Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Muda huwa ni mwalimu mzuri sana.

Nakumbuka mabazazi na madunya wa humu ndani mnamo tarehe 24 February 2022 siku ambayo Urusi alivamia Ukraine walinitafuta na kunisimanga sana. Wengine walidiriki hadi kukashifu taaluma yangu. Walishangaa kwamba kwanini Urusi ameshindwa kuivamia Ukraine na kuimaliza kwa haraka ilhali anajiita taifa kubwa (Super-Power). Niliwaambia vijana wa humu ndani kwamba Urusi alifanya makosa kuvamia jirani yake na kuna mambo alikosea, lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)

Mpaka 2026, Urusi na Ukraine wanapigana, huku Ukraine wakiwa wameumizwa zaidi. Urusi anatumia fedha nyingi sana kwenye vita na usalama, jambo ambalo siku vita ikiisha litazua matatizo makubwa mno kwasababu watu wengi watakosa ajira ambazo wanazifanya sasa. Pia kuna mambo kadha wa kadha. Sasa huu ni utangulizi tu:

Naomba niwaulize ninyi vijana wa humu ndani, kwanini Marekani (The Only Global Super-Power) ameshindwa kulimaliza taifa la Iran ndani ya wiki kama alivyofanya Afghanistani au Venezuela ??? Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).

Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi. Ila sasa yametokea tofauti. Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000. Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.

Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.

SASA IRAN ANAPAMBANAJE: Mwaka 2018 nakumbuka kuna uzi wangu nilifurumushiwa matusi na mabazazi na madunya wa humu ndani, nilioandika kuhusu dhana ya ASYMETRIC WARFARE. Dhana hii inafanya kazi pale ambapo taifa dogo au kikundi kidogo kinapambana na taifa kubwa. Lengo siyo kutaka kupambana CONVENTIONAL WARFARE, ila ni kumsababishia maumivu makubwa yule aliye mkubwa kiasi cha kufanya akimbie. Mfano halisi, ni USSR vs Mujahedeen au USA vs Vietcong.

Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???

MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:

Mosi
, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika. Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani, nani anaamini kabisa kwamba kambi za Marekani zilizopo South-Korea, Philippines, Japan na Guam zitakuwa salama, kama tu kambi kubwa za Marekani barani Asia zimelipuliwa juzi na jana na Iran, taifa ambalo halina nguvu kama Uchina. Kiukweli, Marekani alizichanga karata vibaya na yanamtokea puani.

Pili, Urusi atapata nguvu kubwa kutokana na bei ya mafuta kupanda. Saudi Arabia, UAE, Oman, Qatar na Bahrain wanaogopa kupitisha mafuta Mfereji wa Hormuz, ambao kwa siku mapipa milioni 17 yanapita. Vita ikiendelea hivi na Iran akafanikiwa kufunga kabisa mfereji, basi mafuta ya Ulaya na Asia itabidi yapatikane Urusi ambako kuna vikwazo. Juzi Vladmir Putin kasema anafikiria kusitisha kabisa kuuza gesi Ulaya. Sasa USA na EU watabakiwa na maamuzi kama haya: Ondoa vikwazo ili tupate nishati kutoka Urusi. Bahati mbaya wakiondoa vikwazo Ukraine ndiyo kwaheri.

Tatu, Urusi atapenda kulipiza alichofanyiwa Ukraine. Hii ndiyo tabia kuu ya Urusi. Niguse-Ninuke. Marekani akitingwa kule Iran, basi lazima atapunguza kuangalia Ukraine. Sasa itabidi silaha zote zinazozalishwa zienda Persian Gulf (Ghuba ya Uajemi) siyo Ukraine. Urusi na Uchina wanaweza kuigeuza Iran, VIETNAM 2 endepo Marekani akiendelea hivi bila kuomba msamaha. Bahati mbaya sana kwa alichokifanya Donald Trump, Marekani ikirudi nyuma kama kipindi cha Twelve Days War mwaka 2024, basi ndiyo mwisho wa siasa za MAGA na Trump, na anaweza kufungwa kwasababu ameanzisha vita bila kibali cha Bunge.

Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???

Tano, THE COLLAPSE OF THE LAW OF NEUTRALITY. Katika sheria za kimataifa hasa wakati wa vita, The Law of Neutrality huyalinda mataifa ambayo hayapambani moja kwa moja, hata kama yanakuwa yanauza silaha kwa adui au kuwa na kambi za kijeshi ambazo hazitumiki kijeshi kushambulia adui. Kitendo cha Marekani kuvamia Iran bila sababu ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Hata Iran kuanza kuvamia Saudi-Arabia, UAE na Qatar ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Lakini Marekani hawezi kulalamika katika hili kwasababu yeye ndiye mvunjifu sugu wa sheria za kimataifa. Sheria za kimataifa ili zifuatwe na mataifa madogo, inategemea sana mataifa makubwa.

Hili lisipoangaliwa sana, tutaamka siku na kukuta Urusi kaanza kulipua Poland na Ujerumani kisa tu kuna kambi za jeshi za Marekani, hata kama hazitumiki kushambulia. Huku ndiko tunaelekea. Hivyo tukishafahamu haya, vitaifa masikini kama Tanzania vijiepushe na tabia za kupenda kujipendekeza kwa mataifa makubwa kama Uchina, Urusi na Marekani. Dunia inaelekea kubaya na kama tukitaka kuvuka itabidi kweli tusifungamane na upande wowote. Sasa wale wanopenda pesa za waarabu kisa ni wenzetu katika IMANI wakiendeleza tabia zao za kusajili manowari kule Zenji, wataliletea hili taifa matatizo makubwa mno. Tena kipindi hiki ukipigwa huna pakusemea maana kila mtu anapambana lwake.

==============================================================================

HALAFU KUNA MABAZAZI mengine yanasema INTERNATIONAL LAW IMEKUFA, haya nitayajibu baadaye.HAYANA AKILI

mabazazi na mandunya sidhani kama wamekuelewa...mkuu hivi unafahamu kwamba mabazazi na mandunya wengi wao ni ccm?
 
HATA wewe unalinganisha visivyolinanishika,hakuna kitu Cha maana ulichoandika.

1) Iran Ina vikwazo Kwa zaidi ya miaka 40,wakati Ukraine Haina vikwazo vyovyote.

2) Ukraine ilikua inafundishwa na NATO kwa miaka zaidi ya minane ,wakati Iran ikiwa Iko vikwazoni

3) wiki ya kwanza TU ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ilikaribia kuingia Kiev,west wakaidanganya Urusi kua Ukraine Iko tayari kwa mazungumzo,wakaenda uturuki kuongea kumbe NATO wanajipanga kumsaidia Ukraine,
Ndio maana Hadi Leo NATO wapo Ukraine .
Wakati Iran anahangaika peke yake.
4) Sio mpango wa Urusi kumuua Zelensky wala Regime change Ukraine Bali Ukraine isijiunge NATO na haijajiunga.
Wakati Israel na USA waliidanganya Iran kua wiki ijayo mazungumzo yataendelea ndio ikapelekea Viongozi wa Iran kutoka na hofu ya kuvamiwa walikaa au waliishi Kwa Imani kua wiki ijayo wataemdelea na mazungumzo,walijiachia,kumbe wenzao ni waongo na hawakua waaminifu,walavamia na kumuua Ayatollah na wenzake,wakati Israel na USA wakifanya hayo Benjamin Netanyahu alikimbilia ujerumani kujificha.
5)Iran sera Yao sio kuua Viongozi wa nchi nyingine ,wakati Isarel sera yake ni kuua Viongozi wa nchi maadui
Vivyo hivyo kwa Urusi na Ukraine Urusi Haina mpango wa kumuua Zelensky wala viongozi wa Ukraine lkn Ukraine na west sera Yao ni kuua Viongozi wa nchi nyingine(Ugaidi).

6) Vita vya Urusi imechukua miaka minne Urusi ikipigana na Ukraine inayosaidiawa na All collective west,wakati vita vya Israel-USA - Iran bado haijaisha,tusubiri itaisha lini ndio tuone ulinganifu.wakati Iran ikipigana peke yake dhidi ya Israel Marekani Qartari,Sound Arabia, Jordan,UAE, Bahrain,n.k ambazo zilisaidia sana kuangusha makombora ya iran

7) Iran haijashambulia marekani moja kwa moja kwa sababu za kijiografia na Irani Haina uwezo huo,lkn imepiga Kambi zote za jeshi za USA na ndani ya ardhi ya Israel,hii maana yake kama Marekani ingekua ilipo Turkyl eo hii nayo ingepigwa.
Hata hivyo Kambi za kijeshi za USA ni sehemu ya Marekani kijeshi hivyo zingeachwa zingeshiriki kuipiga Irani,ndio lengo la kuwepo makambi hayo kuirahisishia marekani kuishambulia nchi jirani na Kambi hizo.
Lakini kwa bahati mbaya kwa marekani wanajeshi wote wa USA waliokua kwenye Kambi hizo wamezikimbia kabla na baada yavkupigwa,hivyo lengo la kujenga kabisa hizo limefeli aubhalijasaidia kitu.
8) Abraham Lincoln imeshambuliwa na ikahamishwa au kukimbizwa,hivyo Nayo umeshindwa kufanya kazi iliyokusudiwa au iliyosababiswa kupelekwa ghuba.
9)kama alivyosema mtoa mada toka Dunia hii iumbwe hii ni mara ya pili baada ya Miaka mingi kwa marekani kupigwa kwa miundombinu yake ya kijeshi silaha na vifaa vingine kama rada viwanja vya ndege na bandari za melivita na kuharibiwa vibaya kama kama ilivyotokea ndani ya siku nne TU,baada ya Pearl Harbour attack.
10) katika histotia ya Dunia hakuna kipindi ambacho Marekani ameomba msaada kijeshi kama mwaka huu,na hata kaomba Msaada wa viwanja vya kurushia ndege zake na kanyimwa na Hispania,Sasa najiuliza Kambi zake za middle east zimemsaidia Nini na alizijenga za Nini?
Katika historia ya USA haijawahi kushindwa kuokoa raia wake kwa maelfu waliokwama middle east kama kipindi hiki.,wamekwama aisee.maana kule ghuba ndege za kiraia zimeshindwa kuruka.
Kwa kifupi Iran kazua balaa kubwa.
11) Kuna uzuiaji mkubwa wa habari za Iran inaposhambulia Israel na USA,habari zinatoka kwa kuchujwa mno tofauti na habari zinazorushwa kutoka Vyombo vya magharibi zikiishambulia Iran.
Tutayajua mengi baadae.
12) Sina uhakika lkn inasemwa USA aliiomba Italy ikaiombe Iran wayamalize iache vita ,Iran ikakataa kumaliza vita.
😄😄
 
Hoja kuu ya MALCOM LUMUMBA ambayo ninaiona inamashiko ni Wairan bado wengi wanamshikamano na serikali yao.
Hiyo ndio hoja kuu.

Kwamba Marekani na Israel vita hii itakuwa ngumu kwao kushinda au itachukua muda mrefu kushinda kwa sababu bado Iran inanguvu ya umoja baina yao.

Kwamba Wamerakani wameshindwa kuwagawanya wa Iran. Tofauti na Marekani alivyotarajia.

Hii itapelekea ugumu kwa Marekani kuvamia Iran kijeshi kwa kutumia Majeshi ya ardhini.
Na kama hakuna majeshi ya ardhini itamaanisha lengo la regime change halitafikiwa.
Naona hiyo ndio hoja yako kubwa.

Lakini mpaka sasa Iran yupo kujihami, anajitetea na Hana lengo na hawezi kushinda kwa kusema amuangamize adui yake.

Ukweli ni kuwa Marekani na Israel hii vita wanaitaka, na kwao ni muhimu kushinda. Na Hilo litatokea tuu.

Kwa vile Marekani na Israel nao ni watu kama watu wengine. Ikitokea Wameshindwa kufikia Malengo basi mambo mengi yatabadilika hapo Mashariki ya Kati lakini pia Mtazamo wa mataifa duniani kumhusu Mmarekani
 
Kuvamia taifa jingine huru, kijeshi kwasababu linafanya maamuzi yake kisiasa ni kosa kisheria.

Urusi mwenyewe aliwaruhusu Wayukraini watoke kwenye Muungano mwaka 1991.

Kinachofanyika hapa ni siasa za mataifa makubwa (Great Power Politics) ambapo ukweli mchungu ni kwamba sheria inakataza, ila uhalisia ni kitu kingine, kwamba ukiingilia maslahi ya taifa kubwa halafu wewe ni kitaifa kidogo ndiyo madhara ambayo yanaikuta Ukraine. Sheria inamlinda Ukraine, lakini uhalisia wa siasa za dunia una taswira nyingine kabisa. Marekani na NATO walimponza Ukraine, naye akijidanganya akaingia mazima, mwishowe yakamkuta.

Taiwan na Japan wasipojifunza watakuja kupigwa na kitu kizito nao wasiamini.....

So Kama Hali ndio Iko hii it means fair treat katika siasa haipo na haiwezi kuwepo , Kwa muktadha huu inaweka wazi kwamba Russia ana haki ya kujilinda dhidi ya adui na kama alifuatwa hatua za kidiplomacy kutaka kumaliza mgogoro halafu hakusikilizwa basi Hilo ndio linalo mpaka mandate kabisa ya kufanya kile alicho kifanya
 
Kwa hiyo mkuu Iran na Marekani wangekuwa wanashea mpaka kama ilivyo kwa Urusi na Ukraine makombora na drone za Iran zisingekuwa zinapiga kwenye miji ya Marekani?
Ila ni kweli hatakiwi kulinganisha maana Ukraine ilivamiwa na Urusi peke yake lakini Iran kavamiwa na mataifa mawili.
🤣 Mnanini lakini !? Halafu wamefumba macho na masikio
 
...lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)
Waliweza kuingausha USSR kwasababu ya ukubwa na uchumi. Russia ya leo haiwezi kugawanyika , in fact nchi zilizojitoa zinasikitika. Urusi kama Taifa kubwa ilifanya kosa! kudharau nguvu ya Uzalendo.
Putin alidhani ataingia Kiev kama mkata keki. Kipigo cha mwanzo kilimvuruga na kuijengea Ukraine confidence.
... Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).
Vijana wengi sijui ni kwa kutojua, kiburi , uzembe au udumavu!! hoja hii hawaioni kabisa.

Iran inapigana na Mataifa zaidi 9. Ni Iran iliyo katika vikwazo vya uchumi kwa miaka 40.
Iran haipigani vita, inapigania Survival.

Iran inaangaliwa kwa 'jicho la kengeza ''biased''inatuhumiwa kushambulia majirani bila kujua inapigania survival. Israel ilipopiga Gaza, Lebanon , Syria, Tunisia, Yemen na Qatar ilisemwa hiyo ni ''self defense''.

Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi.
Trump aliwatimua Makamanda walioshiriki vita za nyuma kwa kudhani wanamhujumu.

Makamanda hawakukubali ''ndio mzee'' kwahiyo akapoteza '' institution memory ya Pentagon''
Jaribio la Venezuela likamtia kiburi kwamba Pentagon wanaweza kufanya lolote Duniani

Nia ya Trump ni ''TACO'' kwamba anatisha bila kufanya jambo kuilazimisha Iran ikubali masharti.

Vyombo vya usalama 'kwa taarifa ya jana'' vilimweleza tatizo la kumuua Ayatollah
Trump hakupenda lakini kuna nguvu nyingine, Israel isiyotaka majadiliano bali Iran apigwe.

Waziri wa mambo ya nje M.Rubio amethibisha kwa kauli kwamba hawakutaka lakini Israel ilisema itamuua Ayatollah bila USA. Hilo likawalazimu Marekani kujiunga katika Vita.

Kumuua Ayatollah Khamenei kwa kudhani wananchi wataingia mtaani kuchukua nchi ni kosa.

Vita ya siku 12 ilionyesha Wananchi wa Iran waliungana badala ya kutengana.

Maandamano yanayoratibiwana Israel na Marekani yana watu maelfu lakini kuna mamilioni Wanaipenda serikali yao. Kwa mfano, baada ya kuuawa mamilioni waliingia mtaani licha ya mabomu kurindima katika mitaa yao.
Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000.
Hakuna kambi ya US iliyobaki pale middle east. Nani amewahi kufanya hivyo katika miaka 85!
Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.
Kama utakumbuka , sehemu ya kwanza Iran kushambulia ni ile RADAR kubwa middle east.
Walipoiondoa kukakosekana muundo wa kuona makombora.

Kilichotumika ni THAAD na PATRIOT kutumiwa kuangusha Drone ya USD 25K.

Kwasasa hakuna tena air defense pale middle east, THAAD na PATRIOT zilizobaki zimehamishiwa Israel.
Nchi za Kiarabu zimejawa na jazba kwamba zimetumika na ulinzi umehamishiwa Israel.
Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.
Vita ya siku 12 iliwa andaa sana Iran, hata hivyo kuna usaidizi wa kiitentelejensia kutoka ''within''
Uchunguzi unaendelea kuhusu ndege 3 zilizotunguliwa Kuwait kukiwa na hisia za hujuma.

Intelijensi ya Iran ni rahisi sana ku penetrate middle east kwasababu ya madhebu.
Kwa mfano kuwait na Qatar kuna Shia wengi. Ndivyo ilivyokuwa kwa UAE, Saudi na Oman
Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???
Iran ina wasomi wa maana sana. Siku ya kwanza ya shambulio waliuawa Wasichana zaidi ya 100.

Watu hawajiulizi kwanini waliuawa Wasichana? Marekani na Israel hawajatoa madai yoyote ya eneo la shule kuwa la kijeshi. Kwa taarifa, shule ile ni ya Watoto wenye vipaji katika science.

Iran ina literacy level katika 99 kukiwa na University ambazo Wanawake ni wengi kuliko wanaume.
Iran ni vinara wa mathematics na sayansi ya anga. Nyuma ya computers kuna akili za Wairan

Ni wazuri sana wa Teknolojia .Wasomi wa Iran wanatumia makosa kujifunza
Vita na Iraq, wameona ya Libya na hata vita ya siku 12. Wametumia wataalamu kujifunza
Iran wame survive miaka 40 ya vikwazo, wamegeuza vikwazo kama kichocheo cha maendeleo yao.
MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:

Mosi
, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika.
In fact Iran kaonyesha matundu ya Marekani, na Trump anajitahidi sana pa kutokea vita isiendelee.
Waandishi wa habari wanahoji vifo! ingawa ni siri na tunajua Trump hataki kuonekana ameshindwa, ipo siku watu watabaini vifo si 6 !

Iran imethibtisha yale ambayo vijana hawakuyaona. Kwa miaka mingi tumeeleza hapa kwamba Israel haiwezi kusimama yenyewe, ipo katika mbeleko ya USA. Vijana wakasema ni Taifa lenye nguvu sana za kijeshi. Tel Aviv inatekea! Iron dome, David sling, Arrow, THAAD, PATRIOT Zote zimefeli.
Iran imepiga kila taasisi ya ulinzi ya Israel na kila kona iliyosemwa haiguswi.

Vita iliyopo sasa ni ya Marekani na washirika, Israel inatajwa tu lakini ukweli ni kwamba inapigwa sana
Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani
Marekani haingii
Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???
True!
 
Lakini pia hilo wenda lingeipa urahisi pia Iran kuwadhuru wamarekani tofauti na sasa ambapo wako mbali.
Nadhani unataka kuja na hoja ya kwamba Marekani ingekuwa imepakana na Iran mashambulizi yake dhidi ya Iran yangekuwa rahisi lakini kumbuka kuwa hata sasa kambi zote za Marekani zilizo izunguka Iran zote amezikimbia amerazimika kushambulia kutoka mbali.
Muulize siyupo karibu na Cuba Nini kilicho tokea baada ya kuvamia Cuba !? 😄
 
Hoja kuu ya MALCOM LUMUMBA ambayo ninaiona inamashiko ni Wairan bado wengi wanamshikamano na serikali yao.
Hiyo ndio hoja kuu.

Kwamba Marekani na Israel vita hii itakuwa ngumu kwao kushinda au itachukua muda mrefu kushinda kwa sababu bado Iran inanguvu ya umoja baina yao.

Kwamba Wamerakani wameshindwa kuwagawanya wa Iran. Tofauti na Marekani alivyotarajia.

Hii itapelekea ugumu kwa Marekani kuvamia Iran kijeshi kwa kutumia Majeshi ya ardhini.
Na kama hakuna majeshi ya ardhini itamaanisha lengo la regime change halitafikiwa.
Naona hiyo ndio hoja yako kubwa.

Lakini mpaka sasa Iran yupo kujihami, anajitetea na Hana lengo na hawezi kushinda kwa kusema amuangamize adui yake.

Ukweli ni kuwa Marekani na Israel hii vita wanaitaka, na kwao ni muhimu kushinda. Na Hilo litatokea tuu.

Kwa vile Marekani na Israel nao ni watu kama watu wengine. Ikitokea Wameshindwa kufikia Malengo basi mambo mengi yatabadilika hapo Mashariki ya Kati lakini pia Mtazamo wa mataifa duniani kumhusu Mmarekani
Till now mitazamo ya watu imeshaanza kubadilika kama Nina kupa hadhi / dhamana ya kunilinda and still Nina shambuliwa wakati wewe mlinzi wangu upo so what do you expect!?? .

Wewe ulitegemea kuona kitu kama hicho !?
 
Iran ni taifa dogo kushinda marekani lakini USA ain't having an easy way.

Marekani hawezi kupigana vita bila kuwa na allies ambae kwa sasa ni waarab(wote wamechezea) na Israel.

Iran anasurvive peke yake, pamoja na kwamba amekuwa kwenye economic sanctions kwa miaka zaidi ya 40 sasa.

Waajemi sio wamatumbi kwamba you can have an easy route.
 
Wewe jamaa tangu uandike uongo uongo kule kwenye uzi wa mgogoro wa Urusi na Ukraine, inahitaji kusoma mara mbili mbili unachoandika.
Kwa hiyo nyinyi mnafurahi taifa moja kuua political leadership ya taifa jingine kisa vita???Hiyo ni sign ya weakness sio nguvu.Nguvu inatambulika kwenye utiifu wa sheria za kimataifa, sio kulipua watu na nchi kisa una jeshi kubwa, nguvu kubwa etc.
Pili mlitaka Urus wamle kichwa Zelensky ili tu awafurahishe watu kama nyinyi et ndo nguvu hizo au sio???Umesahau Putin alimuhakikishia waziri mkuu wa Israel kipindi kile kuwa hatomgusa Zelensky???Uo ndo uongozi...
Vita sio betting, au Simba na Yanga, kwamba mna-prove ubishi wenu kwa kutembea na roho za watu.
Et Urusi hatawali anga, mosi hujui kuwa kuna vijeba vimejichimbia pale -NATO na air defenses za Kutosha, utalinganisha na Iran??
Pili Urusi anawezapiga popote kwa missiles akitokea kwake, kwa nini ahangaike kuweka rehani maisha ya airforce yake wakati ana alternative??Makombora tu na drones zinagusa kila kona..

US atashinda pambano pale Iran lakini hatshinda vita...BATTLES yes, atawatwanga kwelikweli lkn kushinda vita sio rahisi pale, nchi kubwa ile, milima na mapango kama yote
[/QUOTE]

Vita ya Urusi niliandika uongo gani, miaka minne iliyopita?

Political leadership haitakiwi kuuwawa ila inategemeana na mazingira, umeona Rais wa Iran anauwawa?
Sasa Ayatollah yeye main policy yake ni "Death to Israel" na haiachi miaka zaidi ya 40 sasa wafanyeje na wameishajizuia miaka mingi kumsitiri, Ayatollah atakayedumu atakaa kwa heshima. Mbona Hezbollah na Hamas nao wamejiheshimu baada ya kila kiongozi anayejifanya amechanganyikiwa, anauwawa.
Ni sheria za wanasiasa hizo ili kujilinda vita ikitokea, ili wapange mipango ya kipuuzi kutuma vijana wa watu wakafie frontline huku nyuma wao wanakula na kusaza. Kukiwepo tishio la kuwaua ndio sense inakaa kichwani mwao wanatafuta suruhisho haraka.
Viongozi wa kijeshi mara nyingi wanauwawa wakiwa kwenye majukumu ya kijeshi, ama yupo kambini au frontline au kwenye ammo dump au anakagua utekelezaji wa mikakati ya vita.

Hilo la air defense systems Iran ilinunua za Urusi na China, na hazijasaidia almost lolote. Iran ilitakiwa inunue fighter jets hasa Su-35 za Urusi zingewasaidia sana ila Urusi wenyewe ndio marafiki wanafiki.
 
Sasa mkuu ata rushaje wakati hawashei mpaka ? Mfano umbali walio nao Iran na Marekani ndo ungekuwa wa Ukraine na Urusi je Ukraine ingeweza kuoshambulia ardhi ya Marekani?
Kwa hiyo migogoro hii miwili inatofautiana katika mkitadha wa kijografia na malengo na sio kiuwezo.

Nje ya mada kwa mtazamo wako unavyo ona huyu mtoto wa Khamenei anaweza kweli kuiongoza Iran?
Huo umbali ndio mojawapo kinachoitofautisha Marekani na Iran, na ndio kinachodhihirisha ubovu wa Urusi maana wapo karibu na Ukraine tofauti na mada na tittle yake.

Ayatollah mpya hajatangazwa rasmi, maana Assembly of Experts haijakaa kutokana na tishio la vita. Ila Mojtaba kijana mkubwa wa Khamenei anatajwa kama mrithi, inaonekana mazingira ya uchaguzi atapita na hasa IRGC inamtaka yeye.
Ingawa sio msomi wa juu kabisa kidini ila kisiasa ana uzoefu underground alikuwa anaendesha mambo kadhaa. Ni hardliner, misimamo kama ya baba yake hivyo simkubali sana kwa enzi za sasa ambazo zina maandamano, uchumi mbovu kabisa na vikwazo vingi. Atakuja kutaka consolidation of power jambo litakalotegemea kama ana uwezo sana au kama hana uwezo nchi inapata hasara kwa muda mrefu.

Wakati Ali Khamenei anachaguliwa alikuja kuwaunganisha watu, hakuwa mtu wa juu kabisa wala mwenye mizizi sana kama ambavyo mwanae alivyo sasa. Napendelea Ayatollah ajaye awe kama Khamenei alivyokuwa wakati anachaguliwa. Pia influence ya Ayatollah ipungue kiasi ili Rais, bunge, Guardian Council na Assembly of Experts viongeze maamuzi zaidi. Tatizo Ayatollah ndio kama anateua wote hao sasa ukileta mzoefu sana ni shida (maana atakuwa mdini lialia) na ukileta mgeni kabisa watamsumbua wazoefu.

Hata interim huyu Ayatollah Alireza Arafi bado simkubali sana naona ni hardliner, ila bora yake kuliko Mujtaba. Iranians wanataka mtu soft kidogo ambaye si msomi mkubwa wa kidini tu bali msomi labda wa sayansi au uchumi ili concentration yake iwe kukuza uchumi kupunguza ugumu wa maisha, kukuza teknolojia, biashara, standard of living ili baadae wajikusanye wakitaka kupigana na Israel. Sio sasa atokee kichwa ngumu waendelee kuumia.
 
Back
Top Bottom