Gorgeousmimi
JF-Expert Member
- Jun 21, 2010
- 9,296
- 7,666
Kheri ya pasaka waungwana!
Ningeanza na kusema kwenye kila jambo kuna pande mbili za shillingi.
Katika pitapita zangu nyingi nimegundua kuna uzi nyingi katika jukwaa hili la MMU zinazowakandamiza na kuwaponda single mothers! Mnasahau kama hao walowatia mimba single mothers nao ni single fathers?
Nakubali katika maisha kuna kukosa na kukosoana lakini ningependa tuwekane sawa katika hili, haimaanishi kwasababu BAADHI ya single mothers hawana msimamo na vigeugeu basi wote wapo hivo.
Na kingine kama mtu ni single mum lazima uelewe kuna sababu ilopelekea hilo sidhani kama kuna mtu anaependa kulea mtoto peke yake bila ya sababu ya msingi.
Au ukiachilia mbali hilo kuna baadhi wanaoamua kulea mwenyewe kwasababu the other part is not the right father figure for their child! Naamini si kila anayeweza kumimbisha mtu anapaswa kuwa baba!
Ningependa tuwekane sawa kuwa kuna single mother wa aina nyingi:
1. Kuna wadada wengi wanaoamua kujizalia tu kwasababu hakuna wanaume wanaoeleweka ambao wanakidhi viwango vyao na umri umeshatupa mkono mtu anaona ajizalie tu apate mrithi, wa aina hii naamini wanaweza kujimudu na kuhudumia watoto wao bila msaada wa mtu na ni watu wanaojielewa.
2. Kuna walopewa mimba ambazo wawili hao walikubaliana kuzaa pamoja na wakatengana kwasababu tofauti. Hawa mara nyingi wapo mguu ndani, mguu nje kwasababu kulikuwa na mapenzi na makubaliano kati yao kwahio ni rahisi kukumbushiana
3. Kuna walobeba ujauzito kibahati mbaya na mwanaume hayupo tayari kubeba majukumu. Wanawake wa kundi hili hawatakagi mahusiano na maex zao kiujumla kwasababu wanakuwa wameumizwa vyakutosha na wakishasonga mbele wamesonga.
4. Kuna walojibebesha mimba kwa matumaini ya kuolewa au kupata mwenza wa maisha au mteremko wa maisha(hawa ni wale ambao wanazaa hata na wanaume za watu). Hawa ni kundi jingine ambalo pia ni mguu ndani, mguu nje yaani anytime anarudiwa na kuachwa madhali yake yanamuendea.
But all in all mwishoni mwa siku kuna mwanaume alihusika katika hili kwa njia moja au nyingine. Kama ni kinga wanapaswa kutumia wote kujikinga na ujauzito usotarajiwa sasa ikiwa wewe unaenda kulala na mwanamke ambaye huna future nae bila kinga yoyote(kondom au uzazi wa mpango) unategemea nini hasa?
Tusihukumu single mothers kama wakosaji ni wao tu na wanaume ndo malaika mbona hamwahukumu single fathers? Au mnataka kusema wao ni tofauti kwasababu hawajabeba ujauzito.
Mtoto siku zote ni wamama ndio maana wamama ndio wanapata jukumu la kulea lakini tukipiga tathimini ya wanaume au ambao wamezaa tu ni single fathers naamini imepiku idadi ya wanawake.
Single fathers pia wanaweza kwenda kwa ex zao na kubinjuana so hakuna tofauti ya kusema ni single mothers tu sio Wife material kwasababu mnahofia wataliwa. Then tunaweza kusema Single fathers nao sio Husband material. This goes both ways kwa jinsia zote.
La muhimu ni kujuana vyema huyo single mum/ dad kabla ya kuanzisha mahusiano naye na mahusiano alokuwa nayo na ex wake lakini sio kuhukumiana!
Ningeanza na kusema kwenye kila jambo kuna pande mbili za shillingi.
Katika pitapita zangu nyingi nimegundua kuna uzi nyingi katika jukwaa hili la MMU zinazowakandamiza na kuwaponda single mothers! Mnasahau kama hao walowatia mimba single mothers nao ni single fathers?
Nakubali katika maisha kuna kukosa na kukosoana lakini ningependa tuwekane sawa katika hili, haimaanishi kwasababu BAADHI ya single mothers hawana msimamo na vigeugeu basi wote wapo hivo.
Na kingine kama mtu ni single mum lazima uelewe kuna sababu ilopelekea hilo sidhani kama kuna mtu anaependa kulea mtoto peke yake bila ya sababu ya msingi.
Au ukiachilia mbali hilo kuna baadhi wanaoamua kulea mwenyewe kwasababu the other part is not the right father figure for their child! Naamini si kila anayeweza kumimbisha mtu anapaswa kuwa baba!
Ningependa tuwekane sawa kuwa kuna single mother wa aina nyingi:
1. Kuna wadada wengi wanaoamua kujizalia tu kwasababu hakuna wanaume wanaoeleweka ambao wanakidhi viwango vyao na umri umeshatupa mkono mtu anaona ajizalie tu apate mrithi, wa aina hii naamini wanaweza kujimudu na kuhudumia watoto wao bila msaada wa mtu na ni watu wanaojielewa.
2. Kuna walopewa mimba ambazo wawili hao walikubaliana kuzaa pamoja na wakatengana kwasababu tofauti. Hawa mara nyingi wapo mguu ndani, mguu nje kwasababu kulikuwa na mapenzi na makubaliano kati yao kwahio ni rahisi kukumbushiana
3. Kuna walobeba ujauzito kibahati mbaya na mwanaume hayupo tayari kubeba majukumu. Wanawake wa kundi hili hawatakagi mahusiano na maex zao kiujumla kwasababu wanakuwa wameumizwa vyakutosha na wakishasonga mbele wamesonga.
4. Kuna walojibebesha mimba kwa matumaini ya kuolewa au kupata mwenza wa maisha au mteremko wa maisha(hawa ni wale ambao wanazaa hata na wanaume za watu). Hawa ni kundi jingine ambalo pia ni mguu ndani, mguu nje yaani anytime anarudiwa na kuachwa madhali yake yanamuendea.
But all in all mwishoni mwa siku kuna mwanaume alihusika katika hili kwa njia moja au nyingine. Kama ni kinga wanapaswa kutumia wote kujikinga na ujauzito usotarajiwa sasa ikiwa wewe unaenda kulala na mwanamke ambaye huna future nae bila kinga yoyote(kondom au uzazi wa mpango) unategemea nini hasa?
Tusihukumu single mothers kama wakosaji ni wao tu na wanaume ndo malaika mbona hamwahukumu single fathers? Au mnataka kusema wao ni tofauti kwasababu hawajabeba ujauzito.
Mtoto siku zote ni wamama ndio maana wamama ndio wanapata jukumu la kulea lakini tukipiga tathimini ya wanaume au ambao wamezaa tu ni single fathers naamini imepiku idadi ya wanawake.
Single fathers pia wanaweza kwenda kwa ex zao na kubinjuana so hakuna tofauti ya kusema ni single mothers tu sio Wife material kwasababu mnahofia wataliwa. Then tunaweza kusema Single fathers nao sio Husband material. This goes both ways kwa jinsia zote.
La muhimu ni kujuana vyema huyo single mum/ dad kabla ya kuanzisha mahusiano naye na mahusiano alokuwa nayo na ex wake lakini sio kuhukumiana!