mwanamakambako
JF-Expert Member
- Jan 3, 2014
- 780
- 120
Lowasa atagombea urais kwa chama kipi, maana mpaka sasa kashavunja miiko na maadili ya chama chake, sasa kama wewe hata chama chako tu hakikutaki, unang'ang'ania nini, hizo fedha anazogawa misikitini na makanisani na kwa vijana wa bodaboda, zitarudi vipi, kama kafikia hatua ya kuchafua nyumba za ibada kwa pesa chafu, itakuwaje akipewa nchi, tutapona kweli, akija kusema hamkunichagua ninyi, zilinichagua fedha tutakataa, na nyinyi mashehe na wachungaji mnaokubali pesa chafu za Lowasa na kuwarubuni waumini wenu wamuone Lowasa ni mzuri, mutawaeleza nini pindi machafuko yatakapoanza, muogopeni Mungu, na kumbukeni yaliyowakuta wenzenu Kenya.