Jamaa_Mbishi
JF-Expert Member
- Jun 15, 2013
- 9,139
- 6,050
Naunga mkono hojaRadio Tanzania/ TBC FM wao ndio Wana archive kubwa kabisa ya nyimbo za zamani, kwani bendi zote za muziki, vikundi vya taarab na kwaya vilirekodi kwenye studio za RTD.
Kuna nyimbo nyingi sana hazipatikani YouTube wala sehemu yoyote Ile, hivyo Basi wapenzi wa muziki ya kwetu hatuna pa kulipata muziki Ile.
Kipindi Kama Tuimbe Sote cha kwaya, kila asubuhi. Tumbuizo asilia, kipindi cha Michael Karembo cha nyimbo za asili. Kipindi cha mashairi cha Malenga Wetu, kipindi cha Mama na Mwana cha Debora Mwenda, Muziki wa Mwambao na vingine vingi tulivipenda, ila Leo hatuna namna Tena ya kujikumbusha.
Namshauri mkurugenzi wa TBC alifanyie kazi Jambo hili.
Bujibuji Ngosha Jasu