa kazi kinacho zungumza ( Instrument um voccale) Akiwa kwenye kundi la vigaa kazi vingine kama ngombe ( instrumentum semi- voccale) na vile visivyoongea kabisa kama majembe , tractor nk ( instrumentum muutu)

🔹 Hivyo kwa Mila za kiarabu katoto kadogo Cha Kiume kana haki na nafasi kuliko mtu mzima mwanamke

🔹 Mwanamke wa kiarabu na miafrika inayojifanya na menyewe ni miarabu humgandamiza mwanamke huku ikimpaka mafuta kwa mgongo wa chupa kuwa eti wanathaminiwa.
lakini mkuu hta sheria za Kikristo ziko hivyo... so Kiufupu dini zote sheria zake ni za Ajabu na zinakandamiza
 
Kama unajifunika kwa hijab, niqab au burka ina maanisha sio rahisi umbile la mwili wako wako kuonekana kwa hiyo hata matamanio ya wanaume yanapungua na inakuwa rahisi kujichanganya bila kuamsha hisia, japo ajabu pia ni kwamba kuna watu kama min -me anasema wanaovaa hivyo ndio huwa anawatamani zaidi!
Sasa unaona, mtu anaweza kujikanda nguo na bado watu wakamtamani. Njia rahisi ni kutengana, ili ibada iwe na utulivu.

Kama wewe ni mkristo niambie, ni sawa baadhi ya wanawake wanavyovaa makanisani?
 
Sasa unaona, mtu anaweza kujikanda nguo na bado watu wakamtamani. Njia rahisi ni kutengana, ili ibada iwe na utulivu.

Kama wewe ni mkristo niambie, ni sawa baadhi ya wanawake wanavyovaa makanisani?
Sijawahi kuona shida yoyote wanawake wanavyovyaa kanisani, I'm not a zealot.
 
Sijawahi kuona shida yoyote wanawake wanavyovyaa kanisani, I'm not a zealot.
Kwamba zile skirt fupi wanazopambana kuvutavuta na yale magauni yaliyochanwa hadi upaja unaonekana kwako ni sawa ibadani?
 
Reasoning capacity yako ni ndogo sana haswa kwenye mambo ya kidini.

Mwanaume kinamvutia sura tu kwa Mwanamke ?

Hapa Jf watu wanatongoza avatar fake bila kujua sura au jina , wengine kisa jina zuri romantic nk anatongoza bila kumjua mtu .

Mwanamke ni fitna hata awe vipi ukimchanganisha na Mwanaume ni kosa anaweza kumshawishi hata avue burka na akavua .

Sawa useme Leo watu walale bila neti kisa dawa za Malaria zipo dukani.
Kama Kuna chanjo ya Malaria hakuna haja ya kulala na neti labda kwa ajili kuondoa usumbufu wa kelele za mbu, pia ikipatikana dawa au chanjo ya ukimwi condoms zitakuwa hazina maana tena.

Halafu sasa kama wanaume wanavutiwa na kutamani chochote kwa mwanamke ina maana gani kuvaa hijabu, niqab au burqa?? Labda mseme hayo mavazi sio kwa ajili ya kuondoa au kupunguza matamanio ya wanaume bali ni sheria ya Allah tu. Wanawake wa zamani kabla ya Uislamu walivaa hivyo kama ishara ya kutawaliwa na mwanaume pamoja utiifu/unyoofu kwa mungu/miungu au social status na sio kwa sababu za matamanio ya wanaume.
 
Huo ni mtazamo batili . Majaribu yanayokujia na sio ya kutafuta makusudi

Kuepuka fitina ni bora kuliko kuifuata makusudi , sawa mtu uende kimboka au club kujipima Imani huo ni uchizi .

Hata wanajeshi kufa vitani ni sifa ya ushujaa lakini kamwe hawaitafuti vita kwa makusudi kisa kujipima ndio maana nchi nyingi zina majeshi na silaha ambazo hawajawahi kutumia kwa miaka mingi na wanajeshi wengine wengi wanaokufa na kustaafu bila kwenda vitani.
Kwa mujibu wa dini, Majaribu huletwa na Mungu, Shetani, watu hadi vitu.

Kwa hiyo tunategemea kusiwepo na exception ya kuchagua aina fulani tu ya majaribu ambayo unaona eidha yanakupa urahisi wa kuyashinda au kwa interest binafsi.
 
Kwamba zile skirt fupi wanazopambana kuvutavuta na yale magauni yaliyochanwa hadi upaja unaonekana kwako ni sawa ibadani?
Hakuna tatizo mkuu, Naelewa shida ni kwa sababu hujazoea kuona upaja mkuu ndio maana unataharuki na kupata shida😁, ukikaa nchi/jamii watu wanaona upaja kila siku na kila mahali wala hutapata shida na kutaharuki.
 
Kwamba zile skirt fupi wanazopambana kuvutavuta na yale magauni yaliyochanwa hadi upaja unaonekana kwako ni sawa ibadani?
Hoja zenu ziimejikita kwenye kuona

Ni kama lile katazo haliwahusu vipofu

Au vipofu ni halali kushea ukumbi wa kuswalia na wanawake kwasababu hawawezi kuona hayo mapaja?
 
Hakuna tatizo mkuu, Naelewa shida ni kwa sababu hujazoea kuona upaja mkuu ndio maana unataharuki na kupata shida😁, ukikaa nchi/jamii watu wanaona upaja kila siku na kila mahali wala hutapata shida na kutaharuki.
Nimeishi na hizo jamii mkuu, ngozi ya wazungu na sisi ni tofauti kabisa. Mwanamke wa kiafrika akiweka upaja nje lazima uangalie mara mbili, mzungu wala hana mshawasha😀
 
Hoja zenu ziimejikita kwenye kuona

Ni kama lile katazo haliwahusu vipofu

Au vipofu ni halali kushea ukumbi wa kuswalia na wanawake kwasababu hawawezi kuona hayo mapaja?
Na hapo ndipo mzizi ulipo mkuu, kuona na kupata mfadhaiko, kutoka kwenye dhana nzima ya kufanya ibada na Mungu wako.
 
kabisa uko sawa ila sijaona utofauti wa uislamu na ukristo pengine ungeniambia ningejua..
mimi ninachokiona uyahudi na uislamu unafanana (na niliwahi kuandika nyuzi pia humu) kuliko uyahudi na ukristo
Uyahudi na Uislamu unafanana kwa kiasi kikubwa(japo sielewi kwa nini Waarabu na Wayahudi huwa wanatwangana muda wote), hata hivyo Ukristo uko mbali sana na Uyahudi pamoja na Uislamu japo zote ni Abrahamic religions.
Tukianza na,
1. Uungu- Sehemu kubwa ya Ukristo wanaamini mungu wa nafsi tatu ambapo kwa Waislamu na Wayahudi wanaona ni upotovu.
2. Yesu Kristo- Ukristo umejengwa juu ya msingi wa kifo na kufufuka kwa Yesu Kristo, Waislamu wanasema Yesu hajafa na Wayahudi wanasema Masihi Kristo hajaja kabisa
3. Vyakula- Wakristo tofauti na Wasabato hawana Sheria za vyakula,
4.Ibada-Wakristo hawana Sheria za mwilini kuhusu Ibada kama za kutawadha, kusujudu n.k kama ilivyo kwa Waislamu na Wayahudi
5.Ndoa- Ukristo hauruhusu ndoa za mitaala
 
lakini mkuu hta sheria za Kikristo ziko hivyo... so Kiufupu dini zote sheria zake ni za Ajabu na zinakandamiza
Hakuna sheria za Kikristu zilivyo hivyo. Hapo itakuwa umesoma vitabu vya historia vilivyojaa Mila ,tamaduni na sheria za kiyahudi za again la kale. Hapa ndio watu wengi Huwa wanakwama . Maelekezo sahihi soma agano la kale kwani Yesu alikuwa kutenganisha mambo ya kitamaduni yaliyokuwepo kwenye agano la kale na ndio maana wayahudi walimuua kwa sababu aliwakosoa kwenye masheria kama haya. Agano kipya ndio mpango.mzima hata kitimoto na bia lakini tunashushia saaafi maana alikosoa zile Mila za walawi za kutoka kula mdudu na lutakasa vyakula vyote
 
Nimeishi na hizo jamii mkuu, ngozi ya wazungu na sisi ni tofauti kabisa. Mwanamke wa kiafrika akiweka upaja nje lazima uangalie mara mbili, mzungu wala hana mshawasha😀
Black Americans, Wakenya, Wazambia, Waganda, Wazulu na jamii nyingine nyingi tu wanawake wanavaa nguo za kuonyesha upaja na wala hakuna tatizo. Tanzania tumeathiriwa zaidi na utamaduni wa mavazi ya kiarabu/kiswahili ndio maana tunababaika na kutaharuki na mini skirts, kaptula na suruali kwa wanawake.
 
Ni kwa nini katika Uislamu wanawake na wanaume hawachanganyikani katika chumba kimoja msikitini?
Uliona kilichowakuta kule wanapompiga mawe shetani kilichowakuta? Maana kule wote wanakua uchi na kujifunika mashuka meupe unakumbuka wanawake walipojichanganya na wanaume kilichowakuta? Km unakumbuka vizuri unakumbuka nini kilichowapata? Sasa hicho kilichowapata ndicho kinachowafanya watenganishwe na wanaume
 
Back
Top Bottom