Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Hii ni tofauti sana hauwezi linganisha, kule Urusi aliingia mazima mazima kwa kataifa jirani hapo, tena msafara haswa ila akaliwa za uso, lakini kwa hivi vita Iran, Marekani inapigana mbali sana na mpaka wake na inachezea angani tu hamna msafara wala nini na mpaka Sasa imeteka anga lote la Iran, imesambaratisha navy na air force yote ya Iran.
Viongozi wakuu wa Iran wamefyekwo, kilichosalia ni missile launchers ambazo zimefichwa maeneo mbali mbali na zinasakwa na kulipuliwa moja moja, zinasubiriwa zifyatue kisha zinasomwa na satellite na kupigwa.
Huu ndiyo Ubazazi na Udunya ambao nimekuwa nikiusema hapa muda mrefu.

War is waged on Objectives, if the Objectives are not accomplished then it's a waste of time.

Lengo kuu la Marekani kuvamia Iran lilikuwa ni Decapitation-Insurection-Collapse. Ilitakiwa saa hizi watu wawe wameingia barabarani wameshaipindua serikali na vikosi vya Marekani, Israel, UAE, Qatar, Kurd na NATO wameingia na kumalizia kazi dhidi ya Iran. Lengo kuu halijafanikiwa, kama kule Vietnam.

Tatizo jingine ambalo wewe hulitizami na unafanya ushabiki hapa ni kwamba Marekani ni tofauti na Urusi kwasababu anamiliki kambi za jeshi Middle-East yote. Kisheria kambi za jeshi ni kama Ubalozi, zinachukuliwa kama eneo la nchi (Territory of America). Ndiyo maana ukishambulia kambi ya jeshi unakuwa umetangaza vita dhidi ya nchi husika. Lakini jingine, vita hatupigani kwa kushindana kuua raia (Civilians) ambao wanalindwa na sheria, tunashindana kuua wanajeshi wanaopigana (Combatants).

Kisiasa utaweza kuona utaofauti kwasababu ninyi mnataka iwe Conventional Warfare, lakini ukweli ni kwamba hii ni ASYMETRIC WARFARE kama kule Vietnam na Afghanistan. Mwaka 1979 Urusi alivyovamia Afghanistani alifanya vilevile kama ambavyo Marekani amefanya kwa Maduro-Venezuela na kwa Ayatollah-Iran. Warusi walivamia Ikulu Kabul na kumuua Raisi wa nchi na viongozi (A Decapitation). Baadaye vita iliyotakiwa iwe ya wiki, ikaishia kuwa ya miaka 15, iliyojaa mauamivu.

Urusi alidhibiti anga lote la Afghanistani kwa ndege za kisasa zilizofanya mashambulizi, lakini hawakushinda vita. Waliua maelfu ya watu lakini lengo kuu la kuitawala Afghanistan halikufanikiwa. Marekani hata ajaze madege ukanda wote ule, tayari lengo la kwanza halijafanikiwa, na walau ungekuwa umesoma masuala ya kiusalama ungefahamu kwamba vita hatushindi kwa kupitia jeshi la anga (Air-Force), bali jeshi la ardhini (Army/Infantry) ambapo itatakiwa Marekani na Israel wavamie Iran nchi ambayo imezungukwa na milima kama Afghanistani.

Hivi umeiona hata ramani ya Iran, jinsi ilivyo kweli ???

Marekani akijidanganya kuvamia kijeshi Iran, aisee watachinjwa kama kuku. Kiufupi kama alishindwa kulitawala (Occupy) taifa la Iraq, dogo lenye watu milioni 20, ataweza kweli kulitawala taifa la Iran kubwa mara nne ya Iraq na lina watu milioni 100 ??? Hivi mnavyojibugi hivi huwa mnakuwa mmkunywa nini wajameni ??? Ati bro ???
 
Mkuu MALCOM LUMUMBA kwanza nikupe pole kwa maumivu ya kichwa unayopitia katika kipindi hiki cha vita. Nafikiri ulitegemea Iran iwe imelipua aircraft carrier ya Marekani huko Mediterania sea lakini mpaka sasa ni kipondo tu kinatembea. Kiuhalisia Iran inaona mambo ni magumu na baada ya wiki moja ya huu msako wananchi watajitoa mhanga kupambana na serikali ya kiimla ya Iran kwani mpaka sasa haina mkuu wa nchi na hata makamanda wakuu wa jeshi wameshakufa na kuna wasiwasi wa kuuawa kwa rais na wasaidizi wake wote. Kwa sasa Iran hata internet pia imezimwa siku ya sita leo na hili ni hatari kwa usalama wa taifa. Mkuu see you next
Tupo hapa,
Wiki ya kwanza ndiyo ishakata hivyo....
Wiki ingine ikiisha ntakuita hapa, lakini usikimbie.....
 
Hapa unalinganisha tembo na mbuzi kwenye uzito.

Russia imetimiza miaka minne tangu ianzishe mashambulizi dhidi ya Ukraine. Kwa kutumia vifaru, wanajeshi, helicopters, meli za kivita, bombers, fighter jets, submarines, missiles zikiwemo cruise, ballistic na hadi hypersonic, na silaha nyinginezo.

Marekani imeshambulia haina boots on ground, haina kifaru hata kimoja, inatumia missiles, ndege na meli sina hakika kama wametumia submarines mpaka sasa. Tofauti zao sasa:

1. Russia ina miaka minne (4), US haijatimiza mwezi.

2. Russia haijawahi miliki anga la Kiev, wala ndege yake kukatisha anga hilo walau mara moja katika miaka yote minne. US siku ya kwanza tu ndege zake zilifika Tehran na kila siku zinafika zinakotakiwa kufika popote ndani ya Iran. Ndoto kama hii kwa Russia haiwezekani.

3. Russia haijawahi muua mkuu wa majeshi, wala Rais, wala mkuu wa Air force, au wa Navy, au wa Army ya Ukraine. Upande wa Marekani hapa sitaji nitakukumbusha machungu.

4. Iran haijamuua General yeyote wa US, Ukraine imeua Russian Generals zaidi ya 15 kwenye mapigano.

5. Iran hajawahi shambulia mainland US. Wakati Ukraine anashambulia hadi ikulu ya Kremlin ya Urusi.

Hizo ni tofauti kubwa, mengine ni vita zina mambo yake. Ila aliyekutaarifu kuwa Marekani ameshindwa kummaliza Iran "kwa haraka" sijui ni nani.
Fuct
 
Hapa unalinganisha tembo na mbuzi kwenye uzito.

Russia imetimiza miaka minne tangu ianzishe mashambulizi dhidi ya Ukraine. Kwa kutumia vifaru, wanajeshi, helicopters, meli za kivita, bombers, fighter jets, submarines, missiles zikiwemo cruise, ballistic na hadi hypersonic, na silaha nyinginezo.

Marekani imeshambulia haina boots on ground, haina kifaru hata kimoja, inatumia missiles, ndege na meli sina hakika kama wametumia submarines mpaka sasa. Tofauti zao sasa:

1. Russia ina miaka minne (4), US haijatimiza mwezi.

2. Russia haijawahi miliki anga la Kiev, wala ndege yake kukatisha anga hilo walau mara moja katika miaka yote minne. US siku ya kwanza tu ndege zake zilifika Tehran na kila siku zinafika zinakotakiwa kufika popote ndani ya Iran. Ndoto kama hii kwa Russia haiwezekani.

3. Russia haijawahi muua mkuu wa majeshi, wala Rais, wala mkuu wa Air force, au wa Navy, au wa Army ya Ukraine. Upande wa Marekani hapa sitaji nitakukumbusha machungu.

4. Iran haijamuua General yeyote wa US, Ukraine imeua Russian Generals zaidi ya 15 kwenye mapigano.

5. Iran hajawahi shambulia mainland US. Wakati Ukraine anashambulia hadi ikulu ya Kremlin ya Urusi.

Hizo ni tofauti kubwa, mengine ni vita zina mambo yake. Ila aliyekutaarifu kuwa Marekani ameshindwa kummaliza Iran "kwa haraka" sijui ni nani.
HATA wewe unalinganisha visivyolinanishika,hakuna kitu Cha maana ulichoandika.

1) Iran Ina vikwazo Kwa zaidi ya miaka 40,wakati Ukraine Haina vikwazo vyovyote.

2) Ukraine ilikua inafundishwa na NATO kwa miaka zaidi ya minane ,wakati Iran ikiwa Iko vikwazoni

3) wiki ya kwanza TU ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ilikaribia kuingia Kiev,west wakaidanganya Urusi kua Ukraine Iko tayari kwa mazungumzo,wakaenda uturuki kuongea kumbe NATO wanajipanga kumsaidia Ukraine,
Ndio maana Hadi Leo NATO wapo Ukraine .
Wakati Iran anahangaika peke yake.
4) Sio mpango wa Urusi kumuua Zelensky wala Regime change Ukraine Bali Ukraine isijiunge NATO na haijajiunga.
Wakati Israel na USA waliidanganya Iran kua wiki ijayo mazungumzo yataendelea ndio ikapelekea Viongozi wa Iran kutoka na hofu ya kuvamiwa walikaa au waliishi Kwa Imani kua wiki ijayo wataemdelea na mazungumzo,walijiachia,kumbe wenzao ni waongo na hawakua waaminifu,walavamia na kumuua Ayatollah na wenzake,wakati Israel na USA wakifanya hayo Benjamin Netanyahu alikimbilia ujerumani kujificha.
5)Iran sera Yao sio kuua Viongozi wa nchi nyingine ,wakati Isarel sera yake ni kuua Viongozi wa nchi maadui
Vivyo hivyo kwa Urusi na Ukraine Urusi Haina mpango wa kumuua Zelensky wala viongozi wa Ukraine lkn Ukraine na west sera Yao ni kuua Viongozi wa nchi nyingine(Ugaidi).

6) Vita vya Urusi imechukua miaka minne Urusi ikipigana na Ukraine inayosaidiawa na All collective west,wakati vita vya Israel-USA - Iran bado haijaisha,tusubiri itaisha lini ndio tuone ulinganifu.wakati Iran ikipigana peke yake dhidi ya Israel Marekani Qartari,Sound Arabia, Jordan,UAE, Bahrain,n.k ambazo zilisaidia sana kuangusha makombora ya iran

7) Iran haijashambulia marekani moja kwa moja kwa sababu za kijiografia na Irani Haina uwezo huo,lkn imepiga Kambi zote za jeshi za USA na ndani ya ardhi ya Israel,hii maana yake kama Marekani ingekua ilipo Turkyl eo hii nayo ingepigwa.
Hata hivyo Kambi za kijeshi za USA ni sehemu ya Marekani kijeshi hivyo zingeachwa zingeshiriki kuipiga Irani,ndio lengo la kuwepo makambi hayo kuirahisishia marekani kuishambulia nchi jirani na Kambi hizo.
Lakini kwa bahati mbaya kwa marekani wanajeshi wote wa USA waliokua kwenye Kambi hizo wamezikimbia kabla na baada yavkupigwa,hivyo lengo la kujenga kabisa hizo limefeli aubhalijasaidia kitu.
8) Abraham Lincoln imeshambuliwa na ikahamishwa au kukimbizwa,hivyo Nayo umeshindwa kufanya kazi iliyokusudiwa au iliyosababiswa kupelekwa ghuba.
9)kama alivyosema mtoa mada toka Dunia hii iumbwe hii ni mara ya pili baada ya Miaka mingi kwa marekani kupigwa kwa miundombinu yake ya kijeshi silaha na vifaa vingine kama rada viwanja vya ndege na bandari za melivita na kuharibiwa vibaya kama kama ilivyotokea ndani ya siku nne TU,baada ya Pearl Harbour attack.
10) katika histotia ya Dunia hakuna kipindi ambacho Marekani ameomba msaada kijeshi kama mwaka huu,na hata kaomba Msaada wa viwanja vya kurushia ndege zake na kanyimwa na Hispania,Sasa najiuliza Kambi zake za middle east zimemsaidia Nini na alizijenga za Nini?
Katika historia ya USA haijawahi kushindwa kuokoa raia wake kwa maelfu waliokwama middle east kama kipindi hiki.,wamekwama aisee.maana kule ghuba ndege za kiraia zimeshindwa kuruka.
Kwa kifupi Iran kazua balaa kubwa.
11) Kuna uzuiaji mkubwa wa habari za Iran inaposhambulia Israel na USA,habari zinatoka kwa kuchujwa mno tofauti na habari zinazorushwa kutoka Vyombo vya magharibi zikiishambulia Iran.
Tutayajua mengi baadae.
12) Sina uhakika lkn inasemwa USA aliiomba Italy ikaiombe Iran wayamalize iache vita ,Iran ikakataa kumaliza vita.
 
Hapa unalinganisha tembo na mbuzi kwenye uzito.

Russia imetimiza miaka minne tangu ianzishe mashambulizi dhidi ya Ukraine. Kwa kutumia vifaru, wanajeshi, helicopters, meli za kivita, bombers, fighter jets, submarines, missiles zikiwemo cruise, ballistic na hadi hypersonic, na silaha nyinginezo.

Marekani imeshambulia haina boots on ground, haina kifaru hata kimoja, inatumia missiles, ndege na meli sina hakika kama wametumia submarines mpaka sasa. Tofauti zao sasa:

1. Russia ina miaka minne (4), US haijatimiza mwezi.

2. Russia haijawahi miliki anga la Kiev, wala ndege yake kukatisha anga hilo walau mara moja katika miaka yote minne. US siku ya kwanza tu ndege zake zilifika Tehran na kila siku zinafika zinakotakiwa kufika popote ndani ya Iran. Ndoto kama hii kwa Russia haiwezekani.

3. Russia haijawahi muua mkuu wa majeshi, wala Rais, wala mkuu wa Air force, au wa Navy, au wa Army ya Ukraine. Upande wa Marekani hapa sitaji nitakukumbusha machungu.

4. Iran haijamuua General yeyote wa US, Ukraine imeua Russian Generals zaidi ya 15 kwenye mapigano.

5. Iran hajawahi shambulia mainland US. Wakati Ukraine anashambulia hadi ikulu ya Kremlin ya Urusi.

Hizo ni tofauti kubwa, mengine ni vita zina mambo yake. Ila aliyekutaarifu kuwa Marekani ameshindwa kummaliza Iran "kwa haraka" sijui ni nani.
Bwana Armata, Marekani ya leo 2026 haina nguvu kama Marekani ya 1964.

Marekani ya mwaka 1964 was a formidable military behemoth lakini alishindwa Vietnam.

Anga lote la Vietnam lilikuwa limejaa ndege za Marekani huku chini wamejaa maelfu ya askari.

Marekani alilipua hivihivi na kufutilia vijiji vya watu ambapo mwishowe aliuawa watu milioni 4.

Alifanya yote lakini akashindwa....

Wanachoshindana sasa Marekani na Iran ni PAIN-ABSORPTION, ambapo kweli Iran katandikwa kelubu za kutosha na kutisha. Haya ambayo Marekani kafanya Iran, yangefanyika kwingine nchi ingekuwa ishaparanganyika. Mpaka sasa Iran katushangaza, serikali yote haipo lakini bado wanapigana vita. Sasa Marekani naye ameguswa, na Iran analenga kufanya kilekile alichofanya Vietnam (Kill many American Boys and send them home in body bags). Iran akiweza kuua hata Wamarekani 5000 tu, kelele zitatokea nyingi mno Marekani na Donald Trump na Pete Hegseth watashughulikiwa ipasavyo.

Ponapona ya Marekani ni kushinda hii vita, jambo ambalo haliwezi kufanyika kwa kuua majenerali. Mwaka 1934 kwenye Chinese-Civil War, Chiang-Kai Shek aliua maelfu ya wanajeshi wa Mao Zedong wakiwemo majenerali lakini yote hayo mwisho wake alichoka yeye, maana wakomunisti walikuwa wamejikataa, wakamshinda akakimbilia Taiwani mwaka 1949.

Likivuka hili wiki tu, wiki ijayo utatembea hapo Dar kwa mguu nakwambia. Mbaya zaidi hadi kule USA, Europe kutakuwa na hali mbaya maana Iran anashambulia Energy Infrastructure kuhakikisha kwamba Attack zake zinakuwa na The Multiplier Effect. Wamarekani wako mbali na Iran, lakini Iran has sent them A War Bill. Mfumuko wa bei utakaotokea Wamarekani watakuwa wa kwanza kuumia. Tena sanaaa.
 
Kama Russia walifanya makosa kumshambulia jirani yake ambaye ni Ukraine

Naomba kuuliza Wewe Malcolm ulitaka Russia wafanye Nini wakati majirani zao hao Ukraine walikuwa wana mpango wa kujiunga katika uwanachama wa NATO !?? Je alipaswa kuwaacha wajiunge !?

Kama ange waacha wajiunge vipi kuhusu Hali ya usalama wa Russia ingekuwaje !?

Naomba muongozo
Kuvamia taifa jingine huru, kijeshi kwasababu linafanya maamuzi yake kisiasa ni kosa kisheria.

Urusi mwenyewe aliwaruhusu Wayukraini watoke kwenye Muungano mwaka 1991.

Kinachofanyika hapa ni siasa za mataifa makubwa (Great Power Politics) ambapo ukweli mchungu ni kwamba sheria inakataza, ila uhalisia ni kitu kingine, kwamba ukiingilia maslahi ya taifa kubwa halafu wewe ni kitaifa kidogo ndiyo madhara ambayo yanaikuta Ukraine. Sheria inamlinda Ukraine, lakini uhalisia wa siasa za dunia una taswira nyingine kabisa. Marekani na NATO walimponza Ukraine, naye akijidanganya akaingia mazima, mwishowe yakamkuta.

Taiwan na Japan wasipojifunza watakuja kupigwa na kitu kizito nao wasiamini.....

 
Hii ni tofauti sana hauwezi linganisha, kule Urusi aliingia mazima mazima kwa kataifa jirani hapo, tena msafara haswa ila akaliwa za uso, lakini kwa hivi vita Iran, Marekani inapigana mbali sana na mpaka wake na inachezea angani tu hamna msafara wala nini na mpaka Sasa imeteka anga lote la Iran, imesambaratisha navy na air force yote ya Iran.
Viongozi wakuu wa Iran wamefyekwo, kilichosalia ni missile launchers ambazo zimefichwa maeneo mbali mbali na zinasakwa na kulipuliwa moja moja, zinasubiriwa zifyatue kisha zinasomwa na satellite na kupigwa.
Umenena vyema, mimi nashangaa Mtanzania anayeongozwa na ccm akawa na maarifa ya kusoma ramani ya mapambano kumshinda Trump aliyezungukwa na CIA na MOSSAD juu.

CIA na MOSSAD zikae chini for years waje na suluhisho halafu mtu uje tu uone US na Israel zimekosea, HAPANA.
 
Kuvamia taifa jingine huru, kijeshi kwasababu linafanya maamuzi yake kisiasa ni kosa kisheria.

Urusi mwenyewe aliwaruhusu Wayukraini watoke kwenye Muungano mwaka 1991.

Kinachofanyika hapa ni siasa za mataifa makubwa (Great Power Politics) ambapo ukweli mchungu ni kwamba sheria inakataza, ila uhalisia ni kitu kingine, kwamba ukiingilia maslahi ya taifa kubwa halafu wewe ni kitaifa kidogo ndiyo madhara ambayo yanaikuta Ukraine. Sheria inamlinda Ukraine, lakini uhalisia wa siasa za dunia una taswira nyingine kabisa. Marekani na NATO walimponza Ukraine, naye akijidanganya akaingia mazima, mwishowe yakamkuta.

Taiwan na Japan wasipojifunza watakuja kupigwa na kitu kizito nao wasiamini.....

Wewe jamaa yangu unachekesha sana! Yaani unadiriki kabisa kuiita japani kuwa ni taifa dogo?
Kama eneo ndiyo ukubwa wa taifa basi Tanzania ni taifa kubwa kuliko taifa lolote la ulaya. Japani ni taifa la 3 kwa ukubwa kiuchumi duniani na lina watu milioni 125 how unasema ni taifa dogo?
 
Hapo kinachoonekana ni kwamba "Nisiumie peke yangu" ndicho anachokifanya Iran, kupigwa anajua atapigwa lakini "tutapigana", vita haiwezi kuisha kinyonge na Hili Nadhani wamejiandaa nalo...

Lengo la hii vita ni kuhakikisha Israel anabakia kuwa yeye ndio superpower wa middle East, lisiwepo taifa lolote lile la kuchallenge Israel, hii vita US alitarajia kuingia lakini si Kwa style ya namna hii, Kwa mara nyingine tena Israel anamuingiza US kwenye vita Kwa namna anavyotaka.

Hii vita siyo rahisi kabisa, Kila Aina ya propaganda itapigwa lakini ukweli utajulikana baada ya miezi kadhaa mbele na Hali ikiendelea hivi hivi basi masiku ya mbele kutakuwa na mabadiliko makubwa ya malengo ya hii vita.
Iran yuko kwao lakini mashambulizi yake yote yatamfikia kila Mmarekani kule Hollywood na Chicago. Mashambulizi ya Iran mbali tu na kuua wanajeshi, yana The Economic Multiplier Effect kwasababu hii vita inapiganwa World's Major Energy Choke-Point. Sasa mabazazi na madunya, yenyewe yanadhani kwamba Iran anataka kuua wanajeshi tu. Iran anataka kuua wanajeshi, lakini kubwa zaidi ni kuvuruga mlolongo mzima wa usalama wa nishati ya dunia (World's Energy Security).

Kama ikiendelea hivi, hadi wale Wamarekani wa Tandale watamlaani Donald Trump na Benjamin Netanyahu kwa kuvamia Iran. Mfereji wa Hormuz ukifungwa tu, na miundombinu ya mafuta ya Saudi Arabia, UAE na Qatar ikalipuliwa kule Marekani kutakuwa na madhara makubwa mno kiuchumi, hasa kwenye mzunguko wa dola (Dollar Circulation).

Maumivu yakiwa makubwa, watakaolaumiwa ni WAYAHUDI WA MAREKENI (The Israel Lobby) na Netanyahu kwasababu ukisikiliza kina Tucker Carlson wanalaumu hii vita kwa Israel na magenge ya Wayahudi wa Marekani ambao wanailazimisha Marekani iingie vitani ilhali hawana maslahi huko.
 
Umenena vyema, mimi nashangaa Mtanzania anayeongozwa na ccm akawa na maarifa ya kusoma ramani ya mapambano kumshinda Trump aliyezungukwa na CIA na MOSSAD juu.

CIA na MOSSAD zikae chini for years waje na suluhisho halafu mtu uje tu uone US na Israel zimekosea, HAPANA.
Mtanzania mwenye akili ni lazima afahamu kwamba CIA na MOSSAD siyo makampuni ya mafuta.

Pia Mtanzania mwenye akili ni lazima afahamu kwamba uchumi wa dunia unaendeshwa na Fossil Fuels, hivyo kinachotokea Ghuba ya Uajemi hakihitaji PhD in Economics kufahamu kwamba wiki zijazo hata yeye mwenyewe anaweza akawa anapiga jalamba kutembea ya mguu kutoka Mbezi-Beach hadi Mwenge.

Akili ni nywele, kila mtu ana zake....
 
US kaingia cha kike safari hii
Karuka sarakasi huku kavaa taulo.....

Ukweli mchungu ni kwamba, The Persian Gulf (Ghuba ya Uajemi) ni eneo ambalo linatuwezesha hata mimi na wewe kuweza kuwasiliana hivi hapa mtandaoni. Ni eneo ambalo linaathiri maisha yetu kwa kiwango kikubwa kupita maelezo. Tatizo ni kwamba Mabazazi na Madunya ya humu ndani yanadhania kila kitu ni ushabiki ilhali hayafahamu kwamba wahanga wa kwanza wa Energy Crisis watakuwa wao kwasababu ya mfumuko wa bei (Inflation) na uhaba wa dola (Dollar Scarcity) kwasababu mafuta ni moja ya bidhaa inayoongozwa kusambaza dolla hapa duniani.

Kiukweli Trump kacheza vibaya mno, na aliyemshauri (Netanyahu) katulia pembeni....
 
Wewe jamaa yangu unachekesha sana! Yaani unadiriki kabisa kuiita japani kuwa ni taifa dogo?
Kama eneo ndiyo ukubwa wa taifa basi Tanzania ni taifa kubwa kuliko taifa lolote la ulaya. Japani ni taifa la 3 kwa ukubwa kiuchumi duniani na lina watu milioni 125 how unasema ni taifa dogo?
Unachekesha wewe ambaye umeshindwa kusoma kwa ufahamu.

Japan kwa Uchina ni taifa dogo mno.

Japana kwa Uchina ni dogo kiuchumi, dogo kiukubwa, dogo kieneo, dogo kitamaduni na dogo kiumri.

Japan ni kubwa kwako wewe mtanganyika chogo a.k.a Bazazi Bin Dunya ila dogo kwa Uchina....
 
kwenye namba 5.
Nilitegemea ungetumia akili kidogo kufanya comparison ya kijiografia kati ya IRAN na USA kulinganisha RUSIA na UKRAINE..
Niliiacha kimtego ili mdhihirishe uvivu wa Urusi. Ukitumia akili ya kijiografia unaona Urusi ilivyo na advantage kwenye kuishambulia Ukraine.

Marekani inasafiri kwa ndege na meli kilomita 7,000 kuifuata Iran, wakati Urusi hata kwa miguu inaifikia Ukraine, mwaka wa nne huu.
 
Muda huwa ni mwalimu mzuri sana.

Nakumbuka mabazazi na madunya wa humu ndani mnamo tarehe 24 February 2026 siku ambayo Urusi alivamia Ukraine walinitafuta na kunisimanga sana. Wengine walidiriki hadi kukashifu taaluma yangu. Walishangaa kwamba kwanini Urusi ameshindwa kuivamia Ukraine na kuimaliza kwa haraka ilhali anajiita taifa kubwa (Super-Power). Niliwaambia vijana wa humu ndani kwamba Urusi alifanya makosa kuvamia jirani yake na kuna mambo alikosea, lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)

Mpaka 2026, Urusi na Ukraine wanapigana, huku Ukraine wakiwa wameumizwa zaidi. Urusi anatumia fedha nyingi sana kwenye vita na usalama, jambo ambalo siku vita ikiisha litazua matatizo makubwa mno kwasababu watu wengi watakosa ajira ambazo wanazifanya sasa. Pia kuna mambo kadha wa kadha. Sasa huu ni utangulizi tu:

Naomba niwaulize ninyi vijana wa humu ndani, kwanini Marekani (The Only Global Super-Power) ameshindwa kulimaliza taifa la Iran ndani ya wiki kama alivyofanya Afghanistani au Venezuela ??? Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).

Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi. Ila sasa yametokea tofauti. Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000. Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.

Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.

SASA IRAN ANAPAMBANAJE: Mwaka 2018 nakumbuka kuna uzi wangu nilifurumushiwa matusi na mabazazi na madunya wa humu ndani, nilioandika kuhusu dhana ya ASYMETRIC WARFARE. Dhana hii inafanya kazi pale ambapo taifa dogo au kikundi kidogo kinapambana na taifa kubwa. Lengo siyo kutaka kupambana CONVENTIONAL WARFARE, ila ni kumsababishia maumivu makubwa yule aliye mkubwa kiasi cha kufanya akimbie. Mfano halisi, ni USSR vs Mujahedeen au USA vs Vietcong.

Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???

MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:

Mosi
, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika. Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani, nani anaamini kabisa kwamba kambi za Marekani zilizopo South-Korea, Philippines, Japan na Guam zitakuwa salama, kama tu kambi kubwa za Marekani barani Asia zimelipuliwa juzi na jana na Iran, taifa ambalo halina nguvu kama Uchina. Kiukweli, Marekani alizichanga karata vibaya na yanamtokea puani.

Pili, Urusi atapata nguvu kubwa kutokana na bei ya mafuta kupanda. Saudi Arabia, UAE, Oman, Qatar na Bahrain wanaogopa kupitisha mafuta Mfereji wa Hormuz, ambao kwa siku mapipa milioni 17 yanapita. Vita ikiendelea hivi na Iran akafanikiwa kufunga kabisa mfereji, basi mafuta ya Ulaya na Asia itabidi yapatikane Urusi ambako kuna vikwazo. Juzi Vladmir Putin kasema anafikiria kusitisha kabisa kuuza gesi Ulaya. Sasa USA na EU watabakiwa na maamuzi kama haya: Ondoa vikwazo ili tupate nishati kutoka Urusi. Bahati mbaya wakiondoa vikwazo Ukraine ndiyo kwaheri.

Tatu, Urusi atapenda kulipiza alichofanyiwa Ukraine. Hii ndiyo tabia kuu ya Urusi. Niguse-Ninuke. Marekani akitingwa kule Iran, basi lazima atapunguza kuangalia Ukraine. Sasa itabidi silaha zote zinazozalishwa zienda Persian Gulf (Ghuba ya Uajemi) siyo Ukraine. Urusi na Uchina wanaweza kuigeuza Iran, VIETNAM 2 endepo Marekani akiendelea hivi bila kuomba msamaha. Bahati mbaya sana kwa alichokifanya Donald Trump, Marekani ikirudi nyuma kama kipindi cha Twelve Days War mwaka 2024, basi ndiyo mwisho wa siasa za MAGA na Trump, na anaweza kufungwa kwasababu ameanzisha vita bila kibali cha Bunge.

Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???

Tano, THE COLLAPSE OF THE LAW OF NEUTRALITY. Katika sheria za kimataifa hasa wakati wa vita, The Law of Neutrality huyalinda mataifa ambayo hayapambani moja kwa moja, hata kama yanakuwa yanauza silaha kwa adui au kuwa na kambi za kijeshi ambazo hazitumiki kijeshi kushambulia adui. Kitendo cha Marekani kuvamia Iran bila sababu ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Hata Iran kuanza kuvamia Saudi-Arabia, UAE na Qatar ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Lakini Marekani hawezi kulalamika katika hili kwasababu yeye ndiye mvunjifu sugu wa sheria za kimataifa. Sheria za kimataifa ili zifuatwe na mataifa madogo, inategemea sana mataifa makubwa.

Hili lisipoangaliwa sana, tutaamka siku na kukuta Urusi kaanza kulipua Poland na Ujerumani kisa tu kuna kambi za jeshi za Marekani, hata kama hazitumiki kushambulia. Huku ndiko tunaelekea. Hivyo tukishafahamu haya, vitaifa masikini kama Tanzania vijiepushe na tabia za kupenda kujipendekeza kwa mataifa makubwa kama Uchina, Urusi na Marekani. Dunia inaelekea kubaya na kama tukitaka kuvuka itabidi kweli tusifungamane na upande wowote. Sasa wale wanopenda pesa za waarabu kisa ni wenzetu katika IMANI wakiendeleza tabia zao za kusajili manowari kule Zenji, wataliletea hili taifa matatizo makubwa mno. Tena kipindi hiki ukipigwa huna pakusemea maana kila mtu anapambana lwake.

==============================================================================

HALAFU KUNA MABAZAZI mengine yanasema INTERNATIONAL LAW IMEKUFA, haya nitayajibu baadaye.HAYANA AKILI

Iran kwa sasa ipo kwenye wakati mgumu mno.

The regime is focused on surviving not winning.

T14 Armata
 
Hao Mabazazi na Madunya ni wanafiki wakubwa humu jukwaani na Nje ya jukwaa.
Wakati Urusi inaivamia Ukraine ilivyokua inakaribia kujiunga na NATO ili kuizuia isijiunge,Mabazazi na Madunya waliilaani Urusi na kusema Ukraine ni Taifa huru Urusi iache uonevu.

Leo hii USA na Israel zimeivamia Iran kuizuia etivisimiliki nyukikia Mabazazi na Madunya hawajalaani na wanaihesabia Iran kua muda si mrefu itaanguka na kuiona Marekani na Israel kua Ina haki au Haina makosa ya kuivamia Iran
Hii Dunia Ina watu wanafiki Hadi wananuka uanfiki.
Mabazazi na Madunya wa humu ndani akili zao ziko likizo....

Mimi nimekuwa nao humu ndani tokea mwaka 2012 na nimesema nao sana.....

Walinitukana sana miaka ya 2016-2018 kuhusu siasa za dunia, mwaka 2022 wakazidisha......

Ila sasa naona wanaanza kuelewa kwamba International Politics is not a Masturbation Contest....

International Politics Affects Their Daily Lives....But these fools can't comprehend the gravity...

Binafsi napenda hii vita iendelee ili Mabazazi na Madunya ya Mbezi, Kawe, Mwenge na Masaki yajifunze, pale siku watapoambiwa wapaki gari nyumbani, huku Google ikiwa haifanyi kazi kisa Data Centres zimelipuliwa. Kiukweli hii vita ni ya kifala sanaa...
 
Inshengoma is just a Russia- Obsessed Mofo.
He supports anything that opposes the West.
If Sheitwan come out today and stand against the west,Inshengoma would definitely appoint himself as his favorite demon.
in other hand;
A Muslim is some that reads the Quran,An ex Muslim is some that understands the Quran.
When you throw a stone to a pack of dogs, the first one to holler is a bitch hit by the stone.....
 
Back
Top Bottom