...lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)
Waliweza kuingausha USSR kwasababu ya ukubwa na uchumi. Russia ya leo haiwezi kugawanyika , in fact nchi zilizojitoa zinasikitika. Urusi kama Taifa kubwa ilifanya kosa! kudharau nguvu ya Uzalendo.
Putin alidhani ataingia Kiev kama mkata keki. Kipigo cha mwanzo kilimvuruga na kuijengea Ukraine confidence.
... Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).
Vijana wengi sijui ni kwa kutojua, kiburi , uzembe au udumavu!! hoja hii hawaioni kabisa.
Iran inapigana na Mataifa zaidi 9. Ni Iran iliyo katika vikwazo vya uchumi kwa miaka 40.
Iran haipigani vita, inapigania Survival.
Iran inaangaliwa kwa 'jicho la kengeza ''biased''inatuhumiwa kushambulia majirani bila kujua inapigania survival. Israel ilipopiga Gaza, Lebanon , Syria, Tunisia, Yemen na Qatar ilisemwa hiyo ni ''self defense''.
Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi.
Trump aliwatimua Makamanda walioshiriki vita za nyuma kwa kudhani wanamhujumu.
Makamanda hawakukubali ''ndio mzee'' kwahiyo akapoteza '' institution memory ya Pentagon''
Jaribio la Venezuela likamtia kiburi kwamba Pentagon wanaweza kufanya lolote Duniani
Nia ya Trump ni ''TACO'' kwamba anatisha bila kufanya jambo kuilazimisha Iran ikubali masharti.
Vyombo vya usalama 'kwa taarifa ya jana'' vilimweleza tatizo la kumuua Ayatollah
Trump hakupenda lakini kuna nguvu nyingine, Israel isiyotaka majadiliano bali Iran apigwe.
Waziri wa mambo ya nje M.Rubio amethibisha kwa kauli kwamba hawakutaka lakini Israel ilisema itamuua Ayatollah bila USA. Hilo likawalazimu Marekani kujiunga katika Vita.
Kumuua Ayatollah Khamenei kwa kudhani wananchi wataingia mtaani kuchukua nchi ni kosa.
Vita ya siku 12 ilionyesha Wananchi wa Iran waliungana badala ya kutengana.
Maandamano yanayoratibiwana Israel na Marekani yana watu maelfu lakini kuna mamilioni Wanaipenda serikali yao. Kwa mfano, baada ya kuuawa mamilioni waliingia mtaani licha ya mabomu kurindima katika mitaa yao.
Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000.
Hakuna kambi ya US iliyobaki pale middle east. Nani amewahi kufanya hivyo katika miaka 85!
Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.
Kama utakumbuka , sehemu ya kwanza Iran kushambulia ni ile RADAR kubwa middle east.
Walipoiondoa kukakosekana muundo wa kuona makombora.
Kilichotumika ni THAAD na PATRIOT kutumiwa kuangusha Drone ya USD 25K.
Kwasasa hakuna tena air defense pale middle east, THAAD na PATRIOT zilizobaki zimehamishiwa Israel.
Nchi za Kiarabu zimejawa na jazba kwamba zimetumika na ulinzi umehamishiwa Israel.
Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.
Vita ya siku 12 iliwa andaa sana Iran, hata hivyo kuna usaidizi wa kiitentelejensia kutoka ''within''
Uchunguzi unaendelea kuhusu ndege 3 zilizotunguliwa Kuwait kukiwa na hisia za hujuma.
Intelijensi ya Iran ni rahisi sana ku penetrate middle east kwasababu ya madhebu.
Kwa mfano kuwait na Qatar kuna Shia wengi. Ndivyo ilivyokuwa kwa UAE, Saudi na Oman
Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???
Iran ina wasomi wa maana sana. Siku ya kwanza ya shambulio waliuawa Wasichana zaidi ya 100.
Watu hawajiulizi kwanini waliuawa Wasichana? Marekani na Israel hawajatoa madai yoyote ya eneo la shule kuwa la kijeshi. Kwa taarifa, shule ile ni ya Watoto wenye vipaji katika science.
Iran ina literacy level katika 99 kukiwa na University ambazo Wanawake ni wengi kuliko wanaume.
Iran ni vinara wa mathematics na sayansi ya anga. Nyuma ya computers kuna akili za Wairan
Ni wazuri sana wa Teknolojia .Wasomi wa Iran wanatumia makosa kujifunza
Vita na Iraq, wameona ya Libya na hata vita ya siku 12. Wametumia wataalamu kujifunza
Iran wame survive miaka 40 ya vikwazo, wamegeuza vikwazo kama kichocheo cha maendeleo yao.
MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:
Mosi, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika.
In fact Iran kaonyesha matundu ya Marekani, na Trump anajitahidi sana pa kutokea vita isiendelee.
Waandishi wa habari wanahoji vifo! ingawa ni siri na tunajua Trump hataki kuonekana ameshindwa, ipo siku watu watabaini vifo si 6 !
Iran imethibtisha yale ambayo vijana hawakuyaona. Kwa miaka mingi tumeeleza hapa kwamba Israel haiwezi kusimama yenyewe, ipo katika mbeleko ya USA. Vijana wakasema ni Taifa lenye nguvu sana za kijeshi. Tel Aviv inatekea! Iron dome, David sling, Arrow, THAAD, PATRIOT Zote zimefeli.
Iran imepiga kila taasisi ya ulinzi ya Israel na kila kona iliyosemwa haiguswi.
Vita iliyopo sasa ni ya Marekani na washirika, Israel inatajwa tu lakini ukweli ni kwamba inapigwa sana
Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani
Marekani haingii
Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???
True!