Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Kwanini Marekani ameshindwa kuimaliza Iran haraka?

Bwana Armata, Marekani ya leo 2026 haina nguvu kama Marekani ya 1964.

Marekani ya mwaka 1964 was a formidable military behemoth lakini alishindwa Vietnam.

Anga lote la Vietnam lilikuwa limejaa ndege za Marekani huku chini wamejaa maelfu ya askari.

Marekani alilipua hivihivi na kufutilia vijiji vya watu ambapo mwishowe aliuawa watu milioni 4.

Alifanya yote lakini akashindwa....

Wanachoshindana sasa Marekani na Iran ni PAIN-ABSORPTION, ambapo kweli Iran katandikwa kelubu za kutosha na kutisha. Haya ambayo Marekani kafanya Iran, yangefanyika kwingine nchi ingekuwa ishaparanganyika. Mpaka sasa Iran katushangaza, serikali yote haipo lakini bado wanapigana vita. Sasa Marekani naye ameguswa, na Iran analenga kufanya kilekile alichofanya Vietnam (Kill many American Boys and send them home in body bags). Iran akiweza kuua hata Wamarekani 5000 tu, kelele zitatokea nyingi mno Marekani na Donald Trump na Pete Hegseth watashughulikiwa ipasavyo.

Ponapona ya Marekani ni kushinda hii vita, jambo ambalo haliwezi kufanyika kwa kuua majenerali. Mwaka 1934 kwenye Chinese-Civil War, Chiang-Kai Shek aliua maelfu ya wanajeshi wa Mao Zedong wakiwemo majenerali lakini yote hayo mwisho wake alichoka yeye, maana wakomunisti walikuwa wamejikataa, wakamshinda akakimbilia Taiwani mwaka 1949.

Likivuka hili wiki tu, wiki ijayo utatembea hapo Dar kwa mguu nakwambia. Mbaya zaidi hadi kule USA, Europe kutakuwa na hali mbaya maana Iran anashambulia Energy Infrastructure kuhakikisha kwamba Attack zake zinakuwa na The Multiplier Effect. Wamarekani wako mbali na Iran, lakini Iran has sent them A War Bill. Mfumuko wa bei utakaotokea Wamarekani watakuwa wa kwanza kuumia. Tena sanaaa.
Mfano wako uliotumua wa Vietnam hiyo nchi imekuwa ya kibepari na kuna uwekezaji wa Wamarekani wenyewe na Wachina wanawekeza kwa wingi. Chanzo cha vita ile ni Marekani kutetea ubepari ambao ndio upo kwa sasa, kwahiyo mwisho wa yote sera ya Marekani ndio imeshinda.

Mimi siungi mkono Marekani kuishambulia Iran, ila kulinganisha failure ya Urusi kwa miaka minne dhidi ya mafanikio ya Marekani ndani ya mwezi ni makosa.
 
Niliiacha kimtego ili mdhihirishe uvivu wa Urusi. Ukitumia akili ya kijiografia unaona Urusi ilivyo na advantage kwenye kuishambulia Ukraine.

Marekani inasafiri kwa ndege na meli kilomita 7,000 kuifuata Iran, wakati Urusi hata kwa miguu inaifikia Ukraine, mwaka wa nne huu.
Marekani ana military base ngapi ? Na urusi anazo ngapi na utaje location zake.

Acha ushabiki maandazi mkuu..
 
Marekani hawezi pigana na China kwa vita yoyote ile full stop nimefuta mtazamo wangu wa awali juu ya nguvu na uwezo wa Marekani.
Hongera sana...

Ila ukweli haubadiliki kwamba Marekani ndiyo taifa lenye nguvu kijeshi duniani tangu historia ya binadamu ianze. Kiukweli Marekani lina nguvu mno hasahasa kwenye kipimo cha CONVENTIONAL WARFARE. Tatizo linakuja kwamba vita inategemea mambo mengi sana kushinda, siyo tu silaha na uwezo wa kiuchumi. Marekani wakati anavamia Vietnam mwaka 1964 alikuwa na jeshi linalotisha kuliko hili la leo, na bado akashindwa vita. War is a tool of state politics.

Vita inaweza ikapiganwa vizuri lakini siasa za nchi au dunia zikachangia vita kuisha vibaya. Huu mfano ndiyo aliwahi kusema Albert Einstein "You win the war,but lose the peace". Marekani Vietnam aliua watu milioni 4, huku Vietnam ikiua Wamarekani elfu 60. Ukiwa na akili ya Kibabazi na Kidunya unaweza kusema Marekani ndiyo kashinda vita, bila kuangalia madhara ya kisiasa nchini kwake na duniani kote.

Hili ndilo linasababisha vita zitegemee sana PROPAGANDA ili PUBLIC OPINION iwe upande wao. Bahati mbaya Donald Trump na Netanyahu hawakusoma alama za nyakati. Wamarekani wengi hasa MAGA walimchagua Trump kwa ahadi ya kukomesha vita na kutojihusisha kabisa na Middle-East. Ilikuwa ni America First. Sasa MAGA imevurugika, hadi Tucker Carlson na Candace Owens wanamponda Trump, hivi unadhani hii vita ikiendelea hivi na watu wakaanza kuona mfumuko wa bei na maiti za watoto wao, wataelewa chochote hata kama Marekani anaua viongozi wa Iran kila siku ???

Leo hii ukimchukua Mwakinyo akapigana na Wema Sepetu, halafu Mwakinyo akamchapa kweli Wema Sepetu ngumi za kichwa, ila baadaye Wema Sepetu akafanikiwa kumpiga ngumi moja tu ya pua, na Mwakinyo damu zikaanza kutoka, wewe unadhani watu watazingatia ngumi za kichwa alizopigwa Wema Sepetu ??? A Bleeding Nose, is enough to make Mwakinyo flinch and lose the entire fight...
 
Umenena vyema, mimi nashangaa Mtanzania anayeongozwa na ccm akawa na maarifa ya kusoma ramani ya mapambano kumshinda Trump aliyezungukwa na CIA na MOSSAD juu.

CIA na MOSSAD zikae chini for years waje na suluhisho halafu mtu uje tu uone US na Israel zimekosea, HAPANA.
Teh teh 😃 😃 nyie wabongo bhana .

Acheni kujidharau kiwango hicho.
 
Mfano wako uliotumua wa Vietnam hiyo nchi imekuwa ya kibepari na kuna uwekezaji wa Wamarekani wenyewe na Wachina wanawekeza kwa wingi. Chanzo cha vita ile ni Marekani kutetea ubepari ambao ndio upo kwa sasa, kwahiyo mwisho wa yote sera ya Marekani ndio imeshinda.

Mimi siungi mkono Marekani kuishambulia Iran, ila kulinganisha failure ya Urusi kwa miaka minne dhidi ya mafanikio ya Marekani ndani ya mwezi ni makosa.
Marekani hakwenda Vietnam kupeleka Ubepari bali alikwenda kutengeneza koloni akashindwa. Vietnam (Indochina) lilikuwa koloni la Mfaransa na alivyotoka Marekani akataka kwenda yeye ila bahati mbaya kina Stalin walikuwa washamuwahi. Kafika kakuta Wakomunisti wako tokea mwaka 1930 na wamesoma Urusi, huku wengine wakiwa veterans wa WW2.

Pili, Vietnam siyo taifa la Kibepari (A Capitalist Economy) ni taifa la Kikomunisti (A Communist State) ambalo limeruhusu mfumo wa masoko uliodhibitiwa (Controlled Market) kama Uchina. Kilichobadilika Vietnam ni umiliki wa mali tu na masoko. Siasa na Utawala ni uleule tokea 1930 chini ya Comrade Ho Chi Minh.
 
Marekani ana military base ngapi ? Na urusi anazo ngapi na utaje location zake.

Acha ushabiki maandazi mkuu..
Suala la Urusi kutokuwa na military bases za kutosha kuweza kupigana na jirani Ukraine ndio uvivu wenyewe ninaosema hapa. Mbona unaniunga mkono kwa kunipinga mkuu.

Kama Urusi ilijua haina bases za kutosha ingeacha, yanini kuanzisha mwenyewe kurusha ngumi alafu mkipigana unalamika huna nguvu za kutosha. Tangu mwanzo si ungeacha sasa.
 
Jmn kama haupo vizuri kichwan kwenye huu uzi usichangie...mnakula za uso vibaya mno 🤣

Wacheni mihemko ya umarekan wa buza.

MALCOM...Tuendee baba.
Endelea kudanganywa sasa yaani mtu mwenye akili timamu unaweza kukubali kabisa kuwa Iran ameiwin hii vita? Iran leo wanasema Marekani imeua askari wake wadogo kwenye meli ya kijeshi bahari ya hindi hivyo itaenda mahakamani? Aseeee
 
Muda huwa ni mwalimu mzuri sana.

Nakumbuka mabazazi na madunya wa humu ndani mnamo tarehe 24 February 2026 siku ambayo Urusi alivamia Ukraine walinitafuta na kunisimanga sana. Wengine walidiriki hadi kukashifu taaluma yangu. Walishangaa kwamba kwanini Urusi ameshindwa kuivamia Ukraine na kuimaliza kwa haraka ilhali anajiita taifa kubwa (Super-Power). Niliwaambia vijana wa humu ndani kwamba Urusi alifanya makosa kuvamia jirani yake na kuna mambo alikosea, lakini kusema kwamba NATO+EU wataiangusha ni jambo lisilowezekana. Mataifa makubwa huwa yanafanya makosa pia (Political Blunders)

Mpaka 2026, Urusi na Ukraine wanapigana, huku Ukraine wakiwa wameumizwa zaidi. Urusi anatumia fedha nyingi sana kwenye vita na usalama, jambo ambalo siku vita ikiisha litazua matatizo makubwa mno kwasababu watu wengi watakosa ajira ambazo wanazifanya sasa. Pia kuna mambo kadha wa kadha. Sasa huu ni utangulizi tu:

Naomba niwaulize ninyi vijana wa humu ndani, kwanini Marekani (The Only Global Super-Power) ameshindwa kulimaliza taifa la Iran ndani ya wiki kama alivyofanya Afghanistani au Venezuela ??? Fahamuni tu kwamba hivi vita hapigani Marekani peke yake bali anasaidiwa na Israeli na washirika wengine kama Australia ambao imejulikana hivi karibuni kwamba walisaidia kuzamisha manowari za Iran. Hapo kuna Saudi Arabia, Jordan, Qatar, Bahrain, UAE, Azerbaijan na Mgambo wa kikurdi (kurdish Militia).

Donald J Trump alisema ni siku nne tu baada ya Ayatollah kulambishwa mchanga basi, Iran ingekuwa kaputi. Ila sasa yametokea tofauti. Marekani kweli kawatandika Iran, lakini nao wamemtandika vibaya mno. Mara ya mwisho kambi za kijeshi za Marekani zimelipuliwa hivi ilikuwa ni mwaka 1941 kule Pearl Harbour ambapo Japan aliua zaidi ya wanajeshi 2000. Jambo la kushangaza kulikuwa na silaha za ulinzi za kisasa kabisa kwenye hizo kambi kama THAAD na PATRIOT ambazo zilikuwa na mfumo bora kabisa wa rada duniani ambao umelipuliwa.

Mahoteli ambayo walikuwa wanakaa MAJASUSI na WANAJESHI wa Marekani yamelipuliwa. Mpaka sasa maswali ni mawili tu: Aidha Iran alikuwa amejipanga sana AU kuna mtu anamsaidia maana siyo jambo rahisi kufanya haya ambayo Iran amekuwa akifanya hasa kwenye kufanya mashambulio ya ulengaji bila kukosea (Precision Attack) ambayo hutegemea kwa sehemu kubwa mifumo ya satellite. Israeli nako yamewakuta, sehemu muhimu za kiusalama zinalipuliwa. Utapinga, utanuna, utabisha na kuleta hasara ila hii ndiyo hali ilivyo.

SASA IRAN ANAPAMBANAJE: Mwaka 2018 nakumbuka kuna uzi wangu nilifurumushiwa matusi na mabazazi na madunya wa humu ndani, nilioandika kuhusu dhana ya ASYMETRIC WARFARE. Dhana hii inafanya kazi pale ambapo taifa dogo au kikundi kidogo kinapambana na taifa kubwa. Lengo siyo kutaka kupambana CONVENTIONAL WARFARE, ila ni kumsababishia maumivu makubwa yule aliye mkubwa kiasi cha kufanya akimbie. Mfano halisi, ni USSR vs Mujahedeen au USA vs Vietcong.

Iran hana AIRFORCE kama USA na ISRAEL. Iran hana NAVY kama USA na ISRAEL. Iran alichokiamua ni kutengeneza FORMIDABLE ROCKET AND DRONE FORCE, ambalo lina uwezo wa kisasa kabisa kushambulia taifa lolote lile hapa duniani. Jambo ambalo wengi hatulifahamu ni kwamba Iran mbali na udhaifu wao mwingi, walianza kupambana na Marekani tokea mwaka 1979, na wameshuhudia USA akishambulia wenzake kama Iraq, Afghanistan, Libya na Venezuela. Unadhani ni wajinga ???

MADHARA ENDAPO VITA HAITAISHA MAPEMA:

Mosi
, The Aura of American Invincibility has been shattered before the world. Zile propaganda za kusema hakuna wa kumgusa Marekani hazipo tena. Iran katuonesha kwamba Marekani na Israel wanagusika. Hebu sasa fikiria, endapo Uchina ataamua kuvamia Taiwani, nani anaamini kabisa kwamba kambi za Marekani zilizopo South-Korea, Philippines, Japan na Guam zitakuwa salama, kama tu kambi kubwa za Marekani barani Asia zimelipuliwa juzi na jana na Iran, taifa ambalo halina nguvu kama Uchina. Kiukweli, Marekani alizichanga karata vibaya na yanamtokea puani.

Pili, Urusi atapata nguvu kubwa kutokana na bei ya mafuta kupanda. Saudi Arabia, UAE, Oman, Qatar na Bahrain wanaogopa kupitisha mafuta Mfereji wa Hormuz, ambao kwa siku mapipa milioni 17 yanapita. Vita ikiendelea hivi na Iran akafanikiwa kufunga kabisa mfereji, basi mafuta ya Ulaya na Asia itabidi yapatikane Urusi ambako kuna vikwazo. Juzi Vladmir Putin kasema anafikiria kusitisha kabisa kuuza gesi Ulaya. Sasa USA na EU watabakiwa na maamuzi kama haya: Ondoa vikwazo ili tupate nishati kutoka Urusi. Bahati mbaya wakiondoa vikwazo Ukraine ndiyo kwaheri.

Tatu, Urusi atapenda kulipiza alichofanyiwa Ukraine. Hii ndiyo tabia kuu ya Urusi. Niguse-Ninuke. Marekani akitingwa kule Iran, basi lazima atapunguza kuangalia Ukraine. Sasa itabidi silaha zote zinazozalishwa zienda Persian Gulf (Ghuba ya Uajemi) siyo Ukraine. Urusi na Uchina wanaweza kuigeuza Iran, VIETNAM 2 endepo Marekani akiendelea hivi bila kuomba msamaha. Bahati mbaya sana kwa alichokifanya Donald Trump, Marekani ikirudi nyuma kama kipindi cha Twelve Days War mwaka 2024, basi ndiyo mwisho wa siasa za MAGA na Trump, na anaweza kufungwa kwasababu ameanzisha vita bila kibali cha Bunge.

Nne, mpaka sasa SECURITY DIPLOMACY ya Marekani imekufa. Ameingia makubaliano ya ulinzi na Saudi Arabia mwaka 1971, na mataifa kama UAE, Qatar na Bahrain kwamba wakitumia Dollar kuuza mafuta basi atawalinda. Bahati mbaya wanapigwa na Iran, wanaomba kuuziwa silaha na msaada wa kijeshi lakini bado hawajapata, kipaumbele chake ni Israel na kambi zake. Hii ndiyo vita kubwa ya kipropaganda ambayo Marekani hawezi kuishinda, endapo hatawalinda Saudi Arabia, UAE na Qatar dhidi ya Iran. Ujumbe utakuwa ni kwamba, kama Marekani ameshindwa kuwalinda UAE, Qatar na Saudi Arabia dhidi ya taifa dogo kama Iran, ataweza kweli kuwalinda Japan, South-Korea, Philippines na Australia dhidi ya taifa kubwa kama Uchina ???

Tano, THE COLLAPSE OF THE LAW OF NEUTRALITY. Katika sheria za kimataifa hasa wakati wa vita, The Law of Neutrality huyalinda mataifa ambayo hayapambani moja kwa moja, hata kama yanakuwa yanauza silaha kwa adui au kuwa na kambi za kijeshi ambazo hazitumiki kijeshi kushambulia adui. Kitendo cha Marekani kuvamia Iran bila sababu ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Hata Iran kuanza kuvamia Saudi-Arabia, UAE na Qatar ni uvunjifu wa sheria za kimataifa. Lakini Marekani hawezi kulalamika katika hili kwasababu yeye ndiye mvunjifu sugu wa sheria za kimataifa. Sheria za kimataifa ili zifuatwe na mataifa madogo, inategemea sana mataifa makubwa.

Hili lisipoangaliwa sana, tutaamka siku na kukuta Urusi kaanza kulipua Poland na Ujerumani kisa tu kuna kambi za jeshi za Marekani, hata kama hazitumiki kushambulia. Huku ndiko tunaelekea. Hivyo tukishafahamu haya, vitaifa masikini kama Tanzania vijiepushe na tabia za kupenda kujipendekeza kwa mataifa makubwa kama Uchina, Urusi na Marekani. Dunia inaelekea kubaya na kama tukitaka kuvuka itabidi kweli tusifungamane na upande wowote. Sasa wale wanopenda pesa za waarabu kisa ni wenzetu katika IMANI wakiendeleza tabia zao za kusajili manowari kule Zenji, wataliletea hili taifa matatizo makubwa mno. Tena kipindi hiki ukipigwa huna pakusemea maana kila mtu anapambana lwake.

==============================================================================

HALAFU KUNA MABAZAZI mengine yanasema INTERNATIONAL LAW IMEKUFA, haya nitayajibu baadaye.HAYANA AKILI

Kweli waliokukashifu wapo sahihi!!
Urusi iliivamia Ukraine October 2026!
Kweli wewe ni kilaza mkuu!!
 
Jmn kama haupo vizuri kichwan kwenye huu uzi usichangie...mnakula za uso vibaya mno 🤣

Wacheni mihemko ya umarekan wa buza.

MALCOM...Tuendee baba.
Kuna hili lifala linaitwa let the caged bird sings ni moja kati ya Mabazazi na Madunya ya humu ndani. Limetoka shimoni baada ya maumivu makali ya moyo, likaharisha ujinga halafu likaenda kuvimbiwa futari ya Kwaresma.

Lenyewe na wenzake wengi humu ndani niliwahi kuwaambia mwaka 2022 kwamba muda ni mwalimu mzuri sana, wekeni akiba ya maneno. Katika wooote ambaye huwa hajawahi kunivunjia heshima kwenye mijadala ni mdogo wangu T14 Armata , atabishana na mimi vikali ila hajawahi kubisha kitu bila walau kuweka hoja. Katika hili namheshimu sana sanaaa.

Mengine sasa hivi yanachungulia yanapita kimyakimya kama mapepo yakitegemea walau CNN watangaze chochote kibaya kilichowakuta Iran ili wakilete hapa, lakini wapiiiiii. Mimi niko nao tu hawaa Weekend yote hiiiii
 
Jmn kama haupo vizuri kichwan kwenye huu uzi usichangie...mnakula za uso vibaya mno 🤣

Wacheni mihemko ya umarekan wa buza.

MALCOM...Tuendee baba.
Hii vita haipaswi kuwa ya kishabiki ukitaka kuona athari zake angalia tangazo la EWURA hata wiki halina just image vita hii iende mpaka one month,hakika nakuambia hakuna rangi tutaacha kuona hapa nchini.

Ndo maana Mleta Uzi amewaita Mabazazi na Madunya kwamba hawaoni kwamba hili ni tatizo kubwa,bali wao ni ushabiki kama wa Simba na Yanga.
 
Marekani hakwenda Vietnam kupeleka Ubepari bali alikwenda kutengeneza koloni akashindwa. Vietnam (Indochina) lilikuwa koloni la Mfaransa na alivyotoka Marekani akataka kwenda yeye ila bahati mbaya kina Stalin walikuwa washamuwahi. Kafika kakuta Wakomunisti wako tokea mwaka 1930 na wamesoma Urusi, huku wengine wakiwa veterans wa WW2.

Pili, Vietnam siyo taifa la Kibepari (A Capitalist Economy) ni taifa la Kikomunisti (A Communist State) ambalo limeruhusu mfumo wa masoko uliodhibitiwa (Controlled Market) kama Uchina. Kilichobadilika Vietnam ni umiliki wa mali tu na masoko. Siasa na Utawala ni uleule tokea 1930 chini ya Comrade Ho Chi Minh.
Marekani ilienda Vietnam kuzuia domino theory na kuisaidia serikali ya South Vietnam chini ya Rais Ngo Dinh Diem. Same way na Marekani ilivyoamini kwenye domino theory ikapeleka majeshi South Korea kuisaidia kupigana na North Korea iliyoungwa mkono na China na USSR.

Hilo la Marekani kutaka kuanzisha ukoloni Vietnam hongera kwa kulijua, hata Wamarekani wenyewe hawalijui.
Kwahiyo na kule South Korea, Marekani ilianzisha ukoloni?
 
Hapa unalinganisha tembo na mbuzi kwenye uzito.

Russia imetimiza miaka minne tangu ianzishe mashambulizi dhidi ya Ukraine. Kwa kutumia vifaru, wanajeshi, helicopters, meli za kivita, bombers, fighter jets, submarines, missiles zikiwemo cruise, ballistic na hadi hypersonic, na silaha nyinginezo.

Marekani imeshambulia haina boots on ground, haina kifaru hata kimoja, inatumia missiles, ndege na meli sina hakika kama wametumia submarines mpaka sasa. Tofauti zao sasa:

1. Russia ina miaka minne (4), US haijatimiza mwezi.

2. Russia haijawahi miliki anga la Kiev, wala ndege yake kukatisha anga hilo walau mara moja katika miaka yote minne. US siku ya kwanza tu ndege zake zilifika Tehran na kila siku zinafika zinakotakiwa kufika popote ndani ya Iran. Ndoto kama hii kwa Russia haiwezekani.

3. Russia haijawahi muua mkuu wa majeshi, wala Rais, wala mkuu wa Air force, au wa Navy, au wa Army ya Ukraine. Upande wa Marekani hapa sitaji nitakukumbusha machungu.

4. Iran haijamuua General yeyote wa US, Ukraine imeua Russian Generals zaidi ya 15 kwenye mapigano.

5. Iran hajawahi shambulia mainland US. Wakati Ukraine anashambulia hadi ikulu ya Kremlin ya Urusi.

Hizo ni tofauti kubwa, mengine ni vita zina mambo yake. Ila aliyekutaarifu kuwa Marekani ameshindwa kummaliza Iran "kwa haraka" sijui ni nani.
Kwa hiyo mkuu Iran na Marekani wangekuwa wanashea mpaka kama ilivyo kwa Urusi na Ukraine makombora na drone za Iran zisingekuwa zinapiga kwenye miji ya Marekani?
Ila ni kweli hatakiwi kulinganisha maana Ukraine ilivamiwa na Urusi peke yake lakini Iran kavamiwa na mataifa mawili.
 
Marekani ilienda Vietnam kuzuia domino theory na kuisaidia serikali ya South Vietnam chini ya Rais Ngo Dinh Diem. Same way na Marekani ilivyoamini kwenye domino theory ikapeleka majeshi South Korea kuisaidia kupigana na North Korea iliyoungwa mkono na China na USSR.

Hilo la Marekani kutaka kuanzisha ukoloni Vietnam hongera kwa kulijua, hata Wamarekani wenyewe hawalijui.
Kwahiyo na kule South Korea, Marekani ilianzisha ukoloni?
America is not the Universal Munificent Santa Clause....

Joe Biden na Donald Trump wamekuwa na sifa moja inayofanana tofauti na maraisi wengine wa Marekani waliotangulia. Wamejisemea ukweli kwamba Marekani iko Ukraine kwasababu ya rasilimali na Marekani ilitengeneza Israel na inailinda kwasababu ni uwekezaji wao mkubwa....

Sasa ndugu yangu Armata, nikuulize swali kama lengo la Marekani lingekuwa ni kupambana na Ukomunisti, kwanini Marekani huyohuyo alikuwa anawaunga mkono madikteta wa kikomunisti kama Pol-Pot wa Cambodia, au Tito wa Yugoslavia ???
 
Back
Top Bottom