Kwanini wanawake na wanaume hawachanganyikani msikitini?

Kwanini wanawake na wanaume hawachanganyikani msikitini?

Kama hakuna Aya au hadithi ni wao tu wamejiongeza sasa kwa nini badala ya kuwa na vyumba tofauti isiwe ni chumba kimoja tu ila kila jinsia inakaa upande wake?
Zamani ilifanyika hivyo na hata baadhi ya miskiti inafanyika hivyo...

unajua watu wasichokijua unapotaja uislamu unataka madhehebu mengi sana..Tofauti na mawazo ya watu walio nje
 
Matatizo yataanza pale mwanamke akiinama kuswali, mana hakuna mwanaume atakayekaa mbele 😎
Wanajaa chumba kimoja, wanaume kushoto na wanawake kulia.
 
Mkuu swala hilo linaitwa Ikhtilat kwa lugha ya kiarabu..
sasa nini faida yake:

1. Kulinda Unyenyekevu (Khushui')
Unajua swala ya kiislamu inavyofanyika kuna kugusana baina ya vidole vya miguu na kuna kulinganisha mabega na zaidi kuna rukuu na sigda inayomtaka muumini kuinama na kuinuka na kuinamisha kichwa chini jambo ambalo kama utaswali na mwanamke pembeni linaweza kuondoa utulivu kwa kuamka matamanio na kukuondoa kwenye swala (unajua tena wenzetu wameumbwa na magnnetism)

2. Kuepuka Vishawishi (Fitna)
Uislamu unasisitiza kuzuia mazingira yanayoweza kuleta vishawishi kati ya jinsia mbili katika maeneo ya ibada. Kwa kutenga sehemu za kuswali, jamii inajenga mazingira ya heshima ambapo kila mmoja anaweza kuabudu kwa uhuru.

3. Sunnah
Wakati wa Mtume Muhammad (S.A.W), wanawake waliswali msikitini lakini walikuwa nyuma ya safu za wanaume. Mtume alisema kuwa safu bora kwa wanaume ni za mbele, na safu bora kwa wanawake (katika mazingira ya pamoja) ni za nyuma. Baadaye, kadiri idadi ya watu ilivyoongezeka, kuta au vyumba maalum viliwekwa kwa ajili ya urahisi na faragha zaidi.

SASA mkuu nakurudishia swali kuwa je kwenye biblia au tamaduni za zmani hakuna hiki kitu namaanisha kabla ya uislamu yaani hiki kitu ni kipya ???

hapana sio ktu kipya
Katika nyakati za Wana wa israel na hata baada ya hapo, Hekalu la Yerusalemu lilikuwa na sehemu maalum iitwayo "Ezrat Nashim (עֶזְרַת נָשִׁים)" Yaani Court of the Women.

Wanawake hawakuruhusiwa kuingia katika maeneo ya ndani yaliyotengwa kwa wanaume wa Kiisraeli au makuhani. Huu ulikuwa mgawanyo wa wazi wa kijinsia katika ibada.

Japo kwenye Katika Hekalu la Pili la Yerusalemu (Hekalu la Herode), hili lilikuwa eneo la nje ambapo Wayahudi wote (wanaume kwa wanawake) waliruhusiwa kuingia kwa ajili ya ibada za kawaida na kusikiliza mafundisho. ila wanawake hawakuruhusiwa kupita eneo hili kwenda ndani zaidi kuelekea madhabahuni (eneo lililoitwa Ezrat Yisrael ambalo lilikuwa maalum kwa wanaume tu).

Hadi leo, katika madhehebu ya kiorthodox ya Kiyahudi (ambayo yanafuata sheria za kale za Torati), wanaume na wanawake hukaa sehemu tofauti, mara nyingi zikitenganishwa na ukuta au pazia liitwalo Mechitza.

katika ukristo kwenye Mila za Kale
Kwa karne nyingi, katika makanisa mengi ya kale (ikiwemo baadhi ya makanisa ya Orthodox na Katoliki ya Mashariki), wanaume walikaa upande mmoja wa kanisa na wanawake upande mwingine.

Ingawa Biblia haisemi waziwazi ila inasisitiza juu ya utaratibu na staha. Kwa mfano, katika 1 Wakorintho 14:34-35 na 1 Timotheo 2:11-12, kuna maelekezo yanayoweka mipaka ya ushiriki wa wanawake katika mazingira fulani ya ibada ya hadhara ili kudumisha utaratibu.

Ki ufupi Mgawanyo wa jinsia si jambo la kiislamu pekeeni utaratibu uliokuwepo katika dini zote za Ibrahimu (Uyahudi, Ukristo, na Uislamu) kwa lengo la kudumisha staha na heshima katika nyumba za ibada, ingawa Ukristo wa kisasa katika madhehebu mengi umeacha utaratibu huo.
Ni kweli Kuna makanisa mengi tu wanawake wanakaa upande tofauti na wanaume, nilikuwa nategemea jambo kama hili pia misikiti badala ya wanawake kutengewa kwenye chumba tofauti kabisa.

Hata hivyo mfano wako wa hekalu sio sahihi kwa sababu Ukristo na Uyahudi ni dini tofauti kabisa.
 
Mkuu swala hilo linaitwa Ikhtilat kwa lugha ya kiarabu..
sasa nini faida yake:

1. Kulinda Unyenyekevu (Khushui')
Unajua swala ya kiislamu inavyofanyika kuna kugusana baina ya vidole vya miguu na kuna kulinganisha mabega na zaidi kuna rukuu na sigda inayomtaka muumini kuinama na kuinuka na kuinamisha kichwa chini jambo ambalo kama utaswali na mwanamke pembeni linaweza kuondoa utulivu kwa kuamka matamanio na kukuondoa kwenye swala (unajua tena wenzetu wameumbwa na magnnetism)

2. Kuepuka Vishawishi (Fitna)
Uislamu unasisitiza kuzuia mazingira yanayoweza kuleta vishawishi kati ya jinsia mbili katika maeneo ya ibada. Kwa kutenga sehemu za kuswali, jamii inajenga mazingira ya heshima ambapo kila mmoja anaweza kuabudu kwa uhuru.

3. Sunnah
Wakati wa Mtume Muhammad (S.A.W), wanawake waliswali msikitini lakini walikuwa nyuma ya safu za wanaume. Mtume alisema kuwa safu bora kwa wanaume ni za mbele, na safu bora kwa wanawake (katika mazingira ya pamoja) ni za nyuma. Baadaye, kadiri idadi ya watu ilivyoongezeka, kuta au vyumba maalum viliwekwa kwa ajili ya urahisi na faragha zaidi.

SASA mkuu nakurudishia swali kuwa je kwenye biblia au tamaduni za zmani hakuna hiki kitu namaanisha kabla ya uislamu yaani hiki kitu ni kipya ???

hapana sio ktu kipya
Katika nyakati za Wana wa israel na hata baada ya hapo, Hekalu la Yerusalemu lilikuwa na sehemu maalum iitwayo "Ezrat Nashim (עֶזְרַת נָשִׁים)" Yaani Court of the Women.

Wanawake hawakuruhusiwa kuingia katika maeneo ya ndani yaliyotengwa kwa wanaume wa Kiisraeli au makuhani. Huu ulikuwa mgawanyo wa wazi wa kijinsia katika ibada.

Japo kwenye Katika Hekalu la Pili la Yerusalemu (Hekalu la Herode), hili lilikuwa eneo la nje ambapo Wayahudi wote (wanaume kwa wanawake) waliruhusiwa kuingia kwa ajili ya ibada za kawaida na kusikiliza mafundisho. ila wanawake hawakuruhusiwa kupita eneo hili kwenda ndani zaidi kuelekea madhabahuni (eneo lililoitwa Ezrat Yisrael ambalo lilikuwa maalum kwa wanaume tu).

Hadi leo, katika madhehebu ya kiorthodox ya Kiyahudi (ambayo yanafuata sheria za kale za Torati), wanaume na wanawake hukaa sehemu tofauti, mara nyingi zikitenganishwa na ukuta au pazia liitwalo Mechitza.

katika ukristo kwenye Mila za Kale
Kwa karne nyingi, katika makanisa mengi ya kale (ikiwemo baadhi ya makanisa ya Orthodox na Katoliki ya Mashariki), wanaume walikaa upande mmoja wa kanisa na wanawake upande mwingine.

Ingawa Biblia haisemi waziwazi ila inasisitiza juu ya utaratibu na staha. Kwa mfano, katika 1 Wakorintho 14:34-35 na 1 Timotheo 2:11-12, kuna maelekezo yanayoweka mipaka ya ushiriki wa wanawake katika mazingira fulani ya ibada ya hadhara ili kudumisha utaratibu.

Ki ufupi Mgawanyo wa jinsia si jambo la kiislamu pekeeni utaratibu uliokuwepo katika dini zote za Ibrahimu (Uyahudi, Ukristo, na Uislamu) kwa lengo la kudumisha staha na heshima katika nyumba za ibada, ingawa Ukristo wa kisasa katika madhehebu mengi umeacha utaratibu huo.
Mkuu unajihangaisha tu kutoa haya majibu,
Aina ya mleta mada lengo lao kuu hua ni kukashifu na sio kuuliza ili kujua.
 
Umeona ile mada wanawake wenu wanashambuliwa kwa kuvaa nusu uchi kanisani ukaja kujifariji huku sio?
Wote ni wanawake wetu, sisi sote ni Waafrika kwanza na tunaunganishwa kama ndugu na Uafrica wetu kwanza, dini ni jambo la pili au la tatu huko kama ilivyo siasa, ushabiki wa mpira n.k
 
Ni kweli Kuna makanisa mengi tu wanawake wanakaa upande tofauti na wanaume, nilikuwa nategemea jambo kama hili pia misikiti badala ya wanawake kutengewa kwenye chumba tofauti kabisa.

Hata hivyo mfano wako wa hekalu sio sahihi kwa sababu Ukristo na Uyahudi ni dini tofauti kabisa.
hata nyuma wanakaa , hujawai bahatisha swala yeyote ya sikukuu viungani mkuu?
 
kheeee mwanaume unagubu wew kauliza swali tu imekuwa kosa ndio umchambe hivyo khooooo
Nenda kwenye huu uzi kisha soma comment 22# uone huyo mleta mada alivyomchamba mleta mada badala ya kudeal na hoja,na yeye acha tumuweke sawa kwanza.


 
Nenda kwenye huu uzi kisha soma comment 22# uone huyo mleta mada alivyomchamba mleta mada badala ya kudeal na hoja,na yeye acha tumuweke sawa kwanza.


😂😂😂 mpambano uendelee refa nipo hapa
 
Ni utaratibu tu waliojiwekea Waislam wakiamini kuwa, kila jinsia wakikaa mahali pao wenyewe watapata fursa zaidi ya kuwasiliana na Mungu kwa unyenyekevu zaidi na kuepusha matamanio.
Fikiria upo kwenye Ibada halafu anapita mrembo mwenye figure la ukweli au anaketi karibu na ulipokaa, Unaweza jikuta muda mwingi unawazia Mrembo badala ibada iliyokupeleka.....
Hivi kwa muktadha wa dini, kipimo cha imani si ndio majaribu?

Hivi mtu huitwa mshindi kwasababu amemshinda mpinzani au kwasababu ameepushiwa mshindani?

Utasemaje una imani thabiti ikiwa ni muoga kuya-face majaribu?

Hii inaenda sambamba kwa moja kwa wale wanaomini funga zao zinaweza kuharibika ikiwa tu watu wengine watakuwa huru kula mbele yao.
 
Hivi kwa muktadha wa dini, kipimo cha imani si ndio majaribu?

Hivi mtu huitwa mshindi kwasababu amemshinda mpinzani au kwasababu ameepushiwa mshindani?

Utasemaje una imani thabiti ikiwa ni muoga kuya-face majaribu?

Hii inaenda sambamba kwa moja kwa wale wanaomini funga zao zinaweza kuharibika ikiwa tu watu wengine watakuwa huru kula mbele yao.
Hakika dini zina contradictions nyingi na kubwa sana, ila ndio hivyo binadamu nao wan cognitive dissonance ya hali ya juu sana.
 
Wanawake wanaweza kuswali chumba kimoja na wanaume ila wataswali nyuma yao
Kuna maeneo kama Msikiti wa Makkah wanawake na wanaume wanaswali eneo moja ila wanatenganishwa tu na na barriers kuonesha mipaka yao
Nia ni kuleta modesty na kutoleta temptation na distraction wakati wa swala

Ukienda mbali zaidi, mafundisho ya dini hayaruhusu mchanganyiko usio wa lazima kati ya wanawake na wanaume ambao hawana mahusiano ya kindugu au ukaribu (mahrim)

Kuna baadhi ya nchi hasa za kiarabu ambazo kwenye public transport kama taxi za mchangio,( kwa Tz ni kama ilivyo bajaj) bus, train wanatenganishwa, kwenye foleni za banks pia wanawake na wanaume wana foleni tofauti, kwenye public schools na colleges pia kuna vyuo au madarasa tofauti
Hata nyumba za waarabu wengi kuna sebule 2, moja ya wanawake na nyingine ya wanaume

Kwa upande mwengine, Makanisa ya Eastern Orthodox mf Ethiopia wanafanya hivyo pia na hata Dar kuna kanisa la Father Nkwera wanafanya hivyo, nimeshuhudia kwa macho yangu wanawake na wanaume wanatenganishwa maeneo
 
Binafsi nadhani waislam wapo sahihi kabisa kutenganisha wanaume na wanawake, kwanza ni ile nature ya ibada yao, kuinama na kuinuka multiple times wakati wa kufanya ibada kunaweza kuwa kigezo cha kwanza kabisa, lakini pia kuondoa vishawishi vya macho. Huku kwa wakristo hata humu watu wengi wamekiri kuondolewa utulivu na usikivu kwa muingiliano wa hizi jinsi mbili.
 
Mkuu swala hilo linaitwa Ikhtilat kwa lugha ya kiarabu..
sasa nini faida yake:

1. Kulinda Unyenyekevu (Khushui')
Unajua swala ya kiislamu inavyofanyika kuna kugusana baina ya vidole vya miguu na kuna kulinganisha mabega na zaidi kuna rukuu na sigda inayomtaka muumini kuinama na kuinuka na kuinamisha kichwa chini jambo ambalo kama utaswali na mwanamke pembeni linaweza kuondoa utulivu kwa kuamka matamanio na kukuondoa kwenye swala (unajua tena wenzetu wameumbwa na magnnetism)

2. Kuepuka Vishawishi (Fitna)
Uislamu unasisitiza kuzuia mazingira yanayoweza kuleta vishawishi kati ya jinsia mbili katika maeneo ya ibada. Kwa kutenga sehemu za kuswali, jamii inajenga mazingira ya heshima ambapo kila mmoja anaweza kuabudu kwa uhuru.

3. Sunnah
Wakati wa Mtume Muhammad (S.A.W), wanawake waliswali msikitini lakini walikuwa nyuma ya safu za wanaume. Mtume alisema kuwa safu bora kwa wanaume ni za mbele, na safu bora kwa wanawake (katika mazingira ya pamoja) ni za nyuma. Baadaye, kadiri idadi ya watu ilivyoongezeka, kuta au vyumba maalum viliwekwa kwa ajili ya urahisi na faragha zaidi.

SASA mkuu nakurudishia swali kuwa je kwenye biblia au tamaduni za zmani hakuna hiki kitu namaanisha kabla ya uislamu yaani hiki kitu ni kipya ???

hapana sio ktu kipya
Katika nyakati za Wana wa israel na hata baada ya hapo, Hekalu la Yerusalemu lilikuwa na sehemu maalum iitwayo "Ezrat Nashim (עֶזְרַת נָשִׁים)" Yaani Court of the Women.

Wanawake hawakuruhusiwa kuingia katika maeneo ya ndani yaliyotengwa kwa wanaume wa Kiisraeli au makuhani. Huu ulikuwa mgawanyo wa wazi wa kijinsia katika ibada.

Japo kwenye Katika Hekalu la Pili la Yerusalemu (Hekalu la Herode), hili lilikuwa eneo la nje ambapo Wayahudi wote (wanaume kwa wanawake) waliruhusiwa kuingia kwa ajili ya ibada za kawaida na kusikiliza mafundisho. ila wanawake hawakuruhusiwa kupita eneo hili kwenda ndani zaidi kuelekea madhabahuni (eneo lililoitwa Ezrat Yisrael ambalo lilikuwa maalum kwa wanaume tu).

Hadi leo, katika madhehebu ya kiorthodox ya Kiyahudi (ambayo yanafuata sheria za kale za Torati), wanaume na wanawake hukaa sehemu tofauti, mara nyingi zikitenganishwa na ukuta au pazia liitwalo Mechitza.

katika ukristo kwenye Mila za Kale
Kwa karne nyingi, katika makanisa mengi ya kale (ikiwemo baadhi ya makanisa ya Orthodox na Katoliki ya Mashariki), wanaume walikaa upande mmoja wa kanisa na wanawake upande mwingine.

Ingawa Biblia haisemi waziwazi ila inasisitiza juu ya utaratibu na staha. Kwa mfano, katika 1 Wakorintho 14:34-35 na 1 Timotheo 2:11-12, kuna maelekezo yanayoweka mipaka ya ushiriki wa wanawake katika mazingira fulani ya ibada ya hadhara ili kudumisha utaratibu.

Ki ufupi Mgawanyo wa jinsia si jambo la kiislamu pekeeni utaratibu uliokuwepo katika dini zote za Ibrahimu (Uyahudi, Ukristo, na Uislamu) kwa lengo la kudumisha staha na heshima katika nyumba za ibada, ingawa Ukristo wa kisasa katika madhehebu mengi umeacha utaratibu huo.
Chukua mfano wa mjane mwenye senti chache.
Hapo ndiyo utajua kwenye sinagogi wanaume na wanawake waliabudu pamoja na walikuwa wanaonana.
hamna haja ya maelezo mengi. ni sheria tu za kibinadamu.
 
Back
Top Bottom