Picha kutoka kwa mdau aliyopost mtandaoni sio Taarifa rasmi yenye chanzo chochote cha kuaminika.
Kuna mtu ameanzisha mjadala kwanini wanaume wanakufa haraka kuliko wanawake. Jambo hili lipo kibiolojia zaidi na tafiti zunaendelea kufanyika. lakini nilazima ujue haya
1. Wanaume huanza kufa haraka tangu Mbegu ( Y) , kipindi cha ujauzito, na wakati wa Utotoni na ujanani wanaofika miaka ya uzee ni wachache
2. Hii inafanya takwimu kuonesha wanawake wengi ni wazee na wanaume wengi ni vijana na watoto
3. Je majukumu ndio sababu? Hii haiwez kuwa sababu ya moja kwa moja kwasababu wanaume wengi wanafariki katika umri wa utoto, wakati wa mimba na hata mbegu Y hufa mapema je ina majukumu gani? Vilevile Upande wa majukumu mengi kwa familia ni utamaduni wa africa mashariki nitofauti na nchi nyingine ambapo wanawake na wanaume hushirikina
3. Sababu ya wanaume kuwa na seli dhaifu inaweza kuwa na mashiko? Ndio. Hii inamaana kuwa hata ikiwa utawanyima mwanamke na mwanaume chakula kwa siku kadhaa tunategemea mwanaume kuanza kudhoofu zaidi na hata kufa mapema zaidi kuliko mwanamke.
4. Sababu ya sisi wanaume kuoa wanawake wadogo inaweza kuwa na mashiko? Ndio kwa asilimia chache
5. Habari njema. PAMOJA NA SISI WANAUME KUFA MAPEMA BADO IDADI YETU DUNIANI NI KUBWA KULIKO WANAWAKE KWA ZAIDI YA WANAUME MILION 40. na kufanya kuwa na Uwiano wa 101 Men : 100 women. ( Kwa mujibu wa sensa ya watu kwa kila nchi) World population by gender
Je mtazamo wako ni upi mdau